ABC ZA 2025
JF-Expert Member
- May 2, 2018
- 1,381
- 869
Baada ya David Kafulila kusimama na kuanza kumtetea Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ufasaha na weledi unaostahili kwenye mambo mbalimbali, Kitendo hiki kimeibua kundi linalomuunga mkono Rais Samia pamoja na David Kafulila mwenyewe.
Sayansi ya siasa inasema kwenye uwanja wa kisiasa ni kosa kumpuuza mtu yotote hasa mwenye record za wazi kama ilivyo kwa David Kafulila leo na record zake za Tegeta Escrow.
Limezuka pia kundi kinzani hasa toka Upinzani, hawataki kusikia David Kafulila akitajwa kwa jema lolote kisa tu aliwakimbia na kurejea chama mama cha Mapinduzi CCM wakati akitekeleza moja ya haki zake za kikatiba za kuwa katika chama chochote Cha siasa anachokipenda.
Wapo pia wanaosema kila anayemtaja David Kafulila hapa Jf basi ni yeye mwenyewe David Kafulila, Kwa lugha rahisi wanamaanisha David Kafulila anajipigia debe hawa pia wanahitaji kujipa muda na kufuatilia kwa makini kama nilivyofanya Mimi.
Swali langu kwao, Kama hawa wote wanaomtajataja Kafulila hapa, hao ni Kafulila wenyewe au wanatumwa na Kafulila Je, Yale makofi aliyopigiwa Kafulila pale Bungeni mpaka Spika akayasitisha kibabe alikuwa pia ni yeye Kafulila mwenyewe akijipigia Makofi hayo? kama sivyo, kwani hao Wabunge waliompigia makofi bungeni wao humu Jf hawaruhusiwi kuwepo au kujiunga?
(nitaomba mwenye ile clip ya Kafulila Bungeni anipatie inbox)
Nimejipa muda wa kufanya utafiti hasa hapa Jf na huku mitaani nimeridhika kuwa David Kafulila ni tishio huko mbeleni kama tu Mungu atampa uhai na afya njema kwani ni kweli Watanzania wanataka kijana ambae anaaminika, kijana ambae anachukizwa na rushwa pamoja na ufisadi mwenye kaliba ya David Kafulila.
Naomba na Mimi nitumie haki yangu hii ya kikatiba ya kutoa maoni yangu.
soma pia haya maoni Je, ni nani kati ya hawa 10 anasifa za ziada za kuwa Mrithi wa Rais Samia atakapomaliza kipindi chake?