Kinyume kabisa, umeweka msumari wa nguvu kubwa kwenye hoja. Ninaishi Tanzania lakini nimejaliwa kusafiri sana sehemu mbalimballi duniani. Nakutana na watanzania. Wengi wao niliwafahamu kabla, wazazi wao kama wa kwangu na shuleni walikuwa wazuri tu. Lakini wakaja Ulaya and by default wakaanza kuonja huduma hizi unazoziita first class, lakini kumbe siyo wala. Hawawezi kupata huduma first class hawa hata mara moja ila huduma wanazopata zinazidiana ubora na za pale nyuumbani. Wapo Wasomi wazuri wanataaluma wanafanya kazi za ajabu, ashakum si matusi(sijui wanaisema hivi!) nimeona Engineers, Accountants wanafanya kazi za kuwalisha wazungu wazee, wanafajia, wameajiriwa na watu ambao hawajaenda shule kabisa.
Wanaishi maisha ya kubabaisha. Na wengi wao ni kama omba omba wanapokutana na sisi tunaopita pita. Sasa Mzee wapate huo mshahara wa mwisho wa mwezi, acha bwana ni hizo party unazozisema. Call them anything. Kwa maana halisi ni rahisi hawa kushabikia viongozi wa CCM na wakati mwingine kutaka kuwa karibu na Balozi zetu kama sehemu ya hifadhi. NINAJUA SIO WOTE wanafanya hivi, lakini ni namna ya wale wenye uchovu kutafuta kinga.
Ushauri wangu na hasa kwa hawa ambao wana taaluma (maana wasio na taaluma ni kibao, nadhani SA ni wengi, lakini naona Sweden, Denmark, USA na UK nao ni wengi) WARUDI tuje tusaidiane kuendesha taasisi zetu hasa vyuo ambako kuna uhaba mkubwa kweli wa wakufunzi. Kuna ambao wamerudi na wanang'ara sasa hivi, mifano ni mingi