Watanzania tusidanganywe hakuna kodi ya trilioni 1.4 iliyokusanywa

maramia

JF-Expert Member
Jul 17, 2015
2,030
1,344
Kuna uwezekano mkubwa kwamba serikali inatudanganya kuhusu makusanyo ya kodi ya shilingi trilioni 1.4 kwa mwezi Januari 2016 pekee na kujinasibu kwamba imevuka kusanyo lolote la kodi lililowahi kukusanywa katika kipindi cha mwezi mmoja.

Ninachoamini ni kwamba hakuna kusanyo lolote hapa la kushangaza wala kujitapia kwamba TRA imevunja rekodi kwa kukusanya kodi kubwa kwa mwezi mmoja, isipokuwa wasiojua wanapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.

Ilichofanya serikali ni kukusanya kodi ya nyuma iliyokuwa inakwepwa kulipwa kwa makusudi na uzembe kama ile ya makontena na kuirundika yote kwenye mwezi wa Januari na kuwadanganya watanzanzania kujitafutia sifa.

Kama kweli lengo limevukwa ebu hawa wanaojitapa watupe ushahidi na watuambie ni vyanzo gani vipya vya kodi vya uhakika walivyobuni kama si vile vile vilivyokuwepo, isipokuwa fedha nyingine iliyoongezeka ni arrears za miaka na miezi ya nyuma walizokuwa hawazikusanyi kwa maslahi yao binafsi na wakwepa kodi wengine.
 
Inawezekana vyanzo ni vilevile lakini wameimarisha ukusanyaji wake na wamedhibiti ukwepaji.
Ndo wanachofanya kwa sasa. Wanaimarisha vyanzo vikuu vya mapato na kuviboresha. Mfano mzuri ni hii ya polisi wa usalama wa barabarani kupewa mashine za max malipo za kukusanyia kodi.
 
Kuna mbunge Jana alisema wanakusanya arrears tu na si kodi.
Arrears inaitwaje? labda angeweka vizuri hoja yake. Ana maanisha arrears ya mishahara ama pango la nyumba? Mbona kila kitu kizuri serikali inafanya tunaishia kukebehi?????? Je wasingekusanya arrears tungewaitaje???? kuweni na ufahamu si kila wapinzani wakisema tuawafuate na vise versa chama tawala wakisema tufuate bila kutumia uwezo wa akili zetu ambazo tulipewa bure bila kununuliwa na mtu.
 
Ndo wanachofanya kwa sasa. Wanaimarisha vyanzo vikuu vya mapato na kuviboresha. Mfano mzuri ni hii ya polisi wa usalama wa barabarani kupewa mashine za max malipo za kukusanyia kodi.
Zile mashine unajua ni za nini au ndo unakurupuka tu
 
Kuna uwezekano mkubwa kwamba serikali inatudanganya kuhusu makusanyo ya kodi ya shilingi trilioni 1.4 kwa mwezi Januari 2016 pekee na kujinasibu kwamba imevuka kusanyo lolote la kodi lililowahi kukusanywa katika kipindi cha mwezi mmoja.

Ninachoamini ni kwamba hakuna kusanyo lolote hapa la kushangaza wala kujitapia kwamba TRA imevunja rekodi kwa kukusanya kodi kubwa kwa mwezi mmoja, isipokuwa wasiojua wanapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.

Ilichofanya serikali ni kukiusanya kodi ya nyuma iliyokuwa inakwepwa kulipwa kwa uzembe wake na kuirundika yote kwenye mwezi wa Januari na kuwadanganya watanzania ili sifa zimwendee mheshimiwa Rais.

Kama ukweli si huo ebu hawa wanaojitapa watupe ushahidi na watuambie ni chanzo gani kipya cha kodi walichobuni kama vyanzo si vile vile vilivyokuwepo, fedha nyingine iliyoongezeka ni arrears za miaka na miezi ya nyuma walizokuwa hawazikusanyi kwa maslahi yao binafsi na wakwepa kodi wengine.



Swali ni kwamba Je, zaidi ya trilioni 1.4 zimekusanywa kwa mwezi Janauri au la?
Na haijalishi hizo kodi zimetokea wapi lkn mwisho wa siku cha muhimu ni kwamba mwezi Januari Serikali yetu imekusanya shilingi zaidi ya trilioni 1.4 ambazo zitatumika kwenye mambo ya maendeleo hilo ndiyo muhimu, mengine yote ni blah blah zako tu!
 
Kuna uwezekano mkubwa kwamba serikali inatudanganya kuhusu makusanyo ya kodi ya shilingi trilioni 1.4 kwa mwezi Januari 2016 pekee na kujinasibu kwamba imevuka kusanyo lolote la kodi lililowahi kukusanywa katika kipindi cha mwezi mmoja.

Ninachoamini ni kwamba hakuna kusanyo lolote hapa la kushangaza wala kujitapia kwamba TRA imevunja rekodi kwa kukusanya kodi kubwa kwa mwezi mmoja, isipokuwa wasiojua wanapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.

Ilichofanya serikali ni kukiusanya kodi ya nyuma iliyokuwa inakwepwa kulipwa kwa uzembe wake na kuirundika yote kwenye mwezi wa Januari na kuwadanganya watanzania ili sifa zimwendee mheshimiwa Rais.

Kama ukweli si huo ebu hawa wanaojitapa watupe ushahidi na watuambie ni chanzo gani kipya cha kodi walichobuni kama vyanzo si vile vile vilivyokuwepo, fedha nyingine iliyoongezeka ni arrears za miaka na miezi ya nyuma walizokuwa hawazikusanyi kwa maslahi yao binafsi na wakwepa kodi wengine.

MIMI NAKUBALIANA NA HOJA
 
Back
Top Bottom