Watanzania tukimtumia vizuri Waziri Mwijage China watasubiri!

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,746
109,187
Na hili lazima niliseme ukweli bila kupepesa, kutikisa wala kumung'unya kuwa katika Mawaziri ambao nadhani Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ' amepatia ' katika kumteua ni Waziri wa Viwanda Mheshimiwa Charles Mwijage.

Katika kumfuatilia kwangu kwa marefu na mapana yake yote nimegundua kuwa kwa aina ya uwezo wake mkubwa wa ' kupambanua ' mambo, uzoefu wake na commitment yake kama Watanzania tutamtumia vilivyo nina uhakika muda si mrefu tunaweza kuwafukuza akina Malaysia, Singapore, UAE na hata China katika maendeleo ya Viwanda.

Tuache Siasa zetu za ' maji taka ' tulizonazo na zinazotupotezea muda na tumpe ' ushirikiano ' huyu Waziri wa Viwanda Mheshimiwa Mwijage na kuna siku Tanzania ' tutaheshimika ' Kiviwanda. Na nitoe tu Wito tena kwa Mawaziri wengine kuwa hebu jifunzeni kitu kutoka kwa Waziri Mwijage kwani yeye hazungumzi tu ' blah blah ' bali ' anatenda ' na kuna indicators za kutosha kuwa kwa muda mfupi tu aliokuwa ' madarakani ' Tanzania tumeanza kusogea kwenda huko tunakokutaka katika Tanzania ya Viwanda.

Hongera sana Waziri wa Viwanda Charles Mwijage na nina imani kubwa na Wewe na hakika Tanzania ya Viwanda itakuwa kweli. Kila la kheri.

 
Naona anaufundi wa kuongea kweli/ kama mulongu.../ they how to capture ppl attentions/ while the days go by!..
 
Unachosema no kuwa mheshimiwa Rais hakipatia mawaziri wengi wengine. Ila hujatueleza kikubwa cha kipekee alichokifanya huyu ndugu
 
Kuna wengine wanafanya kazi General Tire wanachukuwa Mshahara Kiltex....hao ni Hewa au mishahara ndiyo hewa...halafu status zao ni za juu ile mbaya.No wonder hata wenzi wao wanawadhalilisha maofisa wetu wapendwa.
 
Shida ya Waafrica/Watanzania badala ya kuunda vyombo vyenye kupanga mikakati ya kimaendeo kwa kuzingatia kipaumbele, tunaabudu watu, yaani mtu mmoja awe Rais, Waziri nk anaweza kufanya maamuzi pekeyake ya kuwaathili watu zaidi ya Milion 45

Inapashwa kubadirika kwa kweli, maamuzi ya nchi yafanywe na watu na sio Mtu mmoja tu
 
Na hili lazima niliseme ukweli bila kupepesa, kutikisa wala kumung'unya kuwa katika Mawaziri ambao nadhani Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ' amepatia ' katika kumteua ni Waziri wa Viwanda Mheshimiwa Charles Mwijage.

Katika kumfuatilia kwangu kwa marefu na mapana yake yote nimegundua kuwa kwa aina ya uwezo wake mkubwa wa ' kupambanua ' mambo, uzoefu wake na commitment yake kama Watanzania tutamtumia vilivyo nina uhakika muda si mrefu tunaweza kuwafukuza akina Malaysia, Singapore, UAE na hata China katika maendeleo ya Viwanda.

Tuache Siasa zetu za ' maji taka ' tulizonazo na zinazotupotezea muda na tumpe ' ushirikiano ' huyu Waziri wa Viwanda Mheshimiwa Mwijage na kuna siku Tanzania ' tutaheshimika ' Kiviwanda. Na nitoe tu Wito tena kwa Mawaziri wengine kuwa hebu jifunzeni kitu kutoka kwa Waziri Mwijage kwani yeye hazungumzi tu ' blah blah ' bali ' anatenda ' na kuna indicators za kutosha kuwa kwa muda mfupi tu aliokuwa ' madarakani ' Tanzania tumeanza kusogea kwenda huko tunakokutaka katika Tanzania ya Viwanda.

Hongera sana Waziri wa Viwanda Charles Mwijage na nina imani kubwa na Wewe na hakika Tanzania ya Viwanda itakuwa kweli. Kila la kheri.
Weka indicators
 
Tatizo la viongozi wengi ni kutekeleza wanayoyasema huyu waziri ukimsikiliza unaweza ukasema waziri ndiyo huyu ila kwenye utekelezaji sasa ndio unaowaangusha Na bajeti pia zinamwangusha
 
Hamna bomu kama yule.Tararira kibao wakati hajui viwanda vinaaishwaje. Debe tupu tu kama kawaida. Kuna mtu aliyejuwa viwanda kitendo kama JK.Nyerere?

Wenye akili walimsikiliza tunapata kichefu chefu
 
Acha uongo mnachojua ni kusifia na visivyostahili?Watanzania tunataka kuona"deeds not words".
 
Hivi Simbachawene yupo kweli?? huyu Mwijage naona kama anafananafanana na Simbachawene kwa sound na tantalila. USIMUAMINI MTANZANIA AKISEMACHO, MUUMINI SIKU AKITEKELEZA AKISEMACHO...
 
Back
Top Bottom