Andrew Nyerere, ni vigumu sana baadhi ya watu kukuelewa. Si Tanzania pekee inayohitaji sana physics bali ni Afrika nzima, isipokuwa hata hiyo physics inayofundishwa hapa kwetu haiwezi kuleta mapinduzi ya technolojia kwa sababu wanafunzi wanafundishwa historia ya sayansi. Hivi unafikiri, itawezekana kwa nchi kama yetu hii ambayo walimu wanawafundisha wanafunzi kufoji practical? Tunahitaji kwanza mtazamo mpya juu ya masomo ya sayansi. Isiwe huu mtazamo tulionao wa kuwafundisha wanafunzi ili wafaulu mitihani. Wakati wenzetu leo wanapambana na jinsi ya kumlaza binadamu kwa siku 180 kwa ajili ya kupunguza gharama za safari ya kwenda Mars sisi hata baloon tu hatujawahi tengeneza.
Magufuri uliyemtaja sidhani kama ana mpango wowote na teknolojia, nikimtazama namuona kasinzia usingizi wa pono. Ukitoa Afrika kusini, nchi nyingi za Afrika haziwazi kuendelea kwa teknolojia nchini mwao. Tutaendelea tu ku-import technology.