Watanzania tuamke usingizini na tuseme sasa basi

Watanzania tuamke usingizini na tuseme sasa basi

Mantuntunu

Senior Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
137
Reaction score
16
​Naomba nianze kwa kuwashukuru wapinzani na wanaharakati wengine ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kutujuvya maovu na ufisadi mwingi ambao umekuwa ukijitokeza Mara kwa Mara, Kuanzia old IPTL ya kina Chenge mpaka Escrow, Kiwira, Epa, mabilioni ya Uswiss, radar, Richmond, n.k. Lakini inakatisha tamaa kuona watanzania hakuna lolote tunalolifanya zaidi ya kulalamika kwenye mitandao, when are going to Say enough is enough???? Wakati ndio huu aw kufanya maamuzi magumu

Hawa viongozi wanafanya wanavyotaka kwa sababu wana watz hakuna lolote tutakalofanya, we are sitting back and let them do what ever they want to do, hii Escrow ndo imeua kabisa.

Mimi ni mmojawapo wanaoamini kuwa mtu mkubwa anajua sana na amehusika kwa namna moja au nyingine kuruhusu Escow na hili halina ubishi. The question is what are going to do about it??

Mimi nasema hili, kuwawajibisha waliohusika sawa lakini hivi mnategemea kutakuwepo na jipya? Hakuna lolote na mmeishaona mifano. Dawa Yao ni kuiondoa hii sirikali madarakani it has proven failure mara zote. Let's take them out of the office, NDUGU ZETU POLISI MLIOZOEA KUPIGA NA KUUA WATU njooni tuungane na tuseme BASI, ninaamini kabisa kuwa hata nyie haya yanayofanyika hamyapendi.

TANZANIANS LETS SAY ENOUGH IS ENOUGH ..! TIME IS NOW, LETS NOT BE COWARDS..!
 
Nikweli lakini nivizuri unge dadavua lengo hasa la uzi huu kama tuingie barabarani na kuandamana au? Na kama tukiandamana tuanzie wapi na tumalizie wapi
Nakama tukiandamana tumejipanga vp na Policcm
Kiukweli mm niko tayari kuanzisha maandamano yoyote yale yanayopinga ufisadi na niko tayari kwa lolote kufa au kupona
Kwani watakaoumia zaidi ni sisi na vizazi vijavyo.
 
The last three months nilienda kansia fulani la kilokole, ni kubwa, walipomaliza kuhubiri nikaona mchungaji anasema "tuombee nchi na serikali" wakaomba wee wakamaliza, mi sikuomba kabisa kwani niliona kaman aiombea ccm.

nikaondoka sikurudi tena hapo church, nikaenda lingine nikakuta wanamwombea kikwete apone kwani wamesikia ameenda kutibiwa kansa ya maeneo fulani...wakaombe mi sikuomba kwasababu simpendi kikwete kabisa na ninajua wanachowafanyia watz huko kwenye ccm ndio maana siwatakii mema kabisa nawaona ni maadui. wakaomba wakamaliza.

leo nikaenda kanisa lilelile, ni kubwa sana, nilichokikuta kimenifurahisha moyo, hawaombei kikwete tena, pamoja na kwamba wamegusia kwamba kikwete ametolewa nyuzi, nilichosikia kwamba tuombee ni WALIOIBA PESA WOTE WAKAMATWE NA MUNGU AWAHUKUMU hata kama serikali haitawahukumu. huwezi amini, mchungaji ametamka kwa kinywa chake kuwa waumini wengine wanakuja hapa wamevaa kandambili hawana hata hela wamekunja nyuso za huzuni ya kukosa pesa wakati kuna watu serikalini wanaiba hela tu. nikagundua kumbe pastor sijui alikutana na nani kujadili. niliporudi kumpigia jamaaangu aliyenishawishi kusali lile kanisa la mwanzo na yeye anasema leo wamehubiri hivyohivyo...nikajua kumbe kampeni zimeshaanza watu wanaelimishwa kuanzia makanisani hadi misikitini kujua namna serikali inavyowafanya wawe na maisha magumu. sipati picha uchaguzi wa mwakani, hapatatosha. leo kwakweli nimefurahi.
 
​Naomba nianze kwa kuwashukuru wapinzani na wanaharakati wengine ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kutujuvya maovu na ufisadi mwingi ambao umekuwa ukijitokeza Mara kwa Mara, Kuanzia old IPTL ya kina Chenge mpaka Escrow, Kiwira, Epa, mabilioni ya Uswiss, radar, Richmond, n.k. Lakini inakatisha tamaa kuona watanzania hakuna lolote tunalolifanya zaidi ya kulalamika kwenye mitandao, when are going to Say enough is enough???? Wakati ndio huu aw kufanya maamuzi magumu

Hawa viongozi wanafanya wanavyotaka kwa sababu wana watz hakuna lolote tutakalofanya, we are sitting back and let them do what ever they want to do, hii Escrow ndo imeua kabisa.

Mimi ni mmojawapo wanaoamini kuwa mtu mkubwa anajua sana na amehusika kwa namna moja au nyingine kuruhusu Escow na hili halina ubishi. The question is what are going to do about it??

Mimi nasema hili, kuwawajibisha waliohusika sawa lakini hivi mnategemea kutakuwepo na jipya? Hakuna lolote na mmeishaona mifano. Dawa Yao ni kuiondoa hii sirikali madarakani it has proven failure mara zote. Let's take them out of the office, NDUGU ZETU POLISI MLIOZOEA KUPIGA NA KUUA WATU njooni tuungane na tuseme BASI, ninaamini kabisa kuwa hata nyie haya yanayofanyika hamyapendi.

TANZANIANS LETS SAY ENOUGH IS ENOUGH ..! TIME IS NOW, LETS NOT BE COWARDS..!

Mfano upo Burikana Faso copy n paste.....wasipomtoa Mhongo/werema mkamchomoe dodoma mjengoni....
 
Hata mimi msikitini kwetu habari ndo hiyo, hatufagilii ujinga aithee!
 
Nikweli lakini nivizuri unge dadavua lengo hasa la uzi huu kama tuingie barabarani na kuandamana au? Na kama tukiandamana tuanzie wapi na tumalizie wapi
Nakama tukiandamana tumejipanga vp na Policcm
Kiukweli mm niko tayari kuanzisha maandamano yoyote yale yanayopinga ufisadi na niko tayari kwa lolote kufa au kupona
Kwani watakaoumia zaidi ni sisi na vizazi vijavyo.

Mdau whichever way alimradi Sirikali hii iondoke, njia yoyote ile haijalishi, Mimi na wewe sidhani Kama itakuwa na impact, nobody knows us, tunahitaji wasomi, waandishi SA habari, madaktari, waalimu, watu maarufu then sasa ndio waongezeke wanasiasa, kuna watu wakimwona mtu Kama Maria Tsarungi, Jenerali Ulimwengu, ppeople like Kubenea, wanaandamana hawatasita kujiunga isiwe Kama ni issue ya upinzani tu, iwajumuishe watu Kama hao. I think it will make sense, that is my opinioted opinion
 
We are tired! Wananchi suffer the most! Cost of living is just sky rocketing!
 
Kufichuka kwa wizi Wa Escrow kumeendelea khthibisha kuwa Tanzania ni Shamba la bibi, yeyote mwenye uwezo ajichukulie atakavyo. Serikali imepoteza nguvu zake na sasa imegeuka kuwa genge la wapigaji.

Serikali ndio chanzo cha viongozi wake kujichotea pesa za umma kwa sababu hakuna mdhibiti. Hapo awali nafasi ya mwanasheria Wa Serikali ilikuwa na heshima lakini toka Andrew Change alivyoitia Najisi amefungua milango kwa wanaomfuata nao kuwa wezi.
 
Kuna tatizo limezuka ambalo hili lina athiri shughuli za kuiondoa CCM madarakani kwa kuwa tu CCM inatumia ile sheria ya wagawa uwatawale ,tumeona hadi leo kule kunakotokea vurugu huwa kama wamelogwa ,hawaelewani na wakizidiwa utasikia kama hamtufanyii hili tutaludisha kadi za CCM.

Hivi miaka yote watu hawa hawajasoma na kuelewa kuwa CCM sio chama kitakachowaletea maendeleo na badala yake ni kuwadumaza tu ,maisha yote wapo palepale kwenye kukogombana kuuwana.

Hivi hawajaelewa kuwa Miiccm huenda kule vijijini na kuwadanganya kwa maneno ya kuwalisha pipi kisha wakawaacha kama walivyo na baada ya siku mbili tatu hurudiana kuuwana ,hawaelewi kuwa sababu ya yote hayo ni kuwa serikali inayoongozwa na CCM haina ukweli zaidi ya udanganyifu ,leo anazuunguka Kinana na mapauro na mifuko ya sementi akipita akiwalaghai wananchi na kuwazuga ,yote ni kuwa uchaguzi umekaribia.

Nafikiri ipo haja ya upinzani kuwaonya wananchi kuwa watapita watu humu na mifuko ya saruji ,mapauro na majembe begani ,wawashitukie na mapema na kuwaepuka ,ila wachukue sementi ,mapauro na majembe hayo wasiyaache. Kwani watu hao hupita siku kama hizi zinazokaribia uchaguzi ili kuwalaghai na baada ya hapo hawatawaona tena.

Utaona watu wakishakorofishana na Miccm hutishia kurudisha kadi ,ujasiri wa aina hiyo sio unaotakikana na sio upinzani wa kweli ni kujidanganya na wewe kuendelea kudanganywa.

Unapoikataa CCM ikatae kwa lolote lile ,ikatae kwa kila kitu chao ,ikatae kwa kila neno watakalo kwambia ,kwani hawana la ukweli zaidi ya ulaghai ,mnaona wanavyogawana hela ,mabilioni kwa mabilioni ,yaani mbali ya mishahara mikubwa bado hawaridhiki ,wanaiba hata hela za kuwaletea wananchi maendeleo,watu gani hao wa kuwaamini na kauli zao wanazopita nazo vijijini ?

Tumeona juzi eti wanatoa zawadi kwa walipa kodi wazuri ,sherehe zile sio wawafurahia wale walipa kodi bali wanaifurahikia ile hela iliyoingia watapata mgao mzuri ,kwani kodi zinalipwa ila hakuna kinachoonekana kinafanyika kutokana na kodi hio ,hao wakulima na wafugaji kila siku wanalipa kodi kwa mazao yao,mashambayao mifugo yao lakini matatiz yao hakuna aneyashughulikia ,kwa maana miccm haiwajali isipokuwa inapokwenda kukusanya kodi kwa polisi na mgambo,uone ni jinsi gani watu wanawakimbia ndani ya nchi yao.

Vyama vya upinzani viweke mikakati ya kufuta hizi kodi za dhulma ,kodi ambazo nchi nyinegine huzisikii kutajwa isipokuwa hapa Tanzania tu.

Msitishie kurudisha kadi ,rudisheni kadi kwa uhakika hivi mnaogopa kitu gani ?
 
Kuna kila dalili kwamba CCM wamelenga kuitumia skandali ya Escrow inayowaandama kama kete ya kushinda kirahisi uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Tathmini niliyoifanya tangu skandali hii ishike kasi hapa nchini inaonyesha kwamba vyama vya siasa na wanachi walio wengi wameelekeza macho na masikio yao kwenye skandali hii kuliko kujielekeza kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao. Hata UKAWA na wafuasi wao nao wameingia mkenge na kujikuta wakitumbukia kwenye mtego huu wa CCM.

Tathmini yangu inaonyesha kwamba hivi sasa CCM wanawatumia makada wao kwenye ngazi za Kata kujipanga kuchakachua matokeo ya uchaguzi huu kuanzia kwenye uandikishaji wa wapiga kura hadi siku ya kupiga, kuhesabu na kujumlisha kura. Leo nimetembelea vituo 15 vya uandikishaji wapiga kura na kati ya vituo vyote hivyo ni vituo 5 tu ambavyo nimekuta vina mawakala wa vyama vya siasa, na wengi wao ni wa CCM. Katika vituo hivyo 5 vilivyokuwa na mawakala ni kituo kimoja tu ambacho kilikuwa na wakala wa UKAWA. Hapa ndipo CCM itakapoanzia kuchakachukua idadi ya wapiga kura na hatimaye kushinda kilaghai. Wakati CCM wakiwatumia makada wao wa ngazi za chini kuchakachua uandikishaji, wanaUKAWA wote wameelekeza nguvu zao kwenye skandali ya Escrow.

Ndio maana CCM wanajitahidi kurefusha hili sakata la Escrow ili wazidi kuwazubaisha UKAWA wakati wao wakiendelea na uchakachuaji kama kawaida yao. Mawakala wa vyama vyote wanapaswa kuwepo kwenye eneo la uandikishaji ili kuhakikisha kwamba wanachi wanaoenda kujiandikisha wanatoka kwenye Mitaa, Vijiji, au Vitongoji husika. Kuna kila dalili kwamba CCM wamejipanga kuchomekea mamluki na kuwaandikisha kwenye maeneo ambayo hawahusiki ili kujiongezea kura haramu na kushinda viti vingi zaidi kuliko UKAWA. Nitoe wito kwa makada wote wa UKAWA, hasa wa ngazi za chini muwe makini na ulaghai huu wa CCM ili kudhibiti aina yoyote ya udanganyifu unaofanywa na CCM. Msipofanya hivyo sasa hivi na kuwaachia CCM kuchomekea mamluki wao kwenye daftari la wapiga kura, ikafika siku ya kupiga kura poliCCM watawasaidia CCM kufanikisha mamluki hao kupiga kura hata kama mtawagundua siku hiyo.

WanaUKAWA msikubali kusubiri hadi siku ya mwisho ndipo mawakala wawazuie mamluki kupiga kura. Mtakuwa mmechelewa sana na hamtafua dafu mbele ya poliCCM wenye silaha za moto na mabomu ya machozi. Ni bora kuziba ukuta sasa kuliko kujenga ukuta.

Nawasilisha.

magamba wamepigika.jpg
:israel:
 
Mitaani ni vita wala usifikirie na wao wasifikirie kwamba tuko ule wakati wa piga tajama ,safari hii ni kufa na kupona ndugu.
 
Ukawa ni wajinga sana. Wakija kushtuka uchaguzi wa serikali za mitaa wameshindwa vibaya na sakata la escrow limeisha.
 
Ukawa ni wajinga sana. Wakija kushtuka uchaguzi wa serikali za mitaa wameshindwa vibaya na sakata la escrow limeisha.

Wajinga ni nyie mnaojidanganya mtatawala milele.
Hamuamini na hamtaki kuamini na mtabakia na historia yenu nyie kwa nyie
 
nimewahi kusoma makala kadhaa za waandishi wa kizungu ambao wenye ubaguzi uliopitiliza. Waaandishi hao walifikia kuhoji kama kweli bongo za waafrika zipo na kama zipo ni dhaifu kiasi gani ukiliganisha na wazungu.Wapo waliotoa vipimo kuthibitisha madai yao. Na pia wapo waliopiga mfano ya mambo ambayo wanafanya waafrika ambayo yanathibitisha bongo zao zilivyo. Ni ubaguzi wenye kuchukiza na unatakiwa kupigwa vita. Hata hivyo nami nimeanza kujiuliza hawa ambao wanaokipigia kura chama chenye kashafa zilizothibitishwa kama hichi kuanzia ndege rais richmond escrow nk kama kweli wenzetu hao bongo zao zinalingana na zetu na kweli zipo. Na hapo ndipo utaona kwanini waandishi hao wanapata sababu za kutukashifu. Mtaona humu wakati tunalia nchi inamalizwa hospital hazina dawa bado kuna watu wananguvu za kutetea dhulma hizi. Na wapo watu wengi tu bado wataipigia kura. Bongo zao zipoje hao? Ndio nikakumbuka hii mistari ya Okot

''My head, he says,
Is as big as that of an elephant
But it is only bones,
There is no brain in it''
 
you cannot fool all the people and all the time
 
Unajua na yote haya yaliyotokea kama ccm ikishinda tena 2015 basi sidhani kama upinzani utaweza kuchukua hii nchi.

Ila ni kweli itakuwa ajabu kama watz watawapigia kura tena ccm mwaka kesho.
 
Ukawa ni wajinga sana. Wakija kushtuka uchaguzi wa serikali za mitaa wameshindwa vibaya na sakata la escrow limeisha.

kwa hiyo wewe harlot unafurahia kuona wezi wakiiba fedha za wananchi? notorious twit!
 
​Naomba nianze kwa kuwashukuru wapinzani na wanaharakati wengine ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kutujuvya maovu na ufisadi mwingi ambao umekuwa ukijitokeza Mara kwa Mara, Kuanzia old IPTL ya kina Chenge mpaka Escrow, Kiwira, Epa, mabilioni ya Uswiss, radar, Richmond, n.k. Lakini inakatisha tamaa kuona watanzania hakuna lolote tunalolifanya zaidi ya kulalamika kwenye mitandao, when are going to Say enough is enough???? Wakati ndio huu aw kufanya maamuzi magumu

Hawa viongozi wanafanya wanavyotaka kwa sababu wana watz hakuna lolote tutakalofanya, we are sitting back and let them do what ever they want to do, hii Escrow ndo imeua kabisa.

Mimi ni mmojawapo wanaoamini kuwa mtu mkubwa anajua sana na amehusika kwa namna moja au nyingine kuruhusu Escow na hili halina ubishi. The question is what are going to do about it??

Mimi nasema hili, kuwawajibisha waliohusika sawa lakini hivi mnategemea kutakuwepo na jipya? Hakuna lolote na mmeishaona mifano. Dawa Yao ni kuiondoa hii sirikali madarakani it has proven failure mara zote. Let's take them out of the office, NDUGU ZETU POLISI MLIOZOEA KUPIGA NA KUUA WATU njooni tuungane na tuseme BASI, ninaamini kabisa kuwa hata nyie haya yanayofanyika hamyapendi.

TANZANIANS LETS SAY ENOUGH IS ENOUGH ..! TIME IS NOW, LETS NOT BE COWARDS..!


1. Kura zetu kwa UKAWA chaguzi za serikali za mitaa
2. Kuikataa katiba pandikizwa kwa kuipigia kura ya HAPANA
3. Kura zetu kwa UKAWA chaguzi za wabunge na raisi 2015

Everything is in our favor this time. Kuna kila ishara kwamba anguko la MiCCM limetimia!
 
Ninaomba kutoa ushauri wangu kwa watz wenzangu juu ya sakata/kashfa inayohusiana na Tegeta escrow. Kwa sehemu lilipofikia suala hili linahitaji si tu nguvu ya Bunge bali hata nguvu ya wananchi. Wananchi tuonyeshe HISIA zetu kwa kukerwa na jambo hili. Kwa wenzetu mliopo Dodoma kusanyikeni nje ya ukumbi wa bunge kwa muda wote wa bunge siku ya jumatano.

Sie tulio nje ya Dodoma tujitahidi kuwa makundi makundi kwa kadri ya maeneo husika tukifuatilia shughuli za bunge siku ya jumatano.

Lengo ni kuonyesha kuguswa na suala hili. Tulifanye hili kama ishala kwa watawala watambue wasipokuwa makini lolote laweza kutokea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom