Watanzania sio waaminifu, hatujui kiingereza

Chereko

Member
Jul 20, 2009
54
16
Sisemi mimi kama Chereko bali nachereka na maneno ya Waziri Kapuya kama nilivyosoma kwenye habari Leo jumamosi iliyopita -eti Watanzania sio waaminifu na hawajui kiingereza ndio maana kwenye mahoteli wafanyakazi wageni wamezidi. Je huyu ni Profesa na Waziri anayefaa kushughulikia mambo ya ajira nchini kwake? Kama kitengo chake cha kuhakiki kazi kwa wageni kimeshindwa kazi abainishe wazi!

1. Kujua kiingereza sio kujua kazi - kule ufaransa mahotelini wafanyakazi wengi tu hawajui kiingereza - sio huko tu, China, Ubelgiji, Urusi, Hispania, Italia, Brazil yale maneno "huyu anaongea kiingereza kigumu" ni jambo la kawaida. Wapo rafiki zangu walienda mji mmoja unaitwa Nice, siku ya kwanza hawakula chakula hotelini kwa kukosa mkalimani wa kiingereza. Kama huduma bora ni lugha, huduma bora hapo ulaya iko wapi?

2. Profesa si ametembea? Wengi wetu pia tumetembea, je si ni hoteli nyingi tu kubwa duniani hukuti mtu wa kukupokea mlangoni?. Hapa kwetu nenda movenpick, kempinski, New Africa, Southern Sun utapokelewa mlangoni vipi leo Waziri anasema "Watanzania wakiona mgeni wanababaika"!!! Si hoteli nyingi tu huku nje wakikuona ni mtu mweusi wanakudharau? Je hao wafanyakazi wa kigeni kazi yao ni kupokea wageni? Hiyo kazi si wanafanya watanzania kwa kuwa ni kazi isiyo na heshima?

3. Mahotelini kote kuna ziada ya wafanyakazi wa kigeni ambao kazi zao zingeweza kufanywa na watanzania, wanalipwa mishahara minono huku wakilipiwa nyumba, watoto wao wanasomeshwa kwa gharama za hoteli, Waziri haoni kuwa hii inapunguza mapato na hivyo kupunguza kodi ambayo ingelipwa serikalini? Idadi hii kubwa inasababisha gharama za uendeshaji wa hoteli kuwa kubwa hivyo bei kuwa kubwa jambo ambalo linasababisha wageni kuona hoteli zetu ni ghali hivyo kuathiri idadi ya watalii waingiao nchini.

4. Kwa kuwa wageni hao wanakuwa wakali kwa wafanyakazi raia wa Tanzania na wengi wao ni wabaguzi wa rangi, wafanyakazi wa ngazi za chini wanaolipwa kiduchu wanakuwa na hasira katika kazi ndio maana wanaweza kuonekana kutopenda kazi zao na kuathiri utendaji wao. Sambamba na pendekezo la Waziri kwa VETA kuweka mtaala fulani kwenye elimu ya mambo ya hoteli, ipo haja ya kutoa tahadhari kali kwa wafanyakazi wageni kabla ya kupewa kibali cha kazi nchini kuwa Tanzania sio nchi ya ubaguzi wa rangi.

5. Ni ukweli pia kwamba kuna wafanyakazi wengi wageni wapo nchini kwenye mahoteli hawana elimu inayokidhi au kufanana na ajira zao - kwa mfano nasikia pale Kempinski yupo mjerumani ambaye hana cheti chochote cha maana na analipwa pesa kibao pamoja na kuwa ni mbaguzi sana wa rangi. Watu kama hawa wapo wengi sana malipo ya mgeni mmoja tu yangeweza kuwa mshahara wa wafanyakazi wengi tu kwa watanzania au mishahara mizuri wangeweza kupatiwa watanzania kadhaa badala yake. Mheshimiwa Waziri usisahau ahadi ya Serikali ya kutengeneza ajira milioni moja!

Haya Mheshimiwa Waziri tumekutonya tuone basi kama wadhifa wako unautumia ipasavyo, kazi kwako. Tafadhali upate ripoti kwenye mahoteli yote makubwa, watu wangapi ni wageni, wana elimu gani, wanalipwa nini na wanafanya kazi gani. Ukipata nafasi utembee ukaongee nao usikie malalamiko yao badala ya kukaa ofisini ukingoja ripoti. Wewe ni Professa.

Chereko anapenda kuchereka hivyo tucherekeshe basi Mh. Waziri, au kwa lugha nyingine tupe raha Watanzania badala ya kututia huzuni. Samahani kama ukweli huu haukuupokea vema.

Watanzania ni marafiki, wanapenda wageni na wanaipenda lugha yao ya Kiswahili - tabasamu sio lazima kujua kiingereza, tabasamu halina lugha.
 
tusimlaumuu sana waziri labda kuna ka ukweli hapooo..tukafanyiee kazii..

uaminifu, uchapakazi, kujali muda, kujielezaa (lugha yeyote)..............
 
tusimlaumuu sana waziri labda kuna ka ukweli hapooo..tukafanyiee kazii..

uaminifu, uchapakazi, kujali muda, kujielezaa (lugha yeyote)..............

Wazungu wametuachia kakovu kabaya ka kujidharau sisi wenyewe, hakuna mantiki ya kusema tabia ambazo hata hao wanaojua kiingereza wanazo! Na kujua kiingereza ni sifa? Mbona wazungu wasiojua kiswahili hakuna mtu anayewadharau? Juzijuzi walibadili jina la uwanja wa ndege toka Julius Kambarage Nyerere kuwa Julius Nyerere eti kwa sababu wazungu hawawezi kutamka jina Kambarage! In short Tanzania ya sasa haina uongozi ulio kwa maslahi ya umma. Everybody for him/herself! Hizo ajira milioni moja wamewaajiri wapi? Labda ukichanganya na za machangudoa na wauza unga zitafika hiyo milioni moja!
 
Kwahili Waziri Kapuya kafulia! Hivi sasa Tanzania ni jalala la manamba kutoka nje! na hii inatokana na watu kama teye! Kuna waasia wamezagaa utadhani uko Punjab achilia mbali hawa jirani zetu waojidai na kiingereza chao ambacho hata sisi twakijua vema!
Mimi niliwahi kufanya kwenye taasisi ya fedha ambayo inamilikiwa na waasia ambapo uongozi ulikuwa tayari kuhonga uhamiaji kuleta 'wataalamu' wasiokuwa na sifa 'VIHIYO' na hao walikuwa wakilipwa mishahara miwili , mmoja kwa pesa za adafu, mwingine kwa USD achilia mbali marupurupu kama hyumba, umeme, mlinzi, house girl, fees za watoto international school na return ticket kwenda kwao kila mwaka! Mshhara huo wa madafu ulikuwa ni mara nne ya ninaolipwa mie.
Cha ajabu mimi nilikuwa ninaqualifications za juu kuliko yeye na hata kazi zake nilizibeba!
Lakini ilifika wakati nikaona nimtose ( Nikaresign) Kilichofuata yeye pia alibidi abwage manyanga within no period maana ngoma ilianza kuwa nzito!
Hivi hawa waasia wanaoletwa na kulazwa kwenye magodown yaliyoko Chang'ombe na Pugu road achilia mbali wanaozidi kujazan kwenye magorofa marefu yanayochipua kama uyoga mitaa ya Upanga na Uhindini vyombo vya dola vipo likizo?
Kwakweli Tanzania imekuwa ni moja ya nchi za ajabu ambapo ukiitwa 'foreigner' ujue umeula. Hebu angalia kwenye mahotel wageni walivyojazana! watanzania wao ni watu wa kudeki vyoo na kupangusa meza!
Hivi viongozi wetu hawajui kwamba itafika wakati walalhoi watesema 'enough is enough'?
 
Kumetumika kigezo gani cha mlinganisho hadi Mh. Prof. Waziri aseme kuwa watanzania siyo waaminifu na hawajui Kiingereza? Wamelinganishwa na raia wa nchi gani hasa? Mimi ninaamini watanzania ni waaminifu sana na wanajua kiingereza. Tunachokikosa watanzania ni kuwa hatuna self-confidence na hatupo aggressive (sijui kiswahili cha haya maneno). Wapo watanzania wenye sifa za kutosha tu kufanya kazi kwenye hayo mahoteli ila tatizo ni jinsi ya kujieleza na kuiweka CV katika mfumo ambao utamvutia mwajiri. Wenzetu hata kama ana uzoefu mdogo au sifa hazitoshelezi atajieleza kiasi kwamba mwenye kutoa ajira atavutiwa naye, kitu ambacho watanzania hatunacho. Sisi ni wapole na wanyenyekevu.
Ni wakati muafaka Mh. Prof. Waziri aangalie kwa undani sheria na sera za maswala ya ajira zinawalinda watanzania kwa kiasi gani na zinatekelezwa kwa kiasi gani na wageni wawekezaji wa mahoteli.
 
Professor mtumwa,Bado na cheo cha uprofessor anahusianisha ujuzi wa kiingereza na utendaji kazi wa mtu,HATARI sana hasa ukutilia maanani kuwa jina lake linashehereshawa na neno Profesa,Ni hatari kwa sababu yeye anatakiwa aongoze wengine wafuate mapito,kama profesa huo ni mtazamo wake kwa kweli itabidi tujiangalie upya uwezo wetu wa kupambanua mambo. Profesa anamaanisha wageni wote kwenye mahoteli yetu ni wajuzi wa kiingereza au ?. Wakati idadi kubwa ya watu ambao wangetakiwa kuwa chachu kwa watanzania kuenzi kiswahili na kukitukuza wanaenzi kiingereza ni HATARI kubwa,labda nashauri wasomi wetu waangalie watanzania wanahusiana na mataifa gani kati biashara zao na katika mambo muhimu ya maendeleo yao halafu wajue jinsi ambayo tunapoteza kalories nyingi kuzalimisha vijana wetu wajue lugha ambayo haina manufaa katika maisha yao ya kila siku. Ungejua gharama tuingiao na kiingereza chetu wakati tukifanya biashara na wajapan na wachina ambao kiingereza kwao sio deal mgelihurumia taifa na kuangalia umuhimu wa kutilia mkazo kiswahili ili watanzania wapate ajira ya ukarimani kwa hao wanaomind maliasili zetu wakituzuga kwa kiingereza chao.Tunalipa fedha nyingi kwa wakalimani wa kichina na kijapan,huku nchini mwetu mkazo ukiwa ni kiingereza ambacho labda kinawasaidia wanadiplomasia...
 
Kwani mnakumbuka Kapuya akifanya jambo gani la kuigwa tangu aitwe Waziri katika Wizara zote alizopitia?Nachelea sana hata kuitika U-professa wake!!Mtu huyu hakika ni mbabaishaji wa kiwango cha juu,hata kwa kauli zake ziwe za msikitini au bungeni anatisha na kusikitisha mno!!Sasa kama mnasema huyu ni Prof.mbona hata kautafiti kadogo saana haka ka uajiri wa wageni katika mahoteli yetu ameshindwa kukafanya?Acha leo anasema watanzania hawajui Kiingereza kumbe yeye Mtusi basi!!
 
Kwa Kiingereza hili Kapuya kafulia. Kwa uaminifu hapa kuna gap. Watoto wanataka kupaa kabla hata ya kufanya kazi. House keeping, wanapekua sana mizigo ya Wageni vyumbani na wengine ukisahau kitu usirudi bure wala huipati. Lakini hata hivyo tuna wengi tu ambao ni waaminifu. Tatizo kubwa hapa ni customer service level iko chini sana kwa watu wetu.
 
Watanzania acheni kujidharau hivyo. Hivi kule East Asian countries aliyekuambia kuwa wanafahamu wote kiingereza fasaha ni nani??? Tena wanafurahi kuongea lugha yao halafu wewe unalazimika kumtafuta mkalimali, tena hapo ni job creation though temporary kwa wenyeji wa nchi husika. Usijione superior kwa utamaduni wa mwenzako. Kwanza tumlaumu yeye si alishakuwa waziri wa Elimu huko nyuma, je alifanya nini katika mtaala wa kiingereza kuhakikisha kinakuwa ni medium of instructions kwa shule zetu za msingi??? Mifumo mibovu ambayo viongozi kama kapuya walishiriki kuiweka ndiyo imetufikisha hapa tulipo. Tungeamka mapema watoto wetu wangekuwa na ufahamu wa lugha ya kiingereza na kiswahili. Mbona Kenya are fluent in English na kishwahili wanacho pia???viongozi wetu hakuwa kiona mbali (wangeomba darubini iwasaidie kuona mbali). Au kwa kuwa their kids and grandchildren waliwapeleka majuu au kusoma Arusha Schoool, IST, ISM, etc. Kama kiongozi hana cha kutaamka cha maana kwa jamii ni vema anyamaze kimya tena kimyaaaa.
 
Kwani mnakumbuka Kapuya akifanya jambo gani la kuigwa tangu aitwe Waziri katika Wizara zote alizopitia?Nachelea sana hata kuitika U-professa wake!!Mtu huyu hakika ni mbabaishaji wa kiwango cha juu,hata kwa kauli zake ziwe za msikitini au bungeni anatisha na kusikitisha mno!!Sasa kama mnasema huyu ni Prof.mbona hata kautafiti kadogo saana haka ka uajiri wa wageni katika mahoteli yetu ameshindwa kukafanya?Acha leo anasema watanzania hawajui Kiingereza kumbe yeye Mtusi basi!!


Asante kaka/dada. Huwa ninajiuliza huyu prof, ni wa fani ipi?? Na alisoma chuo kipi?? Au ni vile vile not acredited???? Mambo yake mengi anayafanya kisanii na miujizaujiza tu!!!! Haya tena kina prof. Maji Marefu!!!!!!
 
Wazungu wametuachia kakovu kabaya ka kujidharau sisi wenyewe, hakuna mantiki ya kusema tabia ambazo hata hao wanaojua kiingereza wanazo! Na kujua kiingereza ni sifa? Mbona wazungu wasiojua kiswahili hakuna mtu anayewadharau? Juzijuzi walibadili jina la uwanja wa ndege toka Julius Kambarage Nyerere kuwa Julius Nyerere eti kwa sababu wazungu hawawezi kutamka jina Kambarage! In short Tanzania ya sasa haina uongozi ulio kwa maslahi ya umma. Everybody for him/herself! Hizo ajira milioni moja wamewaajiri wapi? Labda ukichanganya na za machangudoa na wauza unga zitafika hiyo milioni moja!

If this is true then it has to be the most depressing thing about TZ.jamani how can we have such a complex to ourselves?!change a name because westerners can't pronounce it?!so how long before we change Tanzania to a more western like name?how long before we have no identity after all?!
we should know that most ASIAN countries names are un-pronounceable by most Westerners but ASIANS wont change that for westerners to understand.At least they have their dignity intact.
so sad.
 
definition ya professor:


''a professor is a person who knows much about a very little thing''

kama ana uprofessor wa jicho bas hajui sikio nk nk nk nk..............

simlaumu huyu prof maana huwa anatema pumba toka zamani sana
 
Hawa ndio mawaziri wa JK jamani kwao usomi ni kiingereza, kazi kweli ipo
 
Kwa muda mrefu sasa, nimekuwa nikiwaza kuwa hivi Mheshimiwa JK ametoa wapi baadhi ya mawaziri wake?? Kila siku vituko haviishi!
 
Waziri wa nchi wa muda mrefu, mwenye koungoza Taifa kubwa kama la Tz, kuongea torojo kama hilo ni aibu tupu. Nasema hivyo kwa sababu zifuatazo:
1. Inaonekana katika mikutano na wawekezaji hakuna lolote analosema la kuisaidia nchi yake wala kuitetea ni Professor mtumwa! Alichosema ndicho walichomtuma, yaani amekichomoa midomoni mwao akaliletea taifa ikiwa fresh!
2. Hana takwimu zilizomwongoza kuongea pombe kali namna hiyo
3. Hajatembea akaona duniani sehemu tofauti tofauti kuwa kazi huchapika bila kukijua sana kiingereza na katika hizo nchi ni wajibu wa yule mwekezaji kuwapa training wafanyakazi wake siyo kuwabagua na kuwadharau ndani ya nchi yao.
4. Hana ufahamu kabisa wa tofauti za mishahara kati ya wafanyakazi wa kigeni na wazalendo, hilo ndilo linaleta wageni kuwadharau sana wazalendo, na kuwapaka matope!

UFISADI HUU UNAHITAJI JINA MAALUM.
 
Kama ni kweli Kapuya anaboronga toeni sababu tofauti zinazowafanya waajiri kutaoa ajira kwa wageni.

Kama mtu hawezi kuja na sababu tofauti, basi sababu za Kapuya ni za kweli.
 
Kama ni kweli Kapuya anaboronga toeni sababu tofauti zinazowafanya waajiri kutaoa ajira kwa wageni.

Kama mtu hawezi kuja na sababu tofauti, basi sababu za Kapuya ni za kweli.

Sababu ya kwanza ni kutokua na safety nets policies kwa raia watanzania, policies zina favour wawekezaji zaidi kuliko raia.

Sababu ya pili ni ya attitude ya watanzania kwamba wageni ni wajuzi kuliko watanzania na kigezo cha ujuzi kimekua lugha ya kingereza, kwakua watanzania wengi si fluent katika hiyo lugha hata wale wajuzi ambao hawako fluent mara nyingi wanakuwa eliminated kwenye interviews. Effect kubwa ni kwa wale waliosoma shule za waalimu wa UPE so msingi wa lugha ni mbovu japokuwa ni wazuri na niwaelewa katika area of interests.

Sababu ya tatu ni vitendo vya waliopewa dhamana kuendekeza ufisadi jambo linalofanya watanzania kutothamini uaminifu kwani waaminifu ni watu wasio fanikiwa katika mambo yao. Hii ni hatari kuliko zote kwani it pays to be fisadi kuliko kuwa mwaminifu na hivyo kusababisha transaction costs kuwa kubwa kuliko inavyo paswa kuwa.

Nne ni ubinafsi kwani watu wanaangalia faida yao sasa hivi na hawataki ku invest for the future of the country for it takes one to sacrifice a lot to build a sustainable system and nobody is ready to do that. Yaani ukiamua kubadili mifumo inamaana utabana kula ya watu wengi maana wengi wana interests kwenye hizo investments na ziko kwa makubaliano ambayo siyo public interests so to keep the status quo lazima kuwepo na visingizio vya hapa na pale kusukuma siku ziende hata kama its so obvious maelezo yanayotolewa hayakidhi haja.

Kwa uchache ni hivyo so na wewe leta sababu zako zakuonyesha hiyo statement in justification ya kuelezea hali iliyopo.
 
Watanzania huwa wananifurahisha. Sasa kama hizo hoteli wageni wake wengi wanaongea kiingereza kwanini kisiwe kigezo cha kuajiri? Huwezi kufananisha Tanzania na nchi kama China, Ufaransa nk na kusema kwasababu wahudumu wake hawajui kiingereza basi na sisi si lazima tuongee lugha hiyo. Hizo nchi ziko self sufficient.

Nimeshasema humu ndani kabla na nitasema tena. Watanzania tuna very low self esteem. Hatupendi kukosolewa. Tuamke jamani lasihivyo tutaishia kuwa defensive, kulaumu watu wengine na tutabaki na umaskini wetu kwa muda mrefu sana.
 
Sisemi mimi kama Chereko bali nachereka na maneno ya Waziri Kapuya kama nilivyosoma kwenye habari Leo jumamosi iliyopita -eti Watanzania sio waaminifu na hawajui kiingereza ndio maana kwenye mahoteli wafanyakazi wageni wamezidi. Je huyu ni Profesa na Waziri anayefaa kushughulikia mambo ya ajira nchini kwake? Kama kitengo chake cha kuhakiki kazi kwa wageni kimeshindwa kazi abainishe wazi!

1. Kujua kiingereza sio kujua kazi - kule ufaransa mahotelini wafanyakazi wengi tu hawajui kiingereza - sio huko tu, China, Ubelgiji, Urusi, Hispania, Italia, Brazil yale maneno "huyu anaongea kiingereza kigumu" ni jambo la kawaida. Wapo rafiki zangu walienda mji mmoja unaitwa Nice, siku ya kwanza hawakula chakula hotelini kwa kukosa mkalimani wa kiingereza. Kama huduma bora ni lugha, huduma bora hapo ulaya iko wapi?

2. Profesa si ametembea? Wengi wetu pia tumetembea, je si ni hoteli nyingi tu kubwa duniani hukuti mtu wa kukupokea mlangoni?. Hapa kwetu nenda movenpick, kempinski, New Africa, Southern Sun utapokelewa mlangoni vipi leo Waziri anasema "Watanzania wakiona mgeni wanababaika"!!! Si hoteli nyingi tu huku nje wakikuona ni mtu mweusi wanakudharau? Je hao wafanyakazi wa kigeni kazi yao ni kupokea wageni? Hiyo kazi si wanafanya watanzania kwa kuwa ni kazi isiyo na heshima?

3. Mahotelini kote kuna ziada ya wafanyakazi wa kigeni ambao kazi zao zingeweza kufanywa na watanzania, wanalipwa mishahara minono huku wakilipiwa nyumba, watoto wao wanasomeshwa kwa gharama za hoteli, Waziri haoni kuwa hii inapunguza mapato na hivyo kupunguza kodi ambayo ingelipwa serikalini? Idadi hii kubwa inasababisha gharama za uendeshaji wa hoteli kuwa kubwa hivyo bei kuwa kubwa jambo ambalo linasababisha wageni kuona hoteli zetu ni ghali hivyo kuathiri idadi ya watalii waingiao nchini.

4. Kwa kuwa wageni hao wanakuwa wakali kwa wafanyakazi raia wa Tanzania na wengi wao ni wabaguzi wa rangi, wafanyakazi wa ngazi za chini wanaolipwa kiduchu wanakuwa na hasira katika kazi ndio maana wanaweza kuonekana kutopenda kazi zao na kuathiri utendaji wao. Sambamba na pendekezo la Waziri kwa VETA kuweka mtaala fulani kwenye elimu ya mambo ya hoteli, ipo haja ya kutoa tahadhari kali kwa wafanyakazi wageni kabla ya kupewa kibali cha kazi nchini kuwa Tanzania sio nchi ya ubaguzi wa rangi.

5. Ni ukweli pia kwamba kuna wafanyakazi wengi wageni wapo nchini kwenye mahoteli hawana elimu inayokidhi au kufanana na ajira zao - kwa mfano nasikia pale Kempinski yupo mjerumani ambaye hana cheti chochote cha maana na analipwa pesa kibao pamoja na kuwa ni mbaguzi sana wa rangi. Watu kama hawa wapo wengi sana malipo ya mgeni mmoja tu yangeweza kuwa mshahara wa wafanyakazi wengi tu kwa watanzania au mishahara mizuri wangeweza kupatiwa watanzania kadhaa badala yake. Mheshimiwa Waziri usisahau ahadi ya Serikali ya kutengeneza ajira milioni moja!

Haya Mheshimiwa Waziri tumekutonya tuone basi kama wadhifa wako unautumia ipasavyo, kazi kwako. Tafadhali upate ripoti kwenye mahoteli yote makubwa, watu wangapi ni wageni, wana elimu gani, wanalipwa nini na wanafanya kazi gani. Ukipata nafasi utembee ukaongee nao usikie malalamiko yao badala ya kukaa ofisini ukingoja ripoti. Wewe ni Professa.

Chereko anapenda kuchereka hivyo tucherekeshe basi Mh. Waziri, au kwa lugha nyingine tupe raha Watanzania badala ya kututia huzuni. Samahani kama ukweli huu haukuupokea vema.

Watanzania ni marafiki, wanapenda wageni na wanaipenda lugha yao ya Kiswahili - tabasamu sio lazima kujua kiingereza, tabasamu halina lugha.

Kwa sababu tunaongelea controversial comments za Waziri, naomba nione maneno yake yeye mwenyewe, halafu ndio tuendelee na mjadala. Anaejua Waziri katamka nini na akiweke hapa, nukuu ya neno kwa neno!

Hizo hapo juu ni tafsiri zako wewe, Chereko!
 
Back
Top Bottom