Watanzania ni wasahaulifu sana

Watanzania ni wasahaulifu sana

Busu la Kenge

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2025
Posts
2,331
Reaction score
4,241
Leo hii Polepole ni shujaa. Leo hii Magufuli naye anakumbukwa.

Yani tunasahau haraka sana. Tunasahau uchaguzi wa 2020 ulivyokuwa uchafuzi.

Tunasahau Lissu kunyanyaswa kila mara kukamatwa kutiwa ndani na hatimae kumiminiwa risasi kama punda.

Tumesahau hela za rambirambi kupigwa mchana kweupe.

Tumesahau Godbless Lema kufungwa na kukaa gerezani bila sababu.

Tumesahau Braza Ben sa8 na Azory.

Leo hii Polepole naye eti Shujaa.

Haya ya Polepole yangesemwa na mtu kama Lema, Mnyika sugu N.k yangekuwa na tija.

Kwa tabia zetu hizi za kusahau CCM itatawala Kwa muda mrefu Sana.
 
Acha tu hii nchi ngumu sana imagine kipindi ambacho biashara zilianguka na kufungwa watu walinyimwa ajira hadharani watumishi walinyimwa ongezeko la mishahara eti kinakumbukwa😥😥😥😥kipindi ambacho kina bashiru walikuwa hata huwezi kuwasogelea Wala kuongea nao
 
Uzi wako umedoda ila ngoja nichangie kidogo.

Jamaa ukiacha bange na kujichetua unakuwa na madini , Leo umeandika point za maana sana.
 
Back
Top Bottom