1. Watu wamekuwa wakifanya kazi na kujibidishaa tangu uhuru. Bahati mbaya sana maendeleo hayaji kwa kufanya kazi kama punda kitu ambacho jiwe alifanikiwa sana kuwaaminisha wafuasi wake katik kipindi chake.
Maendeleo yangekuwa yanakuja kwa kufanya kazi kama punda katika hii miaka ungewaona wasukuma mikokoteni, makuli, wamachinga, mama ntilie, bodaboda, watembeza ukwaju/maji, wakulima wengi, n.k wakiwa wameondokana na umaskini.
2. Wawekezaji wa ndani unaowazungumzia ni wapi? Bakhresa, MO, Sayona, Manji, Rostam? Kama ni hao, wengi wao wanataka kuuza juice, ice cream, tambi, bodaboda, mchele, mafuta.
Tunzania inahitaji wawekezaji wakubwa kabisa aina ya Dangote katika kila sekta ili ijitoe mikononi mwa makucha ya umaskini.Wawekezaji wa haina hii ndio watakaotoa ajira na kodi za maana na kuleta tija kwa rasilimali tulizo nazo.
Huu wimbo wa kuendelea kukalia rasilimali unaoimbwa tangu enzi za Nyerere kusubiri watoto wetu waje kupata ujuzi wa kuzivuna umepitwa na wakati. 60 damn years!