BIG X
JF-Expert Member
- Nov 4, 2011
- 777
- 212
Najaribu kutofautisha upole na udhaifu. Hivi sisi waTZ ni wapole au wadhaifu!, Mambo mengi yanayofanywa na serikali yetu dhaifu ingekuwa ni nchi nyingine kama kenya tu hapo mfano tungekuwa tunaongea mengine saahizi, sababu wananchi wasingekubali kuonewa kiasi hiki. Sababu tunaimba Amani kila siku, lakini ni amani gani hii ambayo tunayo wakati roho zetu zinateseka kila siku!!. Wakati mwingine tunamkosea Mungu kumuomba atusaidie wakati sisi wenyewe hatujisaidii, huu ni ujinga!. Napata wasiwasi kusema waTZ ni wapole, mi nadhani sisi waTZ ni wadhaifu na ndio mana tunakubali kuongozwa na serikali na viongozi dhaifu!!.