Watanzania hawa ni kaka,dada zetu wadogo zetu na inawezekana watoto wetu, maisha ya Anasa ni mabaya saana, ni bora nikae siku mia moja masikini kuliko siku moja katika starehe ambayo mwisho ni mateso kwako, familia na taifa. Tujifunze kutafuta hela pasipo dhalilisha utu wetu,
Mtu asiuudharau Ujana wako kwa maslahi yake. Tumpende Mungu na kushika maagizo yake tutashinda.
kWANI Asiyefundishwa na mamaye ,ulimwengu utamfunza, sasa vijana wenzangu tusisubiri kufunzwa na Ulimwengu maana ulimwengu ukikufunza hautajali umri,wadhifa na namna yeyote ile mwisho UTAJUTA tu.
Tusiwape wazazi wetu masononeko ya moyo na machozi yasiyofutika maishani kwa starehe ambayo inapita tu