Watalamu wa madini naomba msaada wenu

Barantogwa

Senior Member
Joined
May 3, 2014
Posts
135
Reaction score
179
Jamani habari za Jumapili.

Kuna rafiki yangu yupo Morogoro, siku kazaa zilizopita alinitumia picha hiyo hapo chini👇,

Akiniomba nimsaidie kuulizia kuwa hayo ni madini Gani na thamani yake ikoje sokoni?

Mimi Sina ujuzi juu ya madini na Vito, kwa mwenye uelewa naomba msaada wenu.

 
Billionaire mpya huyo in Tanzania, yani hata hela za kina Dully Sykes haifui dafu kwa hayo madini
 
Mkuu, mshatoboa aisee
Hayo madini yana pesa sana ni ya tatu kutoka thamani ya gold, aisee mpaka nawaonea wivu mshakuwa mabilionea hapo 🔥
 
Mh huu mwandiko upo kimkakati sana.
 
Uzi umekaa kutapeli ila ngoja nikusaidie

Professional huwezi kufanya gem identification kwa picha ila kwa uzoefu yanaonekana kama ni quartz aina ya amethyst kwa sababu ya rangi yake ya purple hata shape yake mara nyingi quartz huwa na hiyo shape ya kuchongoka na kuhusu thamani yake bei yake ni kawaida sana sokoni.

Hii consultation wenzio wanalipia.
 
Nitapeli kwa faida gani mkuu? Hizo ni picha nimetumiwa na mwenye Mali, yeye yupo Morogoro, Mimi nipo Mwanza. Picha nyingine ni hiyo hapo
 

Attachments

  • IMG-20250829-WA0006.jpg
    18.5 KB · Views: 39
Nimeangalia hayana thamani sana ,maana Gram Moja ni sawa na sh 2500,sasa ili uwe na pesa mingi basi ujaze gunia,yanaitwa Amethyst kwa kingereza na kwa kiswahili ni methisto(madini ya zambarau)
 
Yanaitwa Amethyst. ikiwa na rich purple color, haina cracks, iwe clear- isiwe na inclusions, size kubwa gram 10 kuendelea. Nanunua kwa 500,000 kwa gram.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…