Watalamu naomba msaada kuku wanapukutika

Watalamu naomba msaada kuku wanapukutika

Tuliponga

Senior Member
Joined
Feb 11, 2014
Posts
190
Reaction score
49
Ninafuga kuku wa kienye ambao wamefika 80 na huwa ninawaachia wajitafutie chakula wenyewe,kwa sasa hivi kuku wangu wameanza kufa ghafula bila ya kujua ni kitu gani kinachosababisha vifo hivyo.Nimewapa chanjo ya kideri mara 3 kila baada ya miezi 3.Cha kushangaza ni kwamba kuku wanaingia bandani wakiwa wazima ninapowafungulia asubuhi ninakuta kuku kama 3 wamekufa,nikiwafungulia wakiwa kujitafutia chakula mitaani wengine wanaanguka ghafula hukohuko nakufa.Hawaharishi kinyesi chao ni kigumu isipokuwa nilipofanya uchunguzi kuna kuku mmoja ametoa kinyesi chenye rangi ya kijani japo kuwa ni kigumu kama cha kuku wengine.Kwa maelezo haya ninaomba munisaidie namna ya kufanya au tiba ya kuwapa ili niweze kuokoa kuku wangu.
 
Hello..kuna dawa flani inatwa Agricox au ESB3 pls zijarubu hizi..kama ni magonjwa ya tumbo inaflash haraka..yaani within 24 hrs utaona mabadiliko
 
Kama wanakufa umri wa kuanza kutaga basi ni ugonjwa wa MAREKSI. Naomba kujua wana umri gani.
 
Kama wanakufa umri wa kuanza kutaga basi ni ugonjwa wa MAREKSI. Naomba kujua wana umri gani.

Kuku mmoja alikuwa ameanza kutaga na wengine walikuwa wamekaribia kuanza kutetea kwa sasa vinavyokufa sana ni vifaranga vina umri wa mwezi mmoja na nusu na vingine mwezi mmoja.Vifaranga vingi vinauvimbe kichwani hasa kwenye macho kiasi ambacho uvimbe unakuwa mkubwa kiasi cha kuziba macho kabisa ,uvimbe unaanza jicho moja na baadae unahamia upande mwingine.Baadae macho yote yanaziba na kutoa vitu vizito kama usaa ulioganda.
 
hiyo ni ndui. uliwapa chanjo ya ndui.. kuku wenye nfui huwa wanashambuliwa na magonjwa mengimengi tu. kwa kuwa hawana kinga mwilini. wape antibacteria halafu chanjo. ila ni vzr upeleke kuku mgonjwa wakamuangalie kwa kumchinja uweze kujua ni magonjwa gani haswa.
 
Hivi jameni, kama umeweza kufikisha kuku80 na bado unafuga hulia, badilika na uone kama ufugaji ni kazi na watengenezee hao kuku bando kuepusha kupata magonjwa huko wanakotembelea
Preventiin is cheaper than treatment
 
Hivi jameni, kama umeweza kufikisha kuku80 na bado unafuga hulia, badilika na uone kama ufugaji ni kazi na watengenezee hao kuku bando kuepusha kupata magonjwa huko wanakotembelea
Preventiin is cheaper than treatment

Kwa hasara niliyoipata nikifanikiwa kuwatibu waliobakia nitawafungia ndani.
 
hiyo ni ndui. uliwapa chanjo ya ndui.. kuku wenye nfui huwa wanashambuliwa na magonjwa mengimengi tu. kwa kuwa hawana kinga mwilini. wape antibacteria halafu chanjo. ila ni vzr upeleke kuku mgonjwa wakamuangalie kwa kumchinja uweze kujua ni magonjwa gani haswa.

Sikuwapa chanjo ya ndui zaidi ya chanjo ya kideri.
 
Usisubili wapone anza sasa usisubili kesho
 
wiki 2 zilizopta vifaranga wang kumi wamekufa ghafla ikw ni siku 2 baada ya kuwapa kinga ya kideli, nimemuuliza bwana mifugo ameniambia itakuw nilizdsha dawa hvyo nawew lichungze hlo
 
Kutoka kitu kama sabuni ya mche iliyo lowekwa machoni ni upungufu wa vitamini (A) hauna tiba unakingwa kwa kuwapa majani mabichi. kuku kufa gafura huenda ni shinikizo la damu, wafungie majani kwa kuning'iniza wafanye mazoezi kupunguza mafuta.
 
Kutoka kitu kama sabuni ya mche iliyo lowekwa machoni ni upungufu wa vitamini (A) hauna tiba unakingwa kwa kuwapa majani mabichi. kuku kufa gafura huenda ni shinikizo la damu, wafungie majani kwa kuning'iniza wafanye mazoezi kupunguza mafuta.[/QUOTE

Kumbe Kuku wanapata shinikizo la damu. Nimejifunza kitu hapa.
 
Juzi kuku wangu waliumwa ghafla,nilichokifanya nilitwanga kitunguu thomu nikawapatia,baadae nikawatwangia mwarubaini pamoja na alovera pamoja nikaweka kwenye pumba,nikawanyima maji for two hours,nimekuja kuwafungulia baadae wote ni wazima kabisa,
dawa za asili nazo ni tiba pia.
 
hao kuku wako moja kwa moja wanaumwa ndui ulitakiwa kuwachanja ndui kwa kuwachoma cndani ktk mabawa
 
Kutoka kitu kama sabuni ya mche iliyo lowekwa machoni ni upungufu wa vitamini (A) hauna tiba unakingwa kwa kuwapa majani mabichi. kuku kufa gafura huenda ni shinikizo la damu, wafungie majani kwa kuning'iniza wafanye mazoezi kupunguza mafuta.

Aisee kumbe na kuku wanaweza kupata shinikizo! Bas ndo maana Mama yangu kuku Wake wanaumwa anawafungia!
 
Wakuu Mara zingine kuku hufa gafla ,kama nyumba ni chafu&maji hayatoshi% kuku wanahitaji maji&mazingira masafi ,chakula chenye virutubisho........
 
mkuu Jawilat embu nifafanulie hiyo tiba mbadala. Kitunguu saumu ukikitwanga unaweka kwenye.maji au pumba? Unaweka kwa ratio ipi? Muarobaini na alovera ukiiloweka na kuitwanga unawekaje kwenye pumba?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom