Wataalamu wa Kuziba Paa linalovuja

Wataalamu wa Kuziba Paa linalovuja

Mkombozi

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2008
Posts
844
Reaction score
477
Wakuu,nyumba yangu inavuja sehemu nyingi sana.Mabati yake ni ya migongo kutoka ALAF ya Africa kusini.Niliezeka 2011,mwanzo hayakuniletea shida Ila baadae yakaanza kuvuja.Sasa natafuta wataalamu wa kuziba.Mwanzo walinizibia mafundi wa mtaani kwa Kutumia Maroo(lami) kwenye kila msumari Ila tatizo limekuwa likijirudiarudia sana
 
Aisee hiyo hali hata mimi kwangu ipo ila tatizo ni mafundi wakupauwa.nashidwa hata kuweka jipsam bod maana itaaribika tu namaji,nimeuliza kwa mafundi wendi wanasema hakuna suruhu zaidi yakuziba na hiyo lami
 
Namshauri mtoa mada,awarudishe hao mafundi walioezeka waje kuziba hayo mashimo ya misumari.
Kiufupi hao hawakuwa mafundi ila ni njaa tu,au yeye mwenye nyumba alipenda mafundi cheaper!!
 
Mara nyingi bati za Migongo mipana hasa misumari yake huwa na kofia iliyoambata na Mpira kuzuia maji kupitia juu ya hiyo misumari.Hasa kwa kuwa imekaa kwa muda mrefu mipira hiyo hukakamaa na kupukutika, kwakuwa imeshapigwa na jua na mvua kwa muda mrefu na hivyo kusababisha maji kupita juu ya msumari na kuingia ndani.
 
Mara nyingi bati za Migongo mipana hasa misumari yake huwa na kofia iliyoambata na Mpira kuzuia maji kupitia juu ya hiyo misumari.Hasa kwa kuwa imekaa kwa muda mrefu mipira hiyo hukakamaa na kupukutika, kwakuwa imeshapigwa na jua na mvua kwa muda mrefu na hivyo kusababisha maji kupita juu ya msumari na kuingia ndani.
ndugu umeongea point kubwa sana..so ushauri ni bora tupige misumari ya kawaida au vip??? coz hata mimi nimepiga hiyo misumari yenye rubber..
 
Tumia soda flex , au sika flex. Mtafute Magambo pale nabaki Afrika mwenge atakusaidia .
 
Kama uko dar nina fundi kaziba kwa kutumia silconi sijajuta. Lami jua Kali inayeyuka utaikuta kwenye mashuka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom