Wataalamu njooni na jibu kwa nini jamii nyingi zinazoishi mwambao wa Bahari na Maziwa mwamko wa Elimu uko chini

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,480
37,756
Habari inayobamba kwa sasa kuhusu Elimu yetu baada ya kutangazwa kwa matokeo ya darasa la 4, darasa la 7 na kidato cha 4 ni kuhusu mkoa wa Mtwara kuingiza shule 9 kati ya 10 kwenye orodha ya shule zilizofanya vibaya. Tayari Mkuu wa mkoa Mtwara na NECTA wametoa tamko kukanusha kwamba hayo siyo matokeo ya mwaka Jana bali ni ya miaka mitatu iliyopita. Yote kwa yote bado inabaki kuwa ni matokeo ya mkoa wa Mtwara ulioko mwambao wa Bahari ya Hindi.

Ukiondoa mikoa ya Mwanza, Geita, Kagera na Mara inayopakana na mwambao wa Ziwa Victoria na Mbeya (Kyela) wanaopakana na ziwa Nyasa waliobaki hususani wanaopakana na Bahari ya Hindi yaani mikoa ya Tanga, Pwani, Dar es salaam, Lindi na Mtwara, ile inayopakana na Ziwa Tanganyika yaani Kigoma na Rukwa mwamko wao wa kielimu uko chini sana na matokeo yao ya mitihani kila mwaka yako chini (Tazama matokeo ya Kigoma mwaka Jana) na wenyeji wanaona kama haliwahusu.

Sasa wito wangu ni kwa wataalamu na humu JF naamini mmo wataalamu wa kada mbali mbali ikiwemo utafiti wa kielimu, naomba tuje na andiko la kwa nini maeneo niliyoyataja bado wanaona Elimu si kipaumbele? Zamani kidogo jamii za wafugaji nazo zilikuwa katika mwelekeo huu, lakini Leo Wamasai na Wasukuma ni miongoni mwa makabila yenye mwamko wa kielimu na watoto wao wanafanya vizuri.
Karibuni Kwa maoni na maboresho.
 
Wao wamechagua kupiga mbizi na kuwa wavuvi sio lazima wasome, wakati uchumi wa Kati waneufikia kwa kuvua samaki.
 
Mtwara wao wanataka kua Waimbaji tu hawataki Elimu any way hili tatizo linaanzia kwa wazee wao pengine wao hawakusoma au wanaona elimu haina maana ni kupoteza time tu au hata walimu wanachangia ktk kuangamiza elimu na wanafunzi inafaa radio zipite mitaani kuwauliza wazee kwa nini watoto wao hawataki kusoma.

unajua Taifa hili hivi limekumbwa na ujinga na upunbavu kila mtu anataka kuimba na kuwa star hii ndio shida wameona elimu haina maana tena katika maisha yao na ukiangilia kijujuu tu utaona ni kweli. leo waimbaji hawakusoma lkn wanaonekean ndio bwana wakubwa maana hata wana siasa na maraisi wa nchi hizi wanachezesha muziki na kukata viuno na mtu ambae hakusoma ,sasa hii kitu ndio inawanya kila kijana ana dream ya kuwa kama fulani leo wana muziki imekuwa ndio roll modell yetu ,wkt ndio wajinga wa mwishoo.
 
Mtwara wao wanataka kua Waimbaji tu hawataki Elimu any way hili tatizo linaanzia kwa wazee wao pengine wao hawakusoma au wanaona elimu haina maana ni kupoteza time tu au hata walimu wanachangia ktk kuangamiza elimu na wanafunzi inafaa radio zipite mitaani kuwauliza wazee kwa nini watoto wao hawataki kusoma ,unajua Taifa hili hivi limekumbwa na ujinga na upunbavu kila mtu anataka kuimba na kuwa star hii ndio shida wameona elimu haina maana tena katika maisha yao na ukiangilia kijujuu tu utaona ni kweli ,leo waimbaji hawakusoma lkn wanaonekean ndio bwana wakubwa maana hata wana siasa na maraisi wa nchi hizi wanachezesha muziki na kukata viuno na mtu ambae hakusoma ,sasa hii kitu ndio inawanya kila kijana ana dream ya kuwa kama fulani leo wana muziki imekuwa ndio roll modell yetu ,wkt ndio wajinga wa mwishoo.
Nimekuelewa sana unachotaka tukifahamu. Kwa maana hiyo unamaanisha mwamko mdogo wa Elimu Mtwara na kwingineko Mwambao umechangiwa na Mafanikio ya akina Ali Kiba, Diamond na Harmonize?
Naona kama tunataka kuwatwisha mzigo usio wao maana tatizo hili limeanza zamani na hata hao uliowasema wamepata mafanikio kwa kukata viuoni baadhi yao ni Wahanga.
 
PESA PESA,huko kupata pesa za kuchezea n rahis,hvyo watoto hupata tamaa ya kushika misimbaz wakiwa wangali shule
 
Kiasili watu wa ukanda wa pwani wa bahari ni wavivu sana na ili usome au usomeshe unatakiwa usiwe mvivu

Na ni wavivu kwa sababu ukanda wa pwani maisha ni maraisi sana sana yani hakuna njaa kuna matunda mengi ,kuna mvua nyingi na hata upatikani wa pesa ndogo ndogo za kula pia ni mkubwa

Nakama watu wa pwani wangesoma basi wangeitawala Tanzania katika nyanja zote
 
Namaanisha Elimu Dunia Mkuu, samahani kama nimekuudhi.
Ujiniudhi, na sikumbuki mara ya mwisho kuudhika..
nilichotaka hapa ni wewe kuwa specifically juu ya kile unachotaka kijadiliwe hapa..

we umesema hawana mwamko wa elimu, bila kutaja elimu ipi kusudiwa unayoiongelea hapa.

kuna elimu nyingi, wanaweza wasiwe na hiyo uliyoiksudia wewe hapa, ila ilo haina maana kwamba hawana elimu nyingine.




Nb: kuhusu muamko wa elimu dunia kwa huo ukanda ni tatizo la kihistoria zaidi.. hata Mkapa aliwaisema ili.
 
Nimekuelewa sana unachotaka tukifahamu. Kwa maana hiyo unamaanisha mwamko mdogo wa Elimu Mtwara na kwingineko Mwambao umechangiwa na Mafanikio ya akina Ali Kiba, Diamond na Harmonize?
Naona kama tunataka kuwatwisha mzigo usio wao maana tatizo hili limeanza zamani na hata hao uliowasema wamepata mafanikio kwa kukata viuoni baadhi yao ni Wahanga.
Kama umenielewa sasa tusubiri Wamtwara wapelekewe viongozi ambao c katika wao waje wawatawale tumeona wana muziki wengi wametajikana duniani lkn mwisho wao wamerejea uswahilini na hawakufanya chochote.Elimu ni muhimu sana lazima wazee wajitahidi kuwasomosha watoto wao.
 
Ujiniudhi, na sikumbuki mara ya mwisho kuudhika..
nilichotaka hapa ni wewe kuwa specifically juu ya kile unachotaka kijadiliwe hapa..

we umesema hawana mwamko wa elimu, bila kutaja elimu ipi kusudiwa unayoiongelea hapa.

kuna elimu nyingi, wanaweza wasiwe na hiyo uliyoiksudia wewe hapa, ila ilo haina maana kwamba hawana elimu nyingine.




Nb: kuhusu muamko wa elimu dunia kwa huo ukanda ni tatizo la kihistoria zaidi.. hata Mkapa aliwaisema ili.
Kama ni tatizo la kihistoria sawa, lakini nimetolea mfano wa jamii za Wafugaji ambao nao walikuwa na tatizo hili lakini angalau wao kwa sasa wamejikwamua. Je, hatuna cha kufanya ili kuwaondolea mtazamo huu ambao unazidi kuwatenga na Dunia ya teknolojia.
 
Kiasili watu wa ukanda wa pwani wa bahari ni wavivu sana na ili usome au usomeshe unatakiwa usiwe mvivu

Na ni wavivu kwa sababu ukanda wa pwani maisha ni maraisi sana sana yani hakuna njaa kuna matunda mengi ,kuna mvua nyingi na hata upatikani wa pesa ndogo ndogo za kula pia ni mkubwa

Nakama watu wa pwani wangesoma basi wangeitawala Tanzania katika nyanja zote
Nakukubali mkuu ndio maana wazaramo wa dsm anakuja mtu kutoka mikioni ndio mkuu wa mkoa wao ,wao kazi yao mdundiko tu hawataki kusoma .
 
Kama ni tatizo la kihistoria sawa, lakini nimetolea mfano wa jamii za Wafugaji ambao nao walikuwa na tatizo hili lakini angalau wao kwa sasa wamejikwamua. Je, hatuna cha kufanya ili kuwaondolea mtazamo huu ambao unazidi kuwatenga na Dunia ya teknolojia.
taratibu lakini kwa uhakika, hata uko somo wameanza kulielewa..
muitikio upo mkubwa.
na inabidi watu wa ukanda huo WAHUBIRIWE UKWELI zaidi ya kitu kingine kama ambavyo Mwinyi aliamua kuwachana wazi wazi.

na inshu nyingine japo inaweza isiwe interesting kwako ni kwamba, bahati ya wao kufanikiwa nje ya ELIMU DUNIA ni moja ya sababu inayopunguza kasi ya mabadiliko yaliyopo.

wanafanikiwa katika Biashara, sanaa etc, hali hiyo inawafanya waone si lazima sana kutafuta thamani ya X Darasani.

na jambo jingine, watu kama akina MS wanaoubiri uwepo wa mfumo Kristo wathibitiwe..

kuhubiriwa sana mfumo Kristo kuna mpunguzia mzazi VIBE ya kumsomesha mwanae..
ni mzazi gani yupo tayari amalize pesa yake kulipa ada alafu katika nafasi ya kazi ama masomo ya juu mwanae apigwe kapuni kisa dini yake?.

mfumo Kristo upo kwenye porojo tu, nje na hapo haupo.
 
Back
Top Bottom