Wastaafu EAC "Waiumbua",Waikana CHADEMA

Wastaafu EAC "Waiumbua",Waikana CHADEMA

Tume ya Katiba

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
4,896
Reaction score
1,866
BAADHI ya wazee wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wamesema hawalitambui kundi la watu waliojiunga na Chadema wakidai kwamba ni viongozi wa jumuiya hiyo na kukanusha taarifa kwamba wastaafu wengine wako mbioni kujiunga na chama hicho cha siasa.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wastaafu 13 waliokuwa wamewakilisha wenzao walisema kuwa uongozi wanaoutambua ni ule wa watu saba uliopo Mahakamani na wengine wanaojiita viongozi wa jumuiya hiyo wamelenga kuwarubuni wazee hao.
Akisoma tamko lao kwa niaba ya wenzake, Gregory Sandaria alisema kuwa wameguswa na taarifa iliyotolewa na wastaafu wenzao katika gazeti moja la kila siku (Si HabariLeo), kwamba viongozi hao wameamua kujiunga na Chadema na wastaafu wengine wako mbioni

"Kauli hiyo ya wastaafu hao sita viongozi wa kikundi cha EACORA wakiongozwa na Benjamin Mutembei na Jonas Musokwa picha yao ilipewa hadhi kubwa kwa kuwekwa katika ukurasa wa mbele wa gazeti hilo tena kwa kutumia umaarufu wa wastaafu wa EAC na sio vyama vyao vya siasa walivyo hama, ina utata," alisema.

Alisema "Hatuna tatizo la wao binafsi kujiunga na Chadema au chama chochote kingine cha siasa kwani uamuzi huo ni wa mtu binafsi."

Alisema kinachowasumbua ni staili waliyotumia ya kujiunga na chama hicho kwa kutumia umaarufu wa jina la wazee wastaafu wa EAC ambayo imeleta hisia potofu kwa jamii na hasa wadadisi wa mambo ya kisiasa hapa nchini.

Tunapenda kutamka kwamba hakuna kikao cha wastaafu tulichokaa kwa ujumla wetu na kujadili mapendekezo hayo na kisha uamuzi ukatolewa kwamba wastaafu wa EAC wajiunge na Chadema kama inavyodaiwa na wenzetu hao," alisema.

Tunaomba ieleweke kwamba, Umoja wa Wastaafu wa EAC haukusajiliwa kama chama rasmi, bali umoja ulisajiliwa na wastaafu 17,746 na kuwaunganisha waliokuwa wafanyakazi wa EAC, GFS pamoja na mashirika yake ya EARC, EAHC, EACHS, EAP&T na EAAC baada ya kuvunjwa kwa EAC mwaka 1977," alisema

Sandaria alisema walilazimika kujiunga ili kujenga nguvu za pamoja kwa nia ya kuikabili Serikali ambayo kwa sababu inazozijua yenyewe bado haijawalipa kikamilifu mirathi au haki zao za msingi zilizotokana na ajira zao

Taarifa hiyo imetolewa na kusainiwa na wawakilishi wa wazee hao ambao ni Sandaria, Yusuf Hamsini, Alfred Carere, Mbayo S.M.J, Asumbile Mwambona, Abdallah Masondole, Athuman Mwilima, KessY Gerald na Michael Peter.

Source: Habarileo tarehe 23 feb 2012.

Mytake: CHADEMA IACHE TABIA YA KUTAFUTA POLITICAL GAIN KWA KUPITIA MIGONGO YA WAZEE WETU, KUFANYA HIVYO KUTAWAKOSESHA WAZEE HAKI YAO.

ADC- Kwa maendeleo ya Taifa.
 
Hii iwe fundisho kwa CDM, si vyema kutumia shida za wazee wetu kujinufaisha kisiasa, swala la kisheria liachwe kisheria sio kuliingiza kisiasa.
 
Acha habari hewa CDM waliweka picha za wahusika na tukio, na wewe waambie hao (Umbea Leo) au wewe mwenyewe thibitisha walau kwa picha kama sio video!.
 
Wazee+wa+EAC.jpg

Hao waliokana wana tofauti gani na Yuda Iskarioti, au wale masalia PM7, au Nape Nnauye aliyeikana CCJ mchana kweupe. Wakanaji wote huwa ni wachumia tumbo tu, vipande thelathini vya fedha.
 
Hii iwe fundisho kwa
CDM, si vyema kutumia shida za wazee wetu kujinufaisha kisiasa, swala
la kisheria liachwe kisheria sio kuliingiza kisiasa.

MaCCM mnahangaika sana, wazee wamehama karibu mwezi na ushee hivi, leo ndio mnakuja kukanusha!? siku zote mlikuwa wapi? habari leo lina habari za mwezi nyuma aise!
 
Tume ya Katiba Kumbe iliwauma eh! mbona hamwalipi mafao yao ili hali bado mnawaitaji!
 
Huyo alietoa habari au taarifa hiyo ni mmojawapo wa viongozi wa wastaafu wa EAC? Kama sio mmojawapo wa viongozi, tutaamini vipi kama hajanunuliwa ili kukana?
 
poleni wastaafu mtaendelea kutaabika hadi mtakapo ionja mauti maana mmeamua kuchagua hilo fungu
 
Mkuu mimi kosa langu nini nimenakiri tu habari na kutoa ushauri wangu

Kosa lako ni hili hapa "Mytake: CHADEMA IACHE TABIA YA KUTAFUTA POLITICAL GAIN KWA KUPITIA MIGONGO YA WAZEE WETU, KUFANYA HIVYO KUTAWAKOSESHA WAZEE HAKI YAO".

Au uliandikiwa?
 
Kaka kuyafanya madai ye wazee wenu ni jambo la kisiasa kunafifisha na kudivert hoja zao za msingi, ni lazima sisi sote tukemee hii tabia.

umeambiwa wewe au hilo gazeti lako la aibu leo muweke hapo juu picha za hao waliokanusha kama cdm ilivyoweka wazi picha za wale waliojiunga,naona unakalia kubwabwaja tu
 
Kaka kuyafanya madai ye wazee wenu ni jambo la kisiasa kunafifisha na kudivert hoja zao za msingi, ni lazima sisi sote tukemee hii tabia.

Mkuu, kwani katika kujiunga kwao CDM hao wazee wa iliyokuwa EAC kulikuwa na sharti la CDM kuishinikiza serikali kuwalipa madeni yao?

Kama halikuwepo kutumia jina la wastaafu ilikuwa ni utambulisho tu wa lile kundi na si umaarufu wake. Lazima angetokea mtu akauliza, hao wazee wametokea wapi? Jibu rahisi na la kueleweka ni kutoka katika kundi la waliokuwa wastaafu wa EAC ambao wanaidai serikali mfao yao, stop.

Sasa kama hivi ndivyo, hiyo siasa katika madai ya hao wazee inaingilia angle gani?
 
Ndio maana ccm bado ipo madarakan kwa ajili ya wazee kama hawa.
 
Mkuu mimi kosa langu nini nimenakiri tu habari na kutoa ushauri wangu

Wala ula kosa mkuu wangu na mimi nimeariri tu kwa mleta uzi! unajua nini mkuu hii habari yako inanikumbuka uchaguzi wa Arumeru mashariki Nassari alipopewa heshima na wamasai maeno flani kule Meru Magamba walihahaha usiku na mchana wakiongozwa na Ole sendeka ili kujaribu kuwarubuni wale wazee wa kimasai ili wakubali kwenda kwenye media kukanusha kuwa hawajawahi kufanya hicho kitendo.Mission yao ili faili na mwisho wa siku walidondokea pua!:rockon:
 
UKWELI UKO WAPI ??.HABARI LEO SIKU HIZI KAMA UDAKU VILE .HALINA HADHI BORA HATA YA IJUMAA na SANI.
 
Kaka kuyafanya madai ye wazee wenu ni jambo la kisiasa kunafifisha na kudivert hoja zao za msingi, ni lazima sisi sote tukemee hii tabia.

Miaka zaidi ya 35 bado serikali yenu ya magamba inatafakari hoja za msingi za malipo ya wazee wa EAC?? Yani mmewanunulia ubwabwa hao wazee sita na kuwaandikia press statement wakaiwasilisha kwa mhariri wa umbealeo, oh no sorry habarileo.
Habari ndio hiyo wazee wameamua kuunganisha nguvu na Chadema kwakuwa wameridhika kabisa kwamba magamba ni matapeli na wauaji hawana mpango wa kuwalipa haki zao.
 
Back
Top Bottom