Wastaafu EAC "Waiumbua",Waikana CHADEMA

Wastaafu EAC "Waiumbua",Waikana CHADEMA

Wasubiri na vijana waliwafelisha form 4 ambao wengi ni umri zaidi ya miaka 18 watakapo tangaza wamejiunga kwenye ukombozi wa kweli(Chadema)waje wakanushe tena.
CCM badala ya kufanya kazi waliyoiomba 2010 wao wanakimbizana na Chadema.
 
Miaka zaidi ya 35 bado serikali yenu ya magamba inatafakari hoja za msingi za malipo ya wazee wa EAC?? Yani mmewanunulia ubwabwa hao wazee sita na kuwaandikia press statement wakaiwasilisha kwa mhariri wa umbealeo, oh no sorry habarileo.
Habari ndio hiyo wazee wameamua kuunganisha nguvu na Chadema kwakuwa wameridhika kabisa kwamba magamba ni matapeli na wauaji hawana mpango wa kuwalipa haki zao.

Mkuu umeisoma vyema hii taarifa? pia si njia bora kutumia neno "serikali yenu" kila mtu bila kujali chama anawajibika kutoa mchango wake kuhakikisha serikali inatimiza malengo ya kuwahudumia wananchi! sio kuwadanganya wazee kuwa wakihamia chadema ndio matatizo yao yatashughulikiwa.
 
Sasa shida iko wapi? Mi nadhani walipaswa kufurahi wakibaki wachache ili wale pilau jingi zaidi!
 
Miaka zaidi ya 35 bado serikali yenu ya magamba inatafakari hoja za msingi za malipo ya wazee wa EAC?? Yani mmewanunulia ubwabwa hao wazee sita na kuwaandikia press statement wakaiwasilisha kwa mhariri wa umbealeo, oh no sorry habarileo.
Habari ndio hiyo wazee wameamua kuunganisha nguvu na Chadema kwakuwa wameridhika kabisa kwamba magamba ni matapeli na wauaji hawana mpango wa kuwalipa haki zao.

Kwa hiyo ina maana na hao waliojiunga CDM walinunuliwa ubwabwa?:yo:
 
kama niliwasikia vizuri wazee wale walisema wenzao wako njiani na co wazee wote wa eac wako njiani, kwa hiyo kama wao hawako njiani basi ni wao ila kuna wenzao wanajiandaa kuingia cdm, hv hawa wazee watajickiaje kama kesho na keshokutwa wenzao wengine wakijiunga na cdm? Ukipewa nafasi ya kuongea jiongelee mwenyewe na c wengine, mtakuja pata aibu ya uzeeni bure
 
Tanzania tunapoteza muda kwenye mambo madogo ambayo hayana tija hata tone. Yaani ukipita kwenye mitandao ni hoja za ajabu ajabu tu. Ukiwakuta wanasiasa majukwaani nao ni hoja za kitoto tu wanahangaika nazo!

Ifike mahali tubadilike mawazo yetu. Hili la wazee wa EAC kuhama au kutokuhama sio ishu kubwa kivile! Wao waendelee kusubiri mafao yao milele! Mafao gani yasiolipika kwenu tu, ili hali wengine wanalipwa bhana?? Nyie wazee kama mngekua mna thamani kwa serikali mngekuta mshalipwa hela yenu! Hebu waulizeni kina Sumaye, Msuya, Malechela kama nao wanadai mafao yao.
Mkipata majibu ndo mjiulize thamani yenu kwa CCM. Na mjiulize pia wao na nyie wazee wa EAC ni nani alianza kulitumikia Taifa zaidi ya mwenzake.
Mkipata majibu kuwa ninyi ndo mlioanza na hamjalipwa hadi leo, basi mtathmini thamani yenu.
 
BAADHI ya wazee wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wamesema hawalitambui kundi la watu waliojiunga na Chadema wakidai kwamba ni viongozi wa jumuiya hiyo na kukanusha taarifa kwamba wastaafu wengine wako mbioni kujiunga na chama hicho cha siasa.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wastaafu 13 waliokuwa wamewakilisha wenzao walisema kuwa uongozi wanaoutambua ni ule wa watu saba uliopo Mahakamani na wengine wanaojiita viongozi wa jumuiya hiyo wamelenga kuwarubuni wazee hao.
Akisoma tamko lao kwa niaba ya wenzake, Gregory Sandaria alisema kuwa wameguswa na taarifa iliyotolewa na wastaafu wenzao katika gazeti moja la kila siku (Si HabariLeo), kwamba viongozi hao wameamua kujiunga na Chadema na wastaafu wengine wako mbioni

"Kauli hiyo ya wastaafu hao sita viongozi wa kikundi cha EACORA wakiongozwa na Benjamin Mutembei na Jonas Musokwa picha yao ilipewa hadhi kubwa kwa kuwekwa katika ukurasa wa mbele wa gazeti hilo tena kwa kutumia umaarufu wa wastaafu wa EAC na sio vyama vyao vya siasa walivyo hama, ina utata," alisema.

Alisema "Hatuna tatizo la wao binafsi kujiunga na Chadema au chama chochote kingine cha siasa kwani uamuzi huo ni wa mtu binafsi.”

Alisema kinachowasumbua ni staili waliyotumia ya kujiunga na chama hicho kwa kutumia umaarufu wa jina la wazee wastaafu wa EAC ambayo imeleta hisia potofu kwa jamii na hasa wadadisi wa mambo ya kisiasa hapa nchini.

Tunapenda kutamka kwamba hakuna kikao cha wastaafu tulichokaa kwa ujumla wetu na kujadili mapendekezo hayo na kisha uamuzi ukatolewa kwamba wastaafu wa EAC wajiunge na Chadema kama inavyodaiwa na wenzetu hao,” alisema.

Tunaomba ieleweke kwamba, Umoja wa Wastaafu wa EAC haukusajiliwa kama chama rasmi, bali umoja ulisajiliwa na wastaafu 17,746 na kuwaunganisha waliokuwa wafanyakazi wa EAC, GFS pamoja na mashirika yake ya EARC, EAHC, EACHS, EAP&T na EAAC baada ya kuvunjwa kwa EAC mwaka 1977,” alisema

Sandaria alisema walilazimika kujiunga ili kujenga nguvu za pamoja kwa nia ya kuikabili Serikali ambayo kwa sababu inazozijua yenyewe bado haijawalipa kikamilifu mirathi au haki zao za msingi zilizotokana na ajira zao

Taarifa hiyo imetolewa na kusainiwa na wawakilishi wa wazee hao ambao ni Sandaria, Yusuf Hamsini, Alfred Carere, Mbayo S.M.J, Asumbile Mwambona, Abdallah Masondole, Athuman Mwilima, KessY Gerald na Michael Peter.

Source: Habarileo tarehe 23 feb 2012.

Mytake: CHADEMA IACHE TABIA YA KUTAFUTA POLITICAL GAIN KWA KUPITIA MIGONGO YA WAZEE WETU, KUFANYA HIVYO KUTAWAKOSESHA WAZEE HAKI YAO.

ADC- Kwa maendeleo ya Taifa.
mosi,chadema imekuwa maarufu hata kabla ya hao wazee kujiunga,pili,watakosaje haki zao kama zipo?kujiunga chadema ndio kukosa haki?u are too myopic........
FIKIRI KWA KUTUMIA AKILI NA SIO MASABURI

 
Mkuu mimi kosa langu nini nimenakiri tu habari na kutoa ushauri wangu

Sasa kama umenakiri huo ushauri unaupata wapi? At least ungesema "kama ni kweli" basi ndo ukatia huo ----- wako. Wawe wamejiunga au la, ukweli ni upi? Wamelipwa? Na je hawajachoka?
 
poleni wastaafu mtaendelea kutaabika hadi mtakapo ionja mauti maana mmeamua kuchagua hilo fungu

awa wazee bado wopo chini ya kongwa la utumwa la ccm,wanadhani,wakiwakana wenzao ili kujipendekeza kwa ccm,ndio watapewa haki zao,haaaaaaaaaaaaaaaaaaa,mtumwa,ni mtumwa tu,
 
Nimeguswa sana na namna habari Leo, Mhariri wake na uongozi wote kwa namna ubinafsi na njaa zao zinavyoweza kuchafua utu wa wazee wetu. Na hawa wazee waliokosa busara pamoja na umri wao mkubwa kufanya upumbavu wa kuongea hii pumba, pengine ndio Yale yakuwa unapozeeka akili zako zinakua za kijinga maana sisemi za kitoto kwa kuwa watoto wa kitanzania wa Leo hii wasingekubali kufanywa hiki. Hivi Kwa kutoa hii Kauli hawajioni wapumbavu ? Je sio Kweli walivuliwa nguo na kukaa uchi wa mnyama Mbele ya wajukuu wao kwa kutiwa unyonge na Hao wakina habari Leo? Sasa kwa unafiki huo ndio kesi iliyoko mahakamani ambayo hata sijui inahusu nini maana Kama kushinda walishsshinda na wanahabari Leo wakaamua kukatalia haki Yao, au ni kwa kuwa walipewa pilau ya siku mbili hizo ndio utu umewapotea kabisa. Poor wazee wa busara hata wanachoongea hakijulikani, Je wanakataa Hao waliojiunga na chadema si ex EAC workers? Hata muandishi Ku spin hajui kazi za kupeana ki makundi foolish
 
BAADHI ya wazee wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wamesema hawalitambui kundi la watu waliojiunga na Chadema wakidai kwamba ni viongozi wa jumuiya hiyo na kukanusha taarifa kwamba wastaafu wengine wako mbioni kujiunga na chama hicho cha siasa.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wastaafu 13 waliokuwa wamewakilisha wenzao walisema kuwa uongozi wanaoutambua ni ule wa watu saba uliopo Mahakamani na wengine wanaojiita viongozi wa jumuiya hiyo wamelenga kuwarubuni wazee hao.
Akisoma tamko lao kwa niaba ya wenzake, Gregory Sandaria alisema kuwa wameguswa na taarifa iliyotolewa na wastaafu wenzao katika gazeti moja la kila siku (Si HabariLeo), kwamba viongozi hao wameamua kujiunga na Chadema na wastaafu wengine wako mbioni

"Kauli hiyo ya wastaafu hao sita viongozi wa kikundi cha EACORA wakiongozwa na Benjamin Mutembei na Jonas Musokwa picha yao ilipewa hadhi kubwa kwa kuwekwa katika ukurasa wa mbele wa gazeti hilo tena kwa kutumia umaarufu wa wastaafu wa EAC na sio vyama vyao vya siasa walivyo hama, ina utata," alisema.

Alisema "Hatuna tatizo la wao binafsi kujiunga na Chadema au chama chochote kingine cha siasa kwani uamuzi huo ni wa mtu binafsi.”

Alisema kinachowasumbua ni staili waliyotumia ya kujiunga na chama hicho kwa kutumia umaarufu wa jina la wazee wastaafu wa EAC ambayo imeleta hisia potofu kwa jamii na hasa wadadisi wa mambo ya kisiasa hapa nchini.

Tunapenda kutamka kwamba hakuna kikao cha wastaafu tulichokaa kwa ujumla wetu na kujadili mapendekezo hayo na kisha uamuzi ukatolewa kwamba wastaafu wa EAC wajiunge na Chadema kama inavyodaiwa na wenzetu hao,” alisema.

Tunaomba ieleweke kwamba, Umoja wa Wastaafu wa EAC haukusajiliwa kama chama rasmi, bali umoja ulisajiliwa na wastaafu 17,746 na kuwaunganisha waliokuwa wafanyakazi wa EAC, GFS pamoja na mashirika yake ya EARC, EAHC, EACHS, EAP&T na EAAC baada ya kuvunjwa kwa EAC mwaka 1977,” alisema

Sandaria alisema walilazimika kujiunga ili kujenga nguvu za pamoja kwa nia ya kuikabili Serikali ambayo kwa sababu inazozijua yenyewe bado haijawalipa kikamilifu mirathi au haki zao za msingi zilizotokana na ajira zao

Taarifa hiyo imetolewa na kusainiwa na wawakilishi wa wazee hao ambao ni Sandaria, Yusuf Hamsini, Alfred Carere, Mbayo S.M.J, Asumbile Mwambona, Abdallah Masondole, Athuman Mwilima, KessY Gerald na Michael Peter.

Source: Habarileo tarehe 23 feb 2012.

Mytake: CHADEMA IACHE TABIA YA KUTAFUTA POLITICAL GAIN KWA KUPITIA MIGONGO YA WAZEE WETU, KUFANYA HIVYO KUTAWAKOSESHA WAZEE HAKI YAO.

ADC- Kwa maendeleo ya Taifa.

Correction:
Source : Uhuru
 
Miaka zaidi ya 35 bado serikali yenu ya magamba inatafakari hoja za msingi za malipo ya wazee wa EAC?? Yani mmewanunulia ubwabwa hao wazee sita na kuwaandikia press statement wakaiwasilisha kwa mhariri wa umbealeo, oh no sorry habarileo.
Habari ndio hiyo wazee wameamua kuunganisha nguvu na Chadema kwakuwa wameridhika kabisa kwamba magamba ni matapeli na wauaji hawana mpango wa kuwalipa haki zao.

Mkuu Mwita Maranya hakuna kitu cha hatari kama njaa kuingia kichwani.
 
Chadema mkishindishwa kuwashawishi watoto wa sekondari waliofeli kuandamana nendeni kwa chekechea watawaelewa.
 
Mkuu mimi kosa langu nini nimenakiri tu habari na kutoa ushauri wangu

Kwani nani hajui kwamba Jamba leo,Uhuni aah Uhuru ni wasaidizi wa masalia?
Katika akiri ya kawaida ni mzee gani wa E.A aliyemwagiwa maji ya pilipili na CCM na kudhulumiwa,aishangilie CCM?hata babu yake Mwigulu haipendi CCM acheni porojo za mwaka 47.
 
Back
Top Bottom