Wana JF nipo katika mkutano wa CCM katika kijiji cha Ngabobo Kata ya Ngarenanyuki jimbo la Arumeru na mhutubiaji mkuu ni Ole Sendeka mbunge wa Simanjiro na Stephen Wassira Mbunge wa Bunda.
Wassira anasema akija hapa mtu akajitambulisha kwa jina la Nyerere mumfukuze maana anadanganya, Nyerere alishakufa na alikuwa CCM hakuna Nyerere CHADEMA na mtu wa huko Musoma alipozaliwa mwalimu Nyerere na anajiita tu hili jina.
Ole sendeka anasema Wamasai msikubali kuamuliwa na watu wa Musoma, wa Musoma wakae hukohuko kwao huku watuachie wenyewe.
Kibaj anasema mumchague Siyoi kwa kumsaidia ana mzigo mkubwa nyuma yake ana familia kubwa ahurumiwe ili asadie kulisha wanaomtegemea na Mungu atawabariki wote.
Mkutano unafungwa ila kuna makundi makundi yanapinga kauli hizo na wapo wanaokubali.
My Take: CCM hakuna hoja wala mtoa hoja ni vituko tupu
Ni mimi Mgeni wenu wa Jamii Forum