Wasomi wengi ni waoga

Wasomi wengi ni waoga

Mungu Mweusi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
1,474
Reaction score
1,086
Habari zenu wanajamii. Nimekuwa nikitafakari Mara kadhaa na pia kupata mawazo toka kwa wasomi tofauti juu ya nadharia ya kujiajiri. Suala hili inaonekana ni gumu sana sasa sijajua kwamba hawana akili za maisha, hawana mitaji, ni waoga, au hawajiamini. Mtu yupo tayari aajiriwe kwa sh.laki 5 lakini tu awe chini ya mtu. Je, tunawezaje kubadirisha kasumba hii?
 
Huyu Ditto ana matatizo, inaonekana hizi jazba zake zinaweza kuleta maafa mengine atapoendelea kubaki mtaani, bora tu angebaki segerea, we uliona wapi mtu mwenye akili kujibizana kwa hasira na wananchi kwenye mkutano?

Hata kufanya biashara kupata faida ya laki tano kwa mwezi si jambo haba.

Lazima hiyo biashara ichukue muda saana,

Wasomi wengi hatuna mtaji, hatuna elimu ya biashara husika sio kila aliyesoma chuo kasomea biashara. Mfano kuna vitu kama vile walimu, uhandisi, sheria, n.k vitu ambavyo ukimaliza chuo kama mtalam wa fani husika huwezi milik gafla kampuni ya sheria, au shule au engnering company.

Lazima ufanyekaz utafute mtaji na uzoefu husika,


Labda uulize kwanini walio ajiliwa hawaachi kazi na kujiajili? Wakat nao wanalipwa hizo hizo pesa ndogo????? ....

Kimsingi kwa vile hujapitia hali tuliyonayo graduate hujui hindrannce na strings zipi zinatuface.

Unaweza kuta tangu auanzekusoma paka umemaliza hujawah fuga, lima...duh gafla baada ya kumaliza chuo unaambiwa kalime.

So kuna mambo mengi saana yanayoweza mjenga mtu kujiajil katika kitufulani.

Necha ya elimu yetu ipo hovyooo saana inatuandaa kuajiliwa.


Wengi wanashindwa kwa kukosa uwezo binafsi, desa lina asilimia chache saana kwenye kujiajili
 
Edit title yako, umeconclude kuwa ni waoga lakini ndani unajiuliza maswali kibao.
Back to the topic. Kwanza sio wasomi wote huandaliwa wakajiajiri. Kuna wasomi wanaondaliwa wakaajiriwe, hawa watoe kweye kundi hilo. Kwa wanaopaswa kujiajiri ni kweli wengi wana uwezo mdogo na shida inaanzia kwenye ubora wa elimu wanayoipata na pia mazingira ya kujiajiri sio mazuri. Mfano, kuna watu wana ideas lakini hawana mitaji wala sehemu za kupata mitaji.
 
Wengi wamekosa na hawajui wat they want in their life
 
msomi ni nani? tuanzie hapa kwanza.

minimum qualification ya msomi.

maana hata kabla ya wazungu tulikuwa na wasomi.
 
msomi ni nani? tuanzie hapa kwanza.

minimum qualification ya msomi.

maana hata kabla ya wazungu tulikuwa na wasomi.

Wote walioenda shule nadhan kwakuanzia tunaweza kusema hawa wa form four, walioshindwa kujiendeleza

Wale wa colledge mfano veta, certificate...

Nakuendeleaa
 
msomi ni nani? tuanzie hapa kwanza.

minimum qualification ya msomi.

maana hata kabla ya wazungu tulikuwa na wasomi.

Mkuu kwa uelewa wangu,msomi ni mtu yeyote aliyepitia shule na kupata mafunzo ktk nyanja furahi.
Lkn asiishie kupata mafunzo pekee bali kupitia mafunzo hayo aweze kutatua matatizo yanayohusu nyanja aliyoisomea na aweze pia kuitumikia jamii inayomzunguka.


Pia kupitia elimu aliyonayo aweze kuelimisha jamii kuhusu taaluma yake na jamii inufaike kupitia elimu yake au usomi wake alionao.
Hii sio general definition hiyo according to me
 
Kwanza kabisa kujiajiri ni hulka ya mtu binafsi, huwezi fundishwa sehemu yoyote ile jinsi ya kujiajiri, hata kama kama umesoma entreprenuership kama hauna hulka au msukimo binafsi toka ndani yako hautojiajiri kamwe,,,huitaji kua na elimu ya biashara ili kuendesha biashara, tatizo la wasomi wao ni ku psycho analyse kila kitu anakipigia hesabu na mwishoni anaconclude aaah hii biashara nitapata hasara...waajiriwa wengi hawawezi kuacha kazi kujiajiri sababu kwenye ajira kuna security, kwamba hata hali iweje 500,000 yake ipo kwenye kujiajiri leo waweza pata 30,000 kesho 70,000 kesho kutwa 10,000 siku ingine 0 siku zingine zaidi kabisa...kwaio mtu anajikuta hawezi...
 
Kwanza kabisa kujiajiri ni hulka ya mtu binafsi, huwezi fundishwa sehemu yoyote ile jinsi ya kujiajiri, hata kama kama umesoma entreprenuership kama hauna hulka au msukimo binafsi toka ndani yako hautojiajiri kamwe,,,huitaji kua na elimu ya biashara ili kuendesha biashara, tatizo la wasomi wao ni ku psycho analyse kila kitu anakipigia hesabu na mwishoni anaconclude aaah hii biashara nitapata hasara...waajiriwa wengi hawawezi kuacha kazi kujiajiri sababu kwenye ajira kuna security, kwamba hata hali iweje 500,000 yake ipo kwenye kujiajiri leo waweza pata 30,000 kesho 70,000 kesho kutwa 10,000 siku ingine 0 siku zingine zaidi kabisa...kwaio mtu anajikuta hawezi...

kula like mkuu
 
No mtazamo mbovu wa wasomi wengi hapa bongo! Anaona fahari kuvaa smart kwenda kumfanyia kazi mwingine!
 
mmewapa mitaji mmeona wameogopa ku-invest?????
 
WanaJF ni kwamba nchi yetu haijaweka mazingira rafiki ya kujiajiri. Kama vile:-
1. Upatikanaji wa mikopo. Nenda benki ukatake kukopa mamilioni ili uanzishe shule, kampuni ama kilimo utapewa masharti magumu hutakaa urudi tena.
2. Miundombinu wezeshi ya kibiashara hakuna. Masoko ya bidhaa za kilimo, bidhaa za viwandani hayajaandaliwa na wala hayajalindwa ipasavyo. Utaishia kupata hasara tu. Zalisha nguo, sukari, vifaa vya majumbani utashindana na bidhaa za nje mpk ushindwe.
Miundombinu wezeshi ni pomoja na:-
(a) kodi rafiki
(b) nishati ya umeme ya kuaminika
(c) Sera nzuri za kulinda bidhaa za ndani
(d) miundombinu ya uchukuzi iliyo bora
(e) masoko ya kuaminika

Haya yangekuwepo nani angeajiriwa?
Lkn ukitazama haya kama msomi unaishia kuwa mpole tu.
 
Habari zenu wanajamii. Nimekuwa nikitafakari Mara kadhaa na pia kupata mawazo toka kwa wasomi tofauti juu ya nadharia ya kujiajiri. Suala hili inaonekana ni gumu sana sasa sijajua kwamba hawana akili za maisha, hawana mitaji, ni waoga, au hawajiamini. Mtu yupo tayari aajiriwe kwa sh.laki 5 lakini tu awe chini ya mtu. Je, tunawezaje kubadirisha kasumba hii?
wewe ulianzaje kwani?kujiajiri au kuajiriwa
 
Back
Top Bottom