MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,217
- 22,282
WASOMI MSIKATE TAMAA, ELIMU HAINA MBADALA
WanaJF natumaini mko wazima.
Nawasalimu katika jina la Chama Cha Mapinduzi, chama kiendelee. Leo nimeona nitumie haki yangu ya kikatiba kutoa maoni yangu kuhusu wasomi wa nchi hii. Siku za hivi karibuni kumezidi kutokea hali ya wengi kubeza wasomi kwamba elimu haijawasaidia wao wenyewe wala jamii zao kuinuka kiuchumi. Yaani kuanzia mtaani hadi bungeni wasomi wanabezwa. Inasikitisha sana. Utasikia jamaa ana masters lakini anagongea hela ya vocha.
Kwanza kabla ya kuendelea zaidi ningetoa ufafanuzi kuhusu wasomi ninaomaanisha hapa. Ninamaanisha wale wote waliofika chuo kikuu. Lakini katika hao wasomi pia tuwatoe wale wanaoshindwa kutofautisha R na L kwenye maandishi yao. Wale wanaoandika "awo" badala ya "hao", wale wanaotuma msg wanaandika xaxa, ki2, tante, tenkyu, nk. Pia kama huwezi kuongea kiingereza kilichonyooka kwa dakika tatu ninakutoa kwenye kundi la wasomi. Wasomi ninaomaanisha hapa ni walioelimika na walipokuwa chuo walifanya bidii. Yaani watu wanaojiamini kupitia usomi wao na wasio na mambo ya ovyo.
Wanaobeza wasomi ni kutoka lile kundi kubwa la watu ambao hawakubahatika kupata elimu nzuri kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo zilizo ndani na nje ya uwezo wa kibinadamu. Kuna ambao huenda walikosa elimu kutokana na kukosa namna baada ya kuondokewa na wazazi/walezi na sababu zingine kama hizo. Na kuna wale ambao hawana elimu ya kutosha kwa maana ya kufeli mitihani yao kwenye ngazi mbalimbali yaani WANAKESHA LAKINI HAWAPANDISHI. Haya makundi mawili kwa pamoja wanaunda kundi kubwa la watu wajulikanao kama VILAZA.
Lawama kuu kwa wasomi ni kuwa na vyeti vingi ila kipato duni. Na watoa lawama huenda mbali kwa kutoa mifano ya watu ambao hawakusoma lakini ni matajiri wakubwa. Niseme kwamba hao matajiri ni wachache mno... kundi la vilaza hutoa matajiri wachache mno. Na hata hao matajiri ukiwafuatilia wengi wao wamefika walipofika kupitia njia nyingi zisizo za kihalali. Pia biashara nyingi za matajiri kutoka kundi la vilaza hazina ubunifu wowote ndo maana wakipatwa na janga kidogo hufilisika kirahisi na kuishia kusema wamerogwa. Kundi la vilaza hutoa mafukara wengi sana ambao wanasiasa huwatumia kama mitaji. Na watoa lawama wengi ni wale maisha yamewashinda au hawajiamini. Kiasili hakuna kilaza anayeweza kujiamini mbele ya msomi. Matokeo hutumia ujanja wa kumvuruga msomi ili aingie mtego wa kujibizana nae. Wasomi wengi wako na maisha ya middle class.. sio matajiri wala maskini. Na bado wasomi sio wengi kwenye jamii. Bado nchi yetu inahitaji kutengeneza wasomi wengi zaidi. Hawa vilaza waliotapakaa kila kona ya nchi ndo wanafanya jitihada za kujikomboa zinakuwa ngumu.
Niwasihi wasomi wenzangu kwamba hata kama kwa sasa ana kipato duni asikate tamaa asonge mbele. Na wasomi tusiwe waoga kujitosa kufanya mambo makubwa. Wasomi ndo huleta mabadiliko. Kwa mfano msomi mwenzetu Fred Vunjabei anakimbiza vilaza kwenye nguo waliozoea kufanya biashara kimazoea. Hata CHADEMA enzi za uhai wake ilikuzwa zaidi na wasomi wa vyuo vikuu. Bila hivyo kile Chama kisingekuwa kikubwa kabla ya kifo chake. Nimalize kusema nchi haiwezi kwenda mbele bila wasomi ila inaweza songa mbele bila vilaza.
WanaJF natumaini mko wazima.
Nawasalimu katika jina la Chama Cha Mapinduzi, chama kiendelee. Leo nimeona nitumie haki yangu ya kikatiba kutoa maoni yangu kuhusu wasomi wa nchi hii. Siku za hivi karibuni kumezidi kutokea hali ya wengi kubeza wasomi kwamba elimu haijawasaidia wao wenyewe wala jamii zao kuinuka kiuchumi. Yaani kuanzia mtaani hadi bungeni wasomi wanabezwa. Inasikitisha sana. Utasikia jamaa ana masters lakini anagongea hela ya vocha.
Kwanza kabla ya kuendelea zaidi ningetoa ufafanuzi kuhusu wasomi ninaomaanisha hapa. Ninamaanisha wale wote waliofika chuo kikuu. Lakini katika hao wasomi pia tuwatoe wale wanaoshindwa kutofautisha R na L kwenye maandishi yao. Wale wanaoandika "awo" badala ya "hao", wale wanaotuma msg wanaandika xaxa, ki2, tante, tenkyu, nk. Pia kama huwezi kuongea kiingereza kilichonyooka kwa dakika tatu ninakutoa kwenye kundi la wasomi. Wasomi ninaomaanisha hapa ni walioelimika na walipokuwa chuo walifanya bidii. Yaani watu wanaojiamini kupitia usomi wao na wasio na mambo ya ovyo.
Wanaobeza wasomi ni kutoka lile kundi kubwa la watu ambao hawakubahatika kupata elimu nzuri kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo zilizo ndani na nje ya uwezo wa kibinadamu. Kuna ambao huenda walikosa elimu kutokana na kukosa namna baada ya kuondokewa na wazazi/walezi na sababu zingine kama hizo. Na kuna wale ambao hawana elimu ya kutosha kwa maana ya kufeli mitihani yao kwenye ngazi mbalimbali yaani WANAKESHA LAKINI HAWAPANDISHI. Haya makundi mawili kwa pamoja wanaunda kundi kubwa la watu wajulikanao kama VILAZA.
Lawama kuu kwa wasomi ni kuwa na vyeti vingi ila kipato duni. Na watoa lawama huenda mbali kwa kutoa mifano ya watu ambao hawakusoma lakini ni matajiri wakubwa. Niseme kwamba hao matajiri ni wachache mno... kundi la vilaza hutoa matajiri wachache mno. Na hata hao matajiri ukiwafuatilia wengi wao wamefika walipofika kupitia njia nyingi zisizo za kihalali. Pia biashara nyingi za matajiri kutoka kundi la vilaza hazina ubunifu wowote ndo maana wakipatwa na janga kidogo hufilisika kirahisi na kuishia kusema wamerogwa. Kundi la vilaza hutoa mafukara wengi sana ambao wanasiasa huwatumia kama mitaji. Na watoa lawama wengi ni wale maisha yamewashinda au hawajiamini. Kiasili hakuna kilaza anayeweza kujiamini mbele ya msomi. Matokeo hutumia ujanja wa kumvuruga msomi ili aingie mtego wa kujibizana nae. Wasomi wengi wako na maisha ya middle class.. sio matajiri wala maskini. Na bado wasomi sio wengi kwenye jamii. Bado nchi yetu inahitaji kutengeneza wasomi wengi zaidi. Hawa vilaza waliotapakaa kila kona ya nchi ndo wanafanya jitihada za kujikomboa zinakuwa ngumu.
Niwasihi wasomi wenzangu kwamba hata kama kwa sasa ana kipato duni asikate tamaa asonge mbele. Na wasomi tusiwe waoga kujitosa kufanya mambo makubwa. Wasomi ndo huleta mabadiliko. Kwa mfano msomi mwenzetu Fred Vunjabei anakimbiza vilaza kwenye nguo waliozoea kufanya biashara kimazoea. Hata CHADEMA enzi za uhai wake ilikuzwa zaidi na wasomi wa vyuo vikuu. Bila hivyo kile Chama kisingekuwa kikubwa kabla ya kifo chake. Nimalize kusema nchi haiwezi kwenda mbele bila wasomi ila inaweza songa mbele bila vilaza.