Ni jana Stephen Wasira alisikika kupitia vyombo mbalimbali vya habari akiwakana hadharani watoto wa kaka yake kuwa eti siyo binti zake. Sababu kubwa ya kuwakana huko ni pale Dr. Slaa alipotangaza jana yake kuwa mabinti wa mwanasiasa maarufu nchini wamejiunga na CHADEMA. Je Wasira,kuna aibu gani kwako kwa binti zako kujiunga na chama cha upinzani? Na je,ni kweli kuwa watoto wa kaka au ndugu yako siyo watoto wako? Hivi ukitengeneza "FAMILY TREE" ukianza na wazazi wenu,watoto wao(yaani wewe na kaka yako) na kumalizia na watoto wenu(wewe na kaka yako) bado hao hao hawatakuwa sehemu ya familia yako? Licha ya hayo nimekushangaa zaidi pale ulipomwambia Dr. Slaa kuwa suala la mabinti hao kujiunga na CHADEMA siyo hitaji la watanzania kwa sasa. Je,wewe kutoa kauli hadharani ya kuwakana binti zako ndiyo hitaji letu watanzania kwa sasa? Tunaomba sana mh. Wasira punguza kukurupuka.:nono: