Wasioishiwa pumzi ya kuupinga ufisadi tunakutana hapa!

Ndiyo maana nilikuambia kuwa CCM walishammaliza Dr Slaa kwani sifa pekee aliyokuwa anajulikana nayo ni UFISADI.

Waliruhusu makusudi Ufisadi usemwe wazi na mzigo wote akabebeshwa Lowassa wakati siyo kweli.

Ukiniambia Escrow Lowassa alilamba ngapi? Ntailipia kadi yangu ya CCM. Ukiniambia fedha zilizopotea Wizara ya Magufuli Lowassa alikula ngapi? Tatizo lenu ni kutufanya hatuna akili kwa kutulisha upuuzi wenu kuwa Fisadi ni Lowassa peke yake. Nchi ni giza, miaka 10 ya Kikwete bado anaiacha nchi giza. Lawama apewe Lowassa aliyeondoka miaka 8 iliyopita.

Slaa alishapoteza umaarufu wake kwa namna moja au nyingine. Asingeliweza kushindana na CCM hata kidogo. Na ili kuonyesha hilo, serikali za Mitaa, Chadema walifanya vibaya sana. Hata wewe umelijua hilo na umeliandika hapa kwenye BOLD. Sasa ili kutibu hilo tatizo, LOWASSA kaja na kibao kimegeuka. Mnahemewa Kisogoni kwa mara ya kwanza.

Hata kwa Mbinde, safari hii lazima Lowassa awachukue.

https://www.youtube.com/watch?v=mnAlHuGWOFg

CCM ni baba wa UFISADI, kama kweli Magufuli ni mzalendo na Muadilifu kama mnavyompamba kwenye Mabango barabarani atwambie kwanini alikuwa dalali wa uuzaji wa nyumba za serikali, kwanini amenunua Meli chakavu kwa mabilioni ya pesa? kama taasisi iliyo chini yake Tanroads inanuka kwa rushwa je yeye kaponea wapi? Kwanini alikamata meli na kugawa Samaki ilihali alijua kwa kufanya hivyo anavunja sheria za kimataifa...ona sasa tunatakiwa kulipa billions kama fidia....je kwa mifano hiyo michache Unamtofautishaje Magufuli na UFISADI?
 
meningitis ukishaingizwa kaburini ndio mwisho wa maisha yako ya duniani na unaanza maisha mapya ya kaburini kusubiri siku ya hukumu. hakuna fisadi aliyepata nguvu kwani hakuna ithibati yoyote mpaka pale vyombo halali vya sheria vitakapothibitisha pasi na shaka. kwa mtazamo wangu kwa kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu basi vivyo hivyo ni hukumu ya Mungu kwa hiyo tuwachie watanzania wapiga kura wenye vichinjio wakatoe au wakapaze sauti zao ziwe hukumu zao siku ya tarehe 25 oktoba .
Naona mkuu unakuja kwenye njia sahihi.
Kwenye uchaguzi huu hatukutakiwa kupotezwa kwenye ajenda ya msingi ya kuwakataa kwa sababu ni mafisadi.

Nilitegemea Chadema na pengine Ccm iteue wagombea wake kwa kuzingatia uadilifu hasa hasa eneo la ufisadi.

Nilitegemea mwaka huu wa uchaguzi kuwa ni hukumu kuu ya wote wanaotuhumiwa kuwa mafisadi.

Sasa kuna mtu ghafla ghafla katutoa kwenye ajenda hiyo na kuifanya kutojadilika au kuifanya ya kawaida sana.

Sijayasikia haya mawe ya escrow,nyumba,epa,richmond yakivuma mara baada ya julai 28.

Madhara ya jambo hili sio madogo,sasa hivi hakuna anayemkumbuka 'tumbili' ambaye amefunguliwa kesi.

Mafisadi wamepata nguvu baada ya kuwa mapilot wa ndege iliyokuwa ituvushe dhidi ya ufisadi.

Ndio maana nakuja na hoja hii ya kutokuishiwa pumzi kamwe kwani kwa kufanya hivyo ni kukaribisha mikandamizo zaidi kutoka kwa mafisadi.

Na siku moja wajukuu watakuwa wanapiga viboko makaburi yetu.
 
meningitis ukishaingizwa kaburini ndio mwisho wa maisha yako ya duniani na unaanza maisha mapya ya kaburini kusubiri siku ya hukumu. hakuna fisadi aliyepata nguvu kwani hakuna ithibati yoyote mpaka pale vyombo halali vya sheria vitakapothibitisha pasi na shaka. kwa mtazamo wangu kwa kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu basi vivyo hivyo ni hukumu ya Mungu kwa hiyo tuwachie watanzania wapiga kura wenye vichinjio wakatoe au wakapaze sauti zao ziwe hukumu zao siku ya tarehe 25 oktoba .

Watoe hukumu wakiwa wanaelewa Ukweli.
Ukweli ni huu
https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=122460
Mbowe alikiuza chama mwaka 2011
Angalia uzi na kuna mwingine
Kila kilochoandikwa mwaka 2011 kimekuja kutimia 2015
Bado unakataa ukweli ulio mbele yako?
 
Na bado Magufuli na Lowassa nawaweka kapu moja, wote ni MAFISADI hadi tarehe 25/10.

Mie ni CCM na kadi ninayo. Chadema wala kadi sina.... Siupendi Ufisadi ila kwa hali ilivyo sasa, lazima niwe na mtu yeyote aliyepo Chadema ili kusaidia kuipumzisha CCM.


Atakayeshinda kuwa Rais, ntampa heshima zangu zote na kumtetea kwa meno na mateke ikiwa Mburula yeyote atamshambulia hadi uchaguzi utakapokaribia, basi ntaanza tena kumsulubu.

Mengine soma hapo juu nilivyoandika. MUNGU IBARIKI TANZANIA.

labda sikubalianai na mengine mengi ulioyasema ila hii nilio highlight ndi msimamo na mtazamo wangu!atakaeshinda atakua rais wangu na kwa nguvu zote nitamtetea asidhurike,hususan na watu wa nje.ila uchaguzi ukifika nitakua wa kwanza kumsulubu alipokosea....
 
Clinton na Obama walipandishiana sana kwenye uchaguzi. Mwisho wakawa wote ofisini. Ndiyo Demokrasia.

labda sikubalianai na mengine mengi ulioyasema ila hii nilio highlight ndi msimamo na mtazamo wangu!atakaeshinda atakua rais wangu na kwa nguvu zote nitamtetea asidhurike,hususan na watu wa nje.ila uchaguzi ukifika nitakua wa kwanza kumsulubu alipokosea....
 
Clinton na Obama walipandishiana sana kwenye uchaguzi. Mwisho wakawa wote ofisini. Ndiyo Demokrasia.

Mkuu ule uzi wa 2011 sijakuona ukichangia! Hivi ishu ya Obama na Hillary unalinganisha na nini? Labda ungetoa mfano wa Romney kuhamia Democratic party na kufanya kazi na Obama. Mfano wako wa Hillary na Obama ni kama Magufuli afanye kazi na Membe au Mwandosya baada ya uchaguzi.
 
Daima Mbowe atabaki msaliti kwangu na nchi yangu Tz itabaki mbele kwa wote wanaoitakia mema, fisadi kwangu atabaki fisadi na fisadi hana dini wala kabila kwangu Karamagi, Rostamu, Lowassa, Chenge, Mama Tibaijuka, Mengi watabaki mafisadi tu na sitakuja kuibadirisha kauli yangu dhidi yao hata siku moja
 
Kwa maoni yangu kukataa kumshika mkono Tibaijuka Ngeleja na Chenge wasafi waliopitishwa na CCM kugombea Ubunge ni Unafiq category A... Kushikwa Mkono na alieuza Viwanda na kujigawia Migodi ni Ujuha ... Kugawana Nyumba za Serikali zenye viwanja vyenye thamani kubbwa ni Ujambazi wa mali ya Umma .... Mimi nafamilia yangu hatudanganyiki kwani tunajua kuwa mfumo wa CCM ndo UFISADI wenyewe ...
 
susuviri kwa ukweli wako huohuo watanzania wapenda mabadiliko wenye vichinjio watatoa hukumu oktoba 25 na ningekushauri ufanye kazi ya ziada kuwashawishi wabadili mawazo yao..jambo ambalo haliwezekani
Watoe hukumu wakiwa wanaelewa Ukweli.
Ukweli ni huu
Mbowe kuiuza CHADEMA kwa mafisadi
Mbowe alikiuza chama mwaka 2011
Angalia uzi na kuna mwingine
Kila kilochoandikwa mwaka 2011 kimekuja kutimia 2015
Bado unakataa ukweli ulio mbele yako?
 
Tatizo unaonekana umekariri na kufikiri hii ni Bongo Star Search. Uzuri unawakilisha asilimia ndogo ya wapiga kura. Ila asante kwa kutushtua kuwa elimu ya raia muhimu!

Elimu ya uraia nimepata na ndiyo inayonifanya nijitambue na kufata utashi wangu bila kuyumbishwa na mtu yoyote,inaonekana we ni mfuatiliaji mzuri sana Wa bongo star search mwakani jaribu Bahati yako unaweza kuopoa hela za kina Salama, Elimu ya uraia muhimu sana na wewe nakusihi itafute, narudia tena huyo huyo mwizi ndio chaguo langu na familia yangu .
 
susuviri kwa ukweli wako huohuo watanzania wapenda mabadiliko wenye vichinjio watatoa hukumu oktoba 25 na ningekushauri ufanye kazi ya ziada kuwashawishi wabadili mawazo yao..jambo ambalo haliwezekani

Mkuu never say never. Maadam tutaendelea kuwa pamoja Mungu akitujalia basi tutaendelea na mjadala. Ila naamini wapiga kura kiasi tena si ndogo hawajaamua kwa uhakika.
 
nauchukia ufisadi na MAVAZI YAKE YOTE!!! inasikitisha Chadema PESA wametawala CHADEMA Asilia. sasa hivi hawazungumzii rushwa wala UFISADI!!!
 
nauchukia ufisadi na MAVAZI YAKE YOTE!!! inasikitisha Chadema PESA wametawala CHADEMA Asilia. sasa hivi hawazungumzii rushwa wala UFISADI!!!

Watafute kwanza wale kumi na ushee walio ccm wape adhabu kali na uje kwa yule aliyehamia chadema, si unakumbuka List of shame?
 
nauchukia ufisadi na MAVAZI YAKE YOTE!!! inasikitisha Chadema PESA wametawala CHADEMA Asilia. sasa hivi hawazungumzii rushwa wala UFISADI!!!

Nyie mafisiem mnaojifanya mnazungumzia UFISADI mmechukua hatua gani wakat mmeshikilia dola.. kama kweli mnauchukia ufisad tungesikia mafisad wote wameshtakiwa, sio umeshiba kiporo halaf unatuandikia utumbo..
 
Ufisadi una nguvu sana.Yani wana wa mafisadi wameshaivamia thread na kuhakikisha wanawalinda na kuwatetea baba zao mafisadi kwa nguvu zote.
Nachukia fisadi bila kujali chama alipo.
 
Watafute kwanza wale kumi na ushee walio ccm wape adhabu kali na uje kwa yule aliyehamia chadema, si unakumbuka List of shame?

no, tuanze na anayetaka nchi yote kwanza, alafu tutafuatilia wale wanaotaka kurudi mjengo na kisha tutamalizia na wale walioachishwa kazi.
 
no, tuanze na anayetaka nchi yote kwanza, alafu tutafuatilia wale wanaotaka kurudi mjengo na kisha tutamalizia na wale walioachishwa kazi.

Haha Mkuu umejibu vizuri. Wao wanalia na wanaowania majimbo ili tusijikite katika kufuatilia atakayekalia kiti kikuu cha kifalme!?
Hapana acha tuwaweke pembeni hawa wadogo na tumjadili huyu mkubwa. Na anatumia pesa chafu na haramu kufanikisha nia na lengo lake!
Ufisadi wake tutakuja kuufichua hata uchaguzi ukimalizika!
 
Back
Top Bottom