Wasio na vitambulisho vya uraia kutoruhusiwa kumiliki simu

Hao NIDA wanadhani kuna mwananchi asiyetaka kuwa na kitambulisho? La hasha. Tatizo ni NIDA kukosa ubunifu wa kufanya kazi kwa ufanisi.

Tumejiandikisha, tena kwa tabu kubwa sana ya kushinda vituoni, na bado vitambulisho hatupewi. Mie nilijiandikisha awamu ya kwanza na kupigwa picha. Miaka imepita lakini bado sina hicho kitambulisho cha taifa. Ila nina passport.

Huu "ugumu" uko kila sehemu ya serikali Tanzania. Nilikwenda TRA nikashindwa kulipa kodi ya jengo kwani "taarifa walizokusanya mwaka jana bado ziko kwenye makaratasi kama unavyoyaona, bado hazijaingizwa kwenye kompyuta" . Baadaye utawasikia wakigomba kwamba hatutaki kulipa kodi za majengo.

Mheshimiwa Rais, hiyo civil service yako ni mbovu kila mahali. Ifanyike kitu kinaitwa "spill and fill" kila idara. Yaani wanaachishwa wote idara kwa idara, nafasi zinatangazwa na kujazwa upya. Walioachishwa wanashindanishwa na waombaji wapya.
 
Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inaruhusu mtu kuolewa akiwa na miaka 14 kwa kibali cha wazazi ina maana mke hatoweza kumiluki simu ya kuwasiliana na mumewe!

Kuna ajira inaruhusiwa mtu mwenye miaka chini ya 18 kufanya kwa vubali maalum, kwa hiyo ina maana Kutokuweza kumiliki simu kwa mtu wa aina hii atashindwa kufanya mawasiliano mbalimbali.

Kuna suala la ulinzi na usalama, simu zinawezesha mtu kuripoti na kuomba msaada polisi pindi mtu akiwa hatarini ina maana utaratibu mpya wa NIDA utawasumbua.

NIDA wawe makini kwa sababu watajikuta watoto wengi wanainflate miaka yao ili waonekane wana miaka 18 kwa ajili ya kupata kitambulisho hicho kusudi waweze kusajili laini za simu
inatakiwa walipitie upya
 
Rose-Mdami-640x373.jpg


.

Lengo La Mpango Huo Ni Moja Tu, Ili Yule Coward anayedundwa na Kiroho Kuwa Watu Milioni 55 wanamsemaje, Aweze Kusikiliza Simu zaidi akijua Moja kwa Moja Ni ya Huyu. Kisha Akisikia Tu Jina lake linatajwa Vibaya basi Huyu Mhanga anaishia Kwenye Kiroba! Reffer Samwel Doe na Cyprian Habyarimana, Ukiweka Watu kwenye Viroba iko Siku na Wewe hizo Viroba Zitakuhusu! Na Kwa Kesi yako Mungu alivyomtemi, Unaliwa na Samaki ili Litimie Neno La Kujilaani Wenyewe, "IKULU HAKUNA BUDGET YA MAZISHI" Kwa Maneno ya Kinywa Chako Utahukumiwa!
 
Serikali Hii waongo sana... technology iliyopo Tz haiwezi kuzidi technology ya USA
Acheni kuwatisha watu na sheria zenu uchwara
Na hivi sura zenu mnaziuza kama peremende sijui mwisho wake
Tz inaendeshwa kama shule ya msingi
******
Msio na vitambulisho nunueni line kwa internet mambo mswano Mawasiliano kama kawa waacheni wahangaike
Hapo mnakaribisha wezi na majambazi period!
 
Serikali Hii waongo sana... technology iliyopo Tz haiwezi kuzidi technology ya USA
Acheni kuwatisha watu na sheria zenu uchwara
Na hivi sura zenu mnaziuza kama peremende sijui mwisho wake
Tz inaendeshwa kama shule ya msingi
******
Msio na vitambulisho nunueni line kwa internet mambo mswano Mawasiliano kama kawa waacheni wahangaike
Hapo mnakaribisha wezi na majambazi period!
Au Kapateni Line za Simu Kenya. Gharama Inaweza Kuwa Kubwa Kidogo Lakini Unaishi kwa Amani
 
Hili limekua gum kwa wanachuo wengi hawajajisali kupatwa HIV vitamulisho vya taifa kwan wakati zoez likiendelea tulikua chuon na mikoa mingi washamaliza wakat ndo tunenda likizo
So sad!
 
TUTAKWENDA MAHAKAMANI KUBATILISHA AGZO LAKE KWA KUWA LIPO KINYUME NA KATIBA. ANAMAANISHA MTU MWENYE UMRI CHNI YA 18 ASIWE NA CM?? ID ZENYEWE MWAKA MZMA NDO UNAIPATA
 
Kwanini hawana mashine kama za vitambulisho vya mpiga kura ili ukimaliza umemaliza na kitambulisho unapata hapo hapo
 
Hii nchi inachekesha sana.
Je ni umri gani kisheria mtu anaruhusiwa kuajiriwa/ kujiajiri?
Je ni umri gani ambao mtu anaruhusiwa kuandikisha kitambulisho cha uraia? Ni miaka 18.
Kuna vijana wengi sana chini ya miaka 18 wanalea familia zao, kwa kufanya biashara ndogo ndogo. Unapomnyima haki yake ya kuwasiliana unataka Aishi vipi?
TCRA Na nida mmekurupuka


Mkuu usijifanye kuwa mjinga kiasi hicho kuliko ulivyo. Maswali yako yote uliyo yauliza majibu yake unayo.

Hao vijana wanao lea watoto zao watawatumia wazazi wao kufanya hiyo mikataba ya simu. Mbona ni kitu ambacho kina eleweka? Inaonekana kama vile wewe hujishughulishi na mambo ya sheria ya nchi yako vile! Ndiyo maana unawaza na kuandika madude ambayo hata mtoto wa darasa la pili anayaweza. Komaa kidogo.

Vijana chini ya miaka 18 wanaweza wakatumia vitanbulisho vya shule pia.
 
Sheria za ajabu ajabu ambazo zinawapa mianya watu watafute namna ya kuzivunja ili wanufaike. Hakuna nchi yoyote ile duniani ina sheria ya kipuuzi kama hii!

Kumiliki simu na kitambulisho cha uraia wapi na wapi!!!


Acha kusema Mambo ambayo huyajui wewe! Nchi zote zilizoendelea huwezi ukafanya mkataba wa simu, I mean line, bila kitambulisho. Ni Tanzania tu nafikiri ambako kitu kama hicho kimekuwa possible.

Sema tu nyie hamjazoea utaratibu. Mnataka maendeleo ya wazungu kwa principles za Jungle. Amka mkuu kila kitu kina enda na wakati. Mtayashuhudia mengi siku za mbele. Mnatakiwa mjiandae vizuri. Kuishi kiholela holela kuna mwisho.

Nchi za wenzetu zina systems. Kila mtu yuko katika system. Hatuko katika nchi ya migomba ya ndizi. Sisi ni binadam ni lazima tujijengee utaratibu wa maisha vinginvyo ni matatizo.

Tatizo lenu nyie mlidanganyika sana na mkwere yule. Hakuwa Rais mzuri. Hakujua wajibu wa kuwa Rais ni nini? Laiti kama angejua haya mambo asinge yaachia yaende hivyo.

Ulimwengu umebadilika mkuu. "Usione mbachao kwa msala upitao" Mazuri unayo yaona ya wazungu yana mambo ambayo yamejificha!
 
Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inaruhusu mtu kuolewa akiwa na miaka 14 kwa kibali cha wazazi ina maana mke hatoweza kumiluki simu ya kuwasiliana na mumewe!

Kuna ajira inaruhusiwa mtu mwenye miaka chini ya 18 kufanya kwa vubali maalum, kwa hiyo ina maana Kutokuweza kumiliki simu kwa mtu wa aina hii atashindwa kufanya mawasiliano mbalimbali.

Kuna suala la ulinzi na usalama, simu zinawezesha mtu kuripoti na kuomba msaada polisi pindi mtu akiwa hatarini ina maana utaratibu mpya wa NIDA utawasumbua.

NIDA wawe makini kwa sababu watajikuta watoto wengi wanainflate miaka yao ili waonekane wana miaka 18 kwa ajili ya kupata kitambulisho hicho kusudi waweze kusajili laini za simu

Sikuelewi? Si atatumia kitambulisho cha mme wake. What kind of an argument is this one?
 
Lipo tatizo pahala msajili wa biashara na makampuni BRELLA, tayari wameweka mfumo kutambua kitambulisho cha taifa pekee,ktk mfumo kujisajili online! Sijui asilimia ngapi Watanzania wamepata ID tayari?!
 
Lipo tatizo pahala msajili wa biashara na makampuni BRELLA, tayari wameweka mfumo kutambua kitambulisho cha taifa pekee,ktk mfumo kujisajili online! Sijui asilimia ngapi Watanzania wamepata ID tayari?!


Nina uhakika wahusika watakuwa wanalitafutia ufumbuzi.
 
NIDA hii hii au nyingine tatizo la Hawa watu Sasa hivi wamepoteza kabisa mwelekeo badala yake wanafocus kwenye mambo yasiyo Na tija Na wazi hapa wanatoa matamka haya wakiendeshwa Na siasa kutaka thibiti watu mitandaoni lakini wamesahau kwamba NIDA inauwezo mdogo sana zoezi la vitambulisho Dar tu limesuasua mpaka kero watu wanaandikishwa vitambulisho mpaka Leo hawajapata Na kingine hakuna utaratibu mzuri kwa wale wanaopoteza vitambulisho ama kweli ukianza angalia wengine unapoteza kabisa malengo yako
 
Back
Top Bottom