Wasifu wa Mama Salma Kikwete

Wasifu wa Mama Salma Kikwete

Status
Not open for further replies.
Sasa umeuliza ili iweje au unataka kumuajiri? au lipi alilofanya linalokulazimu ujue kiwango chake cha elimu? Ki ukweli mimi binafsi katika familia nzima ya President na watu wengine maarufu huyu mama mimi sina wa kumfananisha nae kubali kataa huu ndio ukweli Mungu amempa hekima na busara vinginevyo tungeaibika Tanzania
...wapi nime mkejeli? usitake kunilisha mawazo yako!
 
....Sina uhakika kama hili jambo la maana sana kulijua........halituhusu.......ni mawazo yangu tuu..
 
....Sina uhakika kama hili jambo la maana sana kulijua........halituhusu.......ni mawazo yangu tuu..

Ila ingekua elimu ya mbowe,lema au sugu lingekua jambo la maana na ungekua curious!
 
acha povu kama hujui kaa kmya... Elimu ya juu ni level ya grade A ya uwalimu(certificate)

pia ana ukiacha elimu ana ILMU ya madrasa.. ambayo imemuwezesha kuwa mtaalamu wa kusoma Quran kwa ufasaha na ustadi.

bora hata yeye anafani kunawengine wanatudanganya wako Cambridge university wengine form six za kimagumashi na ni viongozi wakubwa wakwenye chama chao, ila wafuasi wao wanakesha kuwapondea wenye elimu isiyo ya chuo kikuu..huwa na washangaa kupita kiasi
 
Naomba huyu mama asiwe mjadala hapa ni mama amewalea vijana na ni mke wa Rais pia nafikiri suala la kumjadili huyu sio sahihi .Haihusiani na siasa ni mtazamo tu.
 
Ukiachana na yeye kuwa mke wa rais mstaafu ndg Jakaya Kikwete, mkuu pale WAMA pamoja na kuwa mwalimu kwa wakati fulani lakini wasifu wake hatuna kabisa. Tafadhali mwenye wasifu wake uweke hapa tuweze kumfahamu huyu mtunga sheria wetu, alisoma wapi nk nk.

Hii ni nzuri hasa kujua uwezo wa viongozi wetu. Na nadhani baada ya malalamiko mengi kuhusu kummiss Kikwete naona Magufuli kaona amlete kupitia ubavu wake.
 
Una kusaidia nn huo wasifu wake pambana na maisha yako ya mtu muachie mwenyewe na mungu wake.
Hapana kaka povu la nini ... ni katika kuunga mkono juhudi za serilikali za kuhakiki vyeti na uwezo wa watu kulingana na elimu na nyadhifa zao
 
Mke wa Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete.
Mwalimu kitaaluma.
Mama wa taifa kwa kipindi cha miaka 10.
Mwanzilishi wa taasisi ya WAMA iliyojishughulisha na maendeleo ya kina mama katika nyanja tofauti mf. elimu
Mama wa Mh. Mbunge wa Chalinze Mwanasheria Ridhiwani J.Kikwete.
Mjumbe wa mkutano mkuu CCM
 
Huyu jamaa ameona watu wengi wameukumbuka utawala wa JK uliojaa utu hivyo ameona awaridhishe watu kwa njia hii. Pamoja na kwamba aliingia kwa mkwara wa kuuaminisha umma kwamba yeye ni bora kuliko aliyepita lakini mwenendo wake umedhihirisha kwamba hatii mguu kwa mtangulizi huyo. Kila kukicha watu wanamkumbuka JK. Huyu jamaa atakapoungana nasi uraiani sidhani kama ataheshimika kama walivyo baadhi ya watangulizi wake.
 
Huyu jamaa ameona watu wengi wameukumbuka utawala wa JK uliojaa utu hivyo ameona awaridhishe watu kwa njia hii. Pamoja na kwamba aliingia kwa mkwara wa kuuaminisha umma kwamba yeye ni bora kuliko aliyepita lakini mwenendo wake umedhihirisha kwamba hatii mguu kwa mtangulizi huyo. Kila kukicha watu wanamkumbuka JK. Huyu jamaa atakapoungana nasi uraiani sidhani kama ataheshimika kama walivyo baadhi ya watangulizi wake.
Msiwe waganga wa kienyeji kuguess suess. Unless mniambia aliyeteuliwa hastahili au haruhusiwi kikatiba. Ili mradi kigezo alichopewa Rais ni kimoja tu gender- labda na umri basi muacheni afanye kazi yake!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom