Wasifu wa Kamanda Emmerson Mnangagwa, Tanzania imemjenga vilivyo

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Habari wanaJF,

Nimeona ni vyema nikawapitisha kwenye wasifu mfupi wa ndugu Emmerson Mnangagwa ambaye anatajwa sana hivi sasa katika mgogoro wa kisiasa unaondelea katika nchi ya Zimbabwe.

1711151420-Who-Is-Emmerson-Mnangagwa.jpg

Alizaliwa mnamo tarehe 15 September, 1942.

Alisoma elimu yake ya O-Level na A-Level akiwa ni Mfungwa. Mwaka 1972 alimaliza kusoma Shahada ya Sheria katika Chuo Kikuu cha London na Postgraduate ya Sheria pia.

Mwaka 1962 alijiunga rasmi na chama cha Zimbabwe African Peoples Union (ZAPU) Kisha akaondoka kuja Tanzania kwaajili ya kambi ya mafunzo ya Kijeshi.

Mwaka 1963 Chama cha ZAPU kikamtuma tena kuja Dar es Salaam kisha nchini Misri kwaajili ya mafunzo ya Kijeshi.

Mwaka 1964 alimaliza mafunzo ya Kijeshi na kuunda kundi la 'Crocodile Group' ambalo lilikuwa kwaajili ya kusafirisha silaha kuingia Zimbabwe na kusajili wafuasi ambao wengi wao walisafiri kuja Tanzania kwaajili ya mafunzo.

Mwaka 1965 bwana Mnangagwa alikamatwa na kushikiliwa ambapo aliteswa na kuhukumiwa kwa makosa ya uhaini akafungwa miaka 10 ambapo alikuwa pamoja na Wanaharakati wengine akiwemo Rais Robert Mugabe.

Mwaka 1977 alichaguliwa kuwa msaidizi rasmi wa Rais wa ZANU na kuwa kiongozi wa Divisheni ya Kijeshi ndani ya Chama.

Baada ya ukombozi wa Zimbabwe alihudumu katika nafasi mbalimbali katika Baraza la Mawaziri la Zimbabwe ikiwa ni pamoja na Waziri wa Wizara ya Ulinzi, Sheria, na Masuala ya Bunge.

Ni mmoja kati ya Wanasiasa Matajiri nchini Zimbabwe.

Umoja wa Mataifa umewahi kumtuhumu kwa kujihusisha na biashara ya Almasi kinyume cha Sheria. Umoja wa Mataifa ukashauri awekewe vikwazo vya kusafiri na vya kiuchumi.

Mwezi Disemba mwaka 2014 Rais Robert Mugabe alimteua kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais baada ya kutengua uteuzi wa Joice Mujuru. Mujuru amekuwa hasimu wa muda mrefu wa bwana Mnangagwa katika vita ya kupigania madaraka.

Mnamo tarehe 06 Novemba mwaka 2017 Rais Robert Mugabe alitengua nafasi yake ya umakamu wa Rais na kuanza mchakato wa kumuweka Mke wake Bi. Grace Mugabe.

Ni hayo tu kwa ufupi.
 
Yan nchi wanaitoa kwa nyan wanampa ngedere, waafrika bana,
Anyways acha sisi tupambane na wakwetu huku bongo
 
Watu wamelala maporini huko; wamesota jela miaka na miaka; wamemwaga jasho na damu; wamepata vilema vya maisha; wamepoteza hadi familia, ndugu, na marafiki kwa ajili ya ukombozi halafu "malaya" mmoja tu; simply ni "mzuri"; simply anamfulia mzee nguo za ndani; simply anamtia mzee joto; eti anautaka uongozi wa nchi! Pumbavu zake!
 
Habari wanaJF,

Nimeona ni vyema nikawapitisha kwenye wasifu mfupi wa ndugu Emmerson Mnangagwa ambaye anatajwa sana hivi sasa katika mgogoro wa kisiasa unaondelea katika nchi ya Zimbabwe.


Alizaliwa mnamo tarehe 15 September, 1942.

Alisoma elimu yake ya O-Level na A-Level akiwa ni Mfungwa. Mwaka 1972 alimaliza kusoma Shahada ya Sheria katika Chuo Kikuu cha London na Postgraduate ya Sheria pia.

Mwaka 1962 alijiunga rasmi na chama cha Zimbabwe African Peoples Union (ZAPU) Kisha akaondoka kuja Tanzania kwaajili ya kambi ya mafunzo ya Kijeshi.

Mwaka 1963 Chama cha ZAPU kikamtuma tena kuja Dar es Salaam kisha nchini Misri kwaajili ya mafunzo ya Kijeshi.

Mwaka 1964 alimaliza mafunzo ya Kijeshi na kuunda kundi la 'Crocodile Group' ambalo lilikuwa kwaajili ya kusafirisha silaha kuingia Zimbabwe na kusajili wafuasi ambao wengi wao walisafiri kuja Tanzania kwaajili ya mafunzo.

Mwaka 1965 bwana Mnangagwa alikamatwa na kushikiliwa ambapo aliteswa na kuhukumiwa kwa makosa ya uhaini akafungwa miaka 10 ambapo alikuwa pamoja na Wanaharakati wengine akiwemo Rais Robert Mugabe.

Mwaka 1977 alichaguliwa kuwa msaidizi rasmi wa Rais wa ZANU na kuwa kiongozi wa Divisheni ya Kijeshi ndani ya Chama.

Baada ya ukombozi wa Zimbabwe alihudumu katika nafasi mbalimbali katika Baraza la Mawaziri la Zimbabwe ikiwa ni pamoja na Waziri wa Wizara ya Ulinzi, Sheria, na Masuala ya Bunge.

Ni mmoja kati ya Wanasiasa Matajiri nchini Zimbabwe.

Umoja wa Mataifa umewahi kumtuhumu kwa kujihusisha na biashara ya Almasi kinyume cha Sheria. Umoja wa Mataifa ukashauri awekewe vikwazo vya kusafiri na vya kiuchumi.

Mwezi Disemba mwaka 2014 Rais Robert Mugabe alimteua kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais baada ya kutengua uteuzi wa Joice Mujuru. Mujuru amekuwa hasimu wa muda mrefu wa bwana Mnangagwa katika vita ya kupigania madaraka.

Mnamo tarehe 06 Novemba mwaka 2017 Rais Robert Mugabe alirengua nafasi yake ya umekamu wa Rais na kuanza mchakato wa kumuweka Mke wake Bi. Grace Mugabe.

Ni hayo tu kwa ufupi.

Natafuta ' logical connection ' kati ya Headline yako hapo juu na hii Thread Content yako siioni labda walioiona watanisaidia.
 
Na yeye ni wale wale alikuwa madarakani kwa serikali ile ile kwa miaka yote 37.
Yani wapigania uhuru ndiyo wanataka mpaka leo waendelee ongoza serikali hakuna really democracy hapo
Hata huyo Joice Mujuru hasimu wake nae ni walewale amehudumu kwenye serikali tangu 1983 ..na mumewe alikua ni mkuu Wa majeshi na akauwawa kinyama kwa kuchomwa moto ndani ya nyumba yaje..nilichokipata ama kujua ni kwamba Zimbabwe iko vzr sana kwenye usalama..prominent politicians wote ni zao LA system na ndio maana imekua ngumu kumtoa mzee baba!
 
Nilidhani ni mimi mwenyewe kumbe tupo wengi. Yani mtu kuja Tz tu pengine kwa siku au wiki kadhaa basi eti yadaiwa Tz imemjenga vyema!
Alianza kuja bongo kwaajili ya mafunzo mwaka 1962 hadi 1964 na bado aliendela kuja kuweka kambi na vijana wengine. Its easy to hate than to love. Human beings we are lazy so we prefer an easy route
 
Watu wamelala maporini huko; wamesota jela miaka na miaka; wamemwaga jasho na damu; wamepata vilema vya maisha; wamepoteza hadi familia, ndugu, na marafiki kwa ajili ya ukombozi halafu "malaya" mmoja tu; simply ni "mzuri"; simply anamfulia mzee nguo za ndani; simply anamtia mzee joto; eti anautaka uongozi wa nchi! Pumbavu zake!
Papuchi ina nguvu kuliko bunduki
 
Yaani onesha ni wapi TANZANIA IMEMJENGA VILIVYO!????

Maanake kwa sifa za kijinga hatujambo....
 
Watu wamelala maporini huko; wamesota jela miaka na miaka; wamemwaga jasho na damu; wamepata vilema vya maisha; wamepoteza hadi familia, ndugu, na marafiki kwa ajili ya ukombozi halafu "malaya" mmoja tu; simply ni "mzuri"; simply anamfulia mzee nguo za ndani; simply anamtia mzee joto; eti anautaka uongozi wa nchi! Pumbavu zake!
Pumbavu kweli kweli.
 
ZANU PF na ANC plus NRM Vikitoka madarakani CCM lazima isage meno maana itakosa pa kukimbilia
 
Kwa taarifa huyu jamaa ni worse than Mzee Mugabe tutarajie Zimbabwe Inarudi kwenye mkono wa Dikteta mbaya zaidi
 
Hajapikwa na Tz sana sana ameharibiwa tuu....miaka 75 sio ya kukomaa kuingia ikulu.Ni muda wa kutunza wajukuu.
 
Back
Top Bottom