Wasanii wengi kushabikia CCM,inaashiria nini?

Wasanii wengi kushabikia CCM,inaashiria nini?

Nikwasababu wametoka kiamaisha chinivya sera nzuri za CCM kuna nchi nyingine mfano Rwanda yaani wasinii hawasaminiwi ata kidogo.
 
mkuu usiwalaum wasanii tu kama wasomi wazima ma docta na ma phd yao wanaacha taaluma zao na kujitoa ufaham na kuingia ccm.

mkuu haina.mjadala hakuna anaye ipenda ccm kwa roho safi bali ni kwa masilai binafsi tu.

hao wa sanii huko wanafuata pesa tu mkuu ndio inawafanya uwaone hivyo.
na kwakuwa mziki ni kazi yao so why wakiitwa wafanye kazi na ccm wakatae?? wakati ndio kazi yao
 
Ngoja nisicomment chochote juu ya hawa wanaojiita wasanii lakini kwa akili ya kawaida ni kwamba wameamua kuwajoin Wasanii wenzao
 
Mkuu mi nadhani ni Elimu na uwezo wao wa kufikiri, lakini na mara nyingi ni hawa wanaoimba nyimbo za kulialia na mapenzi. Ila kwa wale wa hip hop ya ukweli na iliyosimama huwakuti wakifanya hivyo kwa sababu wanaupeo mkubwa wa kufikiri, mfano Fid Q, Mwana FA, n.k.

nadhani hujafatilia tu, mwaka 2010 wasanii hao wa Hip Hop uliowataja walikuwa kwenye kampeni na sura zao zilitumika katika posters za kuhamasisha watu kuichangia ccm.
Nadhani mioyo yao haiko CCM ila kwa kua walichukulia dili kama madili mengine ambayo yanawaingizia hela.
 
Malaria iki panda kichwani, najua dawa yake, lkn NJAA ikipanda kichwani si ajabu mtu na akili zake akatoa elfu 2 yake mfukoni kununua kadi ya CCM.

Wasanii wa bongo njaa kali
 
Ccm ni chama ambachoukipata kauongoz kadogo katika mfumo wa chama basi unatajirika
 
Hii ndio demokrasia. Uhuru wa kuchagua. Tatizo la wengi wetu wanalazimisha tufikiri kama wanavyofikiri wao . Ndio maana ma celebrities wengi wa Hollywood wanakifadhili chama cha Democrats na wala Republicans hawaoni ajabu. Bado tuna safari ndefu ya kuona kwamba kutofautiana kisiasa si uadui .Tunadiriki kushangilia mtu akifa. Mbunge Sugu na Lema wameonyesha ustaarabu mkubwa kiwajibu tofauti na wengi wetu hapa tumekalia kutukana na kejeli.
 
Kumekuwa na wimbi kubwa la wasanii wa Bongo fleva na Bongo Movie kushabikia CCM,tumeona wengi tena wale maarufu wakijitokeza waziwazi kwenye shughuli za CCM.Jambo la kujiuliza hivi ni kweli hawa wasanii wana mapenzi ya dhati na chama hiki au ni ubinafsi wao,au kwa kuwa wengi wao wana elimu ndogo hivyo kushindwa kuelewa matatizo makubwa yaliyosababishwa na CCM?

Mkuu umeshasema wasanii basi wengi wao ni usanii, pia baadhi yao shule ni ndogo wanakuwa hawajiamin wana ona bora wawe kwenye hicho chama ili waweze pata rizik
 
wasanii wengi ni njaa kali na kwavile CCM kuna pesa za kumwaga inabidi wajitoe ufahamu na kujifanya wanaipenda CCM ili wapige hela, sidhani kama kweli wanaipenda CCM kwa dhati kabisa. mfano Karamagi alivyokuwa akigawa pesa kwa waendesha bodaboda, akijitokeza msanii hapo kumsapoti Karamagi unadhani hatavuna mkwanja mrefu.
 
Jibu: Wasanii wengi kushabikia chama fulani inaashiria NJAA.
 
Ubinafsi unaochangiwa na njaa, kwa mtu anaye tafsiri maendeleo endelevu (sustainable development) hawezi kushabikia hiki chama. Unahitaji ubinafsi na kutojitambua uliopitiliza ili kuishabikia ccm.
 
Weweeee chama tawala kinalipa vizuri hakina longo longo...ukiingia kwenye system usafiri wa uhakika kwenda kuburudisha na unatumia muda mfupi...sasa wewe upandishwe kwenye gari kwenda kwenye shoo kigoma......wapi na wapi
 
Elimu ndogo sana hawa wasanii wa Tz wanachokuweza ni umalaya, kushabikia CCM, kujichubua, kuvaa Heleni, kukalikiti nywele na upumbavu wa aina hiyo. Sijawahi wala sintakuja nikae ninunue CD za bongo movie.
 
Weweeee chama tawala kinalipa vizuri hakina longo longo...ukiingia kwenye system usafiri wa uhakika kwenda kuburudisha na unatumia muda mfupi...sasa wewe upandishwe kwenye gari kwenda kwenye shoo kigoma......wapi na wapi

Kweli tuna safari ndefu,kama watu wanawaza hivi!!
 
Kumekuwa na wimbi kubwa la wasanii wa Bongo fleva na Bongo Movie kushabikia CCM,tumeona wengi tena wale maarufu wakijitokeza waziwazi kwenye shughuli za CCM.Jambo la kujiuliza hivi ni kweli hawa wasanii wana mapenzi ya dhati na chama hiki au ni ubinafsi wao,au kwa kuwa wengi wao wana elimu ndogo hivyo kushindwa kuelewa matatizo makubwa yaliyosababishwa na CCM?

Sio wanashabikia ccm, wanalamba pesa ya ccm inayomwagwa hovyo kwa kila anayeisifia hata kama imevurunda. Hata mie wangenifuata ningekula hiyo nikaimba kama inalipa kwa nini nikomalie umaskini? Wasnii wa bongo ni wajasiliamali sio kama waimbaji wa zamani walioimba kuifunza jamii "Kuleni kuku mayai mboga samaki maziwa, pa kulala pawe bora........; Dereva kagonga basi haaaaaa! Sawa hiyo?"
 
Back
Top Bottom