Wasanii wa taarabu waja na Usiku wa taarabu Kuthamini Mchango wa Rais Samia

Wasanii wa taarabu waja na Usiku wa taarabu Kuthamini Mchango wa Rais Samia

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
13,709
Reaction score
25,487
Mkurugenzi wa Chocolate Princes na Muandaaji wa Matamasha ya Taarabu Ndg. Mboni Masimba Akiwa na Mfalme Muziki wa Taarabu Mzee Yusuph Wameongea na Vyombo vya Habari Hapa Ukumbi wa Serena Hoteli jijini Dar Es Salaam.

Lengo Kubwa Hasa ilikua ni Kuwajulisha Juu ya Mkesha wa Taarabu, Watu Wote na Wapenzi wa Miziki wa Taarabu Na Wapenzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kuelekea Siku Kubwa ya Nchi ya Uzinduzi wa Kampeni Ambayo Itakuwa ni Siku Rasmi ya Uzinduzi wa Kampeni ya Mama Tarehe 27 Mwezi wa Nane Mwaka Huu, Litafanyika Tamasha la Mkesha Viwanja vya Posta Kuanzia Saa10 jioni Mpaka majogoo.

Kwa Kuthamini Mchango wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkeshaa Huu Ni Alama ya Kusapoti Juhudi Zao Usiku Muhimu Usiku wa Mwambao Ambapo Wasanii Wa Taarabu Maarufu Watakuwepo Kutumbuiza na Baadhi ya Wasanii Hao ni Khadija kopa, East African Melody,Mzee Yusuph, Bi Mwanahawa Ali, Ishaah Mashauzi na Wengine Wengi.

Screenshot_20250823_220835_Instagram.jpg
 
Kila siku Kabla ya kulala nyosha mikono juu sema "nchi ya kipumbavu sana hii" mara tatu.
 
Nchi inaongozwa kwa adabu za kale, kila mtu shikamoo, yaani ni unaafiki mtupu.
 
Hapa kikubwa kila mtu afanye mambo yake anayoona yanamfaa. Kuna watu wanapata hasira kwa wanayofanya wengine, kwa Tanzania utakufa na ugonjwa wa moyo
 
Kila siku Kabla ya kulala nyosha mikono juu sema "nchi ya kipumbavu sana hii" mara tatu.
Hakika. Hwa wanasema ''nchi hupata viongozi inayostahili''. Ukienda sehemu ukikuta kiongozi ni mjinga au mvivu basi ujue wananchi wake nao ni wavivu na wajinga... la sivyo wasingeruhusu awe kiongozi wao.
 
Hapa kikubwa kila mtu afanye mambo yake anayoona yanamfaa. Kuna watu wanapata hasira kwa wanayofanya wengine, kwa Tanzania utakufa na ugonjwa wa moyo

Inaitwa freedom of speech, kila mtu aseme atoe la moyoni. Kwa Tanzania, hapa JF ndio mahala salama kidogo
 
Mkesha wa taarabu wa samia.
Basi sawa Kila la heri,kiingilio bei Gani
 
Wananchi wako bize na mama Samia
CCM wanalazimisha furaha, japo hata wao mioyo yao inatoa machozi.

Mimi nawashauri, kama kweli wanakubalika (wanavyodai). Wafanye kampeni kama zile enzi za Mkapa na Kikwete. Hakuna kusomba watu na magari wala pikipiki. Watumie hamasa ya matangazo, na mtu asilazimishwe kwenda kwenye mkutano.

Wakijaza mafuriko, hata mimi nakuwa chawa rasmi.

NB: Najua hawawezi kufanya hivyo hata jua likichomoza magharibi na kuzama mashariki. Sababu za kutokufanya hilo, wanazo na zinajulikana.
 
Mkurugenzi wa Chocolate Princes na Muandaaji wa Matamasha ya Taarabu Ndg. Mboni Masimba Akiwa na Mfalme Muziki wa Taarabu Mzee Yusuph..
Wanasemaje juu ya wizi wa kura, ufisadi, utekaji, mauaji ya wananchi, nk??
 
Back
Top Bottom