Warioba usiwatishe Watanzania!

Ni vema tukaelewana kuhusu misamiati tunayotumia kwenye huu mjadala. Baada ya kupitia michango mbalimbali, nimeona uelewa wetu wa neno “serikali” unatofautiana.

Tunaweza kukubali kutumia neno “serikali” kama “primitive term”, maana hatuwezi kutoa definition ya kila neno. Ziko primitive terms nyingi kwenye lugha zote. Line, plane, point, etc. are some examples of primitive terms in Euclidean Geometry.

Kwa sasa Tanzania kuna serikali ngapi? Sio mbili tu. Kila wilaya ina serikali yake. Mkuu wa serikali ya wilaya ni DC. Hachaguliwi kidemokrasia lakini hilo ni tatizo tofauti. Kuna mahakama za wilaya, na madiwani ni legislative arm ya wilaya. Miji na majiji nayo yana serikali zao. Kwa hivyo basi, hili swali la serikali moja, mbili au tatu labda linahusu serikali kuu moja mbili au tatu.

Nchi moja haiwezi kuwa na serikali kuu tatu zinazolingana. Tume ya Warioba haijapendekeza serikali kuu tatu zenye madaraka sawa.

Kiuchumi, tatizo sio wingi wa serikali bali ni ukubwa wa serikali. Kwa sasa tuna serikali kuu mbili, lakini gharama yake ni kubwa sana. Serikali ya Muungano peke yake ina zaidi ya mawaziri 60!

Muundo tulio nao sasa wa nchi moja yenye serikali kuu mbili sio mzuri. Matatizo yake tumeyaona. Mwalimu alijaribu kupunguza hayo matatizo kwa kuwa na chama tawala kimoja kinachoongoza serikali zote, lakini haikotosha. Matatizo yaliendelea hata kikafika kile kipindi akatumia nguvu dhidi ya Rais wa Zanzibar (Jumbe).

Stability inataka tuwe nchi moja, yenye serikali kuu moja ya JMT, na serikali za Zanzibar na Tanganyika. Wakuu wa serikali za Zanzibar na Tanganyika wakiitwa Magavana (kama inavyopendekeza Tume) au majina mengine si hoja. Cha msingi ni kwamba wote hao wataapa kuilinda Katiba ya JMT (pamoja na katiba za serikali zao).

Muundo wa serikali za Tanganyika na Zanzibar na ya serikali ya muungano utatakiwa uwe kwenye katiba moja yenye vipengele vyote. Nilitegemea Tume ya Warioba itoe mapendekezo ya KATIBA MOJA, SERIKALI TATU. Na ndio maana Tume ina wawakilishi toka sehemu zote za muungano.

Tunachopashwa kujali sana basi sio wingi wa serikali bali wingi wa katiba zinazojitegemea.
 
Wanasiasa wetu wanatudanganya ili waweze kututawala sisi maskini.Mungu katujalia akili ya kutambua mema na mabaya kwaio inabid tuwe makin tunapowasikiliza hawa mafisad.Warioba japo ya kusifiwa kwamba ana busara bado siwez kumuamin maana amesahau maskin wa taifa hili na kuanza kutetea matajir wenzake.
 
Wanasiasa wetu wanatudanganya ili waweze kututawala sisi maskini.Mungu katujalia akili ya kutambua mema na mabaya kwaio inabid tuwe makin tunapowasikiliza hawa mafisad.Warioba japo ya kusifiwa kwamba ana busara bado siwez kumuamin maana amesahau maskin wa taifa hili na kuanza kutetea matajir wenzake.

Kwanza lazima ukubali watakuwepo watawala ambao ni wanasiasa iwe kwa hiari ama kwa kudanganywa hili halina mjadala.Pili tunatakiwa kujua gharama za uendeshaji wa serikali hizi mbili ni kiasi gani alafu tujue kutapokuwa na serikali tatu zitakuwa na muundo gani na gharama zake ni kiasi gani?Tatu je Warioba anateteaje matajiri wenzake(je huo utajiri anao?) au ni hisia tu zinazotokana na kuchoka kufikiri?Nne umesema tuwe makini tunapowasikiliza hao mafisadi wepi hao?Tano umewahi kuona mzanzibari au mpemba yeyote anayependa Muungano kama si wazanzibara tu wanaulilia?Sita je unadhani ni watanzania wangapi wanaojali kwa kufuatilia maamuzi ya kisiasa yanayoathiri maisha yao kama si kusikiliza tu watu wanaowaamini wakitoa maoni kwa niaba yao?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Kabla ya kuunga mkono hoja yako, ni lazima unifafanulie ToRs za Tume anayoiongoza pengine aliambiwa auokoe badala ya kuuvunja?

Mara ya kwaza sheria ilitoa kabisa wazi wazi muungano usiguswe mara ya pili sheria ikasema tujadili ila jinsi ya kuboresha hiyo ndo kama TOR ya warioba na wenzake
 
Nionavyo mimi hatua za kuunda serikali tatu ni njia ya kuvunja muungano kwa mlango wa amani,kama serikali mbili zina changamoto serikali tatu zitazidi hivyo hatutatui tatizo bali tunagawanyika zaid, itafika kipindi kila mtu kwao,MUNGU ATUSAIDIESANA KUONA VIZURI.
 
Warioba anazungumza kana kwamba msimamo wake na mawazo yake ndiyo sahihi na kwenda kinyume nayo ni hatari kwa taifa. Wamependekeza serikali tatu na inaonekana wamependekeza kwa sababu tu wanataka 'kuuokoa Muungano' si kwa sababu nyingine yeyote ile. Sasa hajatuambia kwanini wanataka kuuokoa Muungano? Lakini zaidi hajasema kama wananchi wengi wanataka Muungano uokolewe!

Sasa hivi inaonekana kuna kampeni ya wapenzi wa 'Serikali tatu" kulazimisha nchi nzima kufuata njia hiyo. Hii si sahihi na si kweli. Zipo njia nyingi za kuuokoa Muungano mojawapo na labda sahihi zaidi ni kuuvunja kwanza! Baada ya kuuvunja nchi mbili zikae chini na kuamua kama wanataka Muungano tena na kwa masharti gani. Lakini njia sahihi ambayo ni chini ya kuuvunja na kupendekeza kwenda serikali na nchi moja mifumo mbalimbali; ni kama ilivyo Canada, UK, China na hata Marekani. Serikali tatu siyo SULUHISHO pekee la kuukoa Muungano - kama unahitaji kuokolewa.

Kwa vile amekuwa Mwenyekiti wa Tume hii ya kusikiliza maoni Warioba anataka watu waogope kupinga misimamo ya tume hiyo na mapendekezo yake ambayo mengine yanapakana na upuuzi. Sasa wananchi wanayo haki, uwezo na sababu wa kupinga ikibidi mapendekezo yote au mapendekezo yale ambayo yanaonekana kusukumwa na ajenda zilizoshindwa.

Wanaotaka serikali tatu wana haki sawa ya kutoa maoni kama vile wale wanaotaka serikali moja; na yeye kama Mwenyekiti wa Tume kusukumiza maoni yake kwa wananchi ni kutumia nafasi yake vibaya!
Mkuu mimi naamini kuwa muungano utavunjika tu kama haujavunjika tayari.
Kumlaumu mzee Warioba ni kupoteza wakati wako bure, maana Zanzibar walipokuwa wakiratibu katiba yao hawakumuuliza mzee Warioba.
Its a fact kuwa tayari Zanzibar imejitenga , at least kwa kutengeneza katiba yao ambayo ina madhumuni ya kujitawala.
Mzee Warioba amechukua uhalisia wa hali yenyewe na vile vile maoni ya wannchi walio wengi.

Kumlaumu mzee Warioba na kutoa prescription ambayo nawewe Mzee Mwanakijiji unajua kabisa kuwa haitekelezeki ni kujidanganya na kutoutambua ukweli.

Nasema HAKUNA mtu atakayejitokeza kusema muungano umevunjika.
Ila katika wakati huu kila Taifa, Tanzanyika na Zanzibar ni wazi wamechokana, Tanganyika iechoka kumbeba Zanzibar na Zanzibar wanataka kuwa huru kujiendeleza watakavyo.

Katika misingi hiyo, it was a very wise decision kupendekeza kuwa na serikali tatu.
Ukweli unauma lakini Tangayika ikiwa na serikali yake , hakuna kuwabeba tena hao watu wa viswani na watawajibika kuchangia sawasawa kama nchi kwa shughuli za muungano.
Wasipochangia then muungano naturally dies!!!
 
Mzee Warioba nao sasa Uzee unamwelemea.
Nimesoma na kusikilza mahojiano yake na nimeridhika kuwa Kilichoandikwa kwenye Rasimu ya Katiba mpya kwa asilimia kubwa ni maoni na mtazamo wa Tume yake pamoja na kwamba wamefanya kazi nzuri lakini kuna maeneno mengi hisia zao zilitawala mtazamo walionao kama watendaji wastaafu wa Umma.

Baadhi ya maoni ya Wananchi ambayo wao kama Tume hawakuyawapenda wao wameyaweka Kapuni na kusahau kuwa kazi yao kubwa ni kuleta maoni yote kwenye Rasimu ilikukata mzizi wa vifitina, maana kura za Wananchi ndiyo itakayotuondolea manunguniko ya aina yoyote.
 
Kwanza lazima ukubali watakuwepo watawala ambao ni wanasiasa iwe kwa hiari ama kwa kudanganywa hili halina mjadala.Pili tunatakiwa kujua gharama za uendeshaji wa serikali hizi mbili ni kiasi gani alafu tujue kutapokuwa na serikali tatu zitakuwa na muundo gani na gharama zake ni kiasi gani?Tatu je Warioba anateteaje matajiri wenzake(je huo utajiri anao?) au ni hisia tu zinazotokana na kuchoka kufikiri?Nne umesema tuwe makini tunapowasikiliza hao mafisadi wepi hao?Tano umewahi kuona mzanzibari au mpemba yeyote anayependa Muungano kama si wazanzibara tu wanaulilia?Sita je unadhani ni watanzania wangapi wanaojali kwa kufuatilia maamuzi ya kisiasa yanayoathiri maisha yao kama si kusikiliza tu watu wanaowaamini wakitoa maoni kwa niaba yao?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
haya ndio matatizo ya kuwa na wanasiasa wengi kuliko wasomi
 
mambo ya muungano haya. Mwisho wa siku tutaungana na mapepo bure. Ktk makosa ambayo Mwalimu alifanya ni kutuunganisha Tanganyika na Zanzibar.
 
Mzee Warioba nao sasa Uzee unamwelemea.
Nimesoma na kusikilza mahojiano yake na nimeridhika kuwa Kilichoandikwa kwenye Rasimu ya Katiba mpya kwa asilimia kubwa ni maoni na mtazamo wa Tume yake pamoja na kwamba wamefanya kazi nzuri lakini kuna maeneno mengi hisia zao zilitawala mtazamo walionao kama watendaji wastaafu wa Umma.

Baadhi ya maoni ya Wananchi ambayo wao kama Tume hawakuyawapenda wao wameyaweka Kapuni na kusahau kuwa kazi yao kubwa ni kuleta maoni yote kwenye Rasimu ilikukata mzizi wa vifitina, maana kura za Wananchi ndiyo itakayotuondolea manunguniko ya aina yoyote.
Haya haya haya haya, mimi nilihudhuria mikutano mingi ya kutoa maoni ya kupata katiba, Watu waliotoa maoni ya kutaka Tanganyika irudi. Mimim kama mzaliwa wa Tanganyika natamani kuona Tanganyika inarudi katikas enzi yake. Haya maoni ya kumshambula Warioba kuwa kaja na hoja yake binafsi, huku sasa ni kufirisika.

Tume imezingatia maoni ya wananchi, suala Tanganyika najua kuna watu linawaumiza sana, kwa sababu wakula huku Tanganyika, wanacheulia Zenj, Kama ni suala la kuwa uwepo wa Tanganyika unaweza sababisha union ikafa, be it.
Tanganyika yetu irudi. Kama ni suala la serikali moja Tanganyika hakuna shida. Wazenj hawataki hilo. Acha Tanganyika irudi. Tutoe maoni kuhakikisha Tanganyika inarudi ulingoni kama zamani
 
Kabla ya kuunga mkono hoja yako, ni lazima unifafanulie ToRs za Tume anayoiongoza pengine aliambiwa auokoe badala ya kuuvunja?

kuna kitu mmesahau ndugu zangu, na mlichosahau katika maoni ya katiba hakukurusiwa kujadili kuvunja muungano bali waliruhusiwa kuboresha muungano ivo bac wengne walisema serikali 3 na wengine mbili na wengne 1 na katika 3 wengne kwa huku znz waltaka pemba iwe na yake unguja(znz) iwe na yake na tanganyika, wengne wakataka kama ilivyotangazwa na warioba, kwa vile wao serikali wamesikiliza maoni ya wengi bac wakaweka serikali 3 na si maoni ya warioba jaman tukumbuke hilo, warioba kawawekeeni mpira nanyi mcheze kama hamtaki serikali 3 bac semeni hatutaki tunataka 1 au kila mtu kwao yote yanawezekana au hatutaki zote tunataka Tanganyika pia itawezekana,lakin mwenzenu neno Tanganyika linanishinda kutamka
 
Mzee Mwanakijiji, nakupinga kwa 100%. Jaji Warioba amezunguka nchi nzima kukusanya maoni ya watanzania, hayo ndiyo aliyo yakusanya na kuyafanyia majumuisho kayarudisha kwetu wananchi ili tuone kilichokusanywa nchi nzima. Warioba HATISHI MTU ila WEWE NDIO UNATAKA KUMTISHA WARIOBA. Kama wewe M.M ulitoa maoni yako unataka serikali moja basi wengi wamesema Tatu! Acheni kuitisha tume, Warioba endelea na mchakato, watu watoe maoni ya KUIBORESHA siyo kuanza kuleta maoni binafsi hatutafika.
 
Mzee mwanakijiji naunga mkono mapendekezo yako 100% baada ya kuondoa sehemu inayomlaumu J Waryoba kwa sababu:
1. Rasimu imetokana na mapendekezo ya wananchi kama yalivyokusanywa na kuratibiwa na wajumbe tuliompa afanye nao kazi kwa uwakilishi wa kuhakikisha tunapata rasimu ya ukweli pia. Hapa tusimlaumu Waryoba tu bali na kamati yake kama unafikiri wameratibu vibaya kuwa wengi walitaka serikali moja kamati imekuja na tatu au wewe ni nani kukosoa maoni ya wananchi wengi?

2. Tunajua na Waryoba amesema hadidu za rejea hazikuruhusu kamati yake kuvunja Muungano.

Kwahiyo, J Waryoba hatishi watanzania bali ni wewe unayetaka kutisha watanzania.
 
Hapo kwenye red mkuu chabuso mimi nakupinga. Si kweli kwamba hamna asiyetaka muungano, mimi binafsi siupendi na siutaki, hususan huu wa Tanganyika na Zanzibar. Siupendi kwa sababu kadhaa:-
1. Sijui faida zake zaidi ya matusi yanayotoka kwa Wazaznibari kwamba sisi tunawang'ang'ania
2. Hakuna nachokiona na kukiita manufaa kwa kuungana kwetu kijamii kwani matatizo ya kiitikadi yanaonekana wazi
3. Matusi na chuki kati ya Zanzibar na Tanganyika yanaletwa na huu muungano

Kama ukinisaidia kuelewa manufaa ya huu MUUNGANO na MWENGE WA UHURU. Otherwise kwangu nitaendelea kuuona kuwa ni kero kwangu binafsi.

Nakubaliana na wewe lakini hayo ni mawazo yako binafsi,Mimi Binafsi naona huu mungano umeleta chuki baina ya watanganyika na wazanzibar,vijana wasasa wanafikiri kuwa kulikuwa hakuna mungano wa watu kati ya zanzibar na tanganyika kabla ya muungano, lakini kwa kweli watu walikuwa wanauhusiano mzuri walikuwa wakitembelana kulikuwa na wazanzibari wanoishi tanganyika na watanganyika wanaoishi zanzibar kabla ya huu mungano wa Nyerere na Karume
 
Mzee Warioba nao sasa Uzee unamwelemea.
Nimesoma na kusikilza mahojiano yake na nimeridhika kuwa Kilichoandikwa kwenye Rasimu ya Katiba mpya kwa asilimia kubwa ni maoni na mtazamo wa Tume yake pamoja na kwamba wamefanya kazi nzuri lakini kuna maeneno mengi hisia zao zilitawala mtazamo walionao kama watendaji wastaafu wa Umma.

Baadhi ya maoni ya Wananchi ambayo wao kama Tume hawakuyawapenda wao wameyaweka Kapuni na kusahau kuwa kazi yao kubwa ni kuleta maoni yote kwenye Rasimu ilikukata mzizi wa vifitina, maana kura za Wananchi ndiyo itakayotuondolea manunguniko ya aina yoyote.

Nitangulize heshima, lakini mkuu hilo la kuweka maoni yote kwenye Rasimu huoni limepitiliza viwango vyote vya sanity? yaani una maana viwepo vipengele kwenye rasimu vinavyotimiza matakwa ya kila mtoa maoni ya katiba, Nina wasiwasi kama tutapata gari lenye ukubwa wa kutosha kubeba print document ya hiyo Rasimu:glasses-nerdy:
 
mambo ya muungano haya. Mwisho wa siku tutaungana na mapepo bure. Ktk makosa ambayo Mwalimu alifanya ni kutuunganisha Tanganyika na Zanzibar.
Halafu akafa analitetea hilo kosa. Yani mpaka kesho sielewi kwa nini Nyerere alituunganisha na kakisiwa, alituuza, ili tu apate umaarufu wa kuwa "African Statesman," kuitwa muunganisha Waafrika.

Muungano unatutesa vichwa mno, and the most insidious of all ni hili swala la distraction, Muungano unatutoa kwenye focus ya mambo mengine. Warioba amefunguka akasema the most painfull headache waliokuwa nayo kwenye kuandika Katiba ni suala la Muungano. Hebu imagine, matatizo yooooote haya tuliyonayo ya kikatiba, kiutawala, kiuchumi, kidemokrasia, kijamii, wao wameona wa focus kwenye Muungano, ambao far from solving the problems ndio kwanza wameunda kero mpya za muungano.

Tulitegemea wakati huu tutakuwa tunazungumzia mapungufu ya rasimu kwenye mambo ya kulinda ardhi yetu, madini yetu, kujenga misingi ya haki dhidi ya police brutality, kuunda institution za kushitaki mafisadi (TAKUKURU wanasema hawana mamlaka ya kushtaki mtu), kuelezea utaratibu wa raia kuandamana bila kupigwa mabomu, kusimika misingi ya kutenganisha kanisa, msikiti na serikali, kudhibiti ukubwa wa serikali na bunge na matumizi ya hela ya umma, jinsi ya kuingia mikataba bila kutuuza, kuipa nguvu Mahakama Kuu kutangua sheria zinazovunga katiba, haya yoooooooote yamesahaulika kwenye rasimu, na kwenye national conversation ya rasimu haya yako crowded out na mjadala wa Muungano, tumeganda tunaongelea li Muungano ambalo hakuna hata kiumbe kimoja nchini kinaweza kukwambia faida yake.

Sasa Muungano unatuchanganya kiasi kwamba tumeandika vituko kwenye rasimu. Warioba na wenzake wameandika kwenye rasimu kwamba kila serikali itakuwa na territory yake ya utawala na Katiba yake, na hakuna kuingiliana na wakataja kipi ni kipi na kipi cha nani cha kufanya, halafu wakasema kuanzia leo "kila mtoto ana haki ya kucheza" na "kila mtoto ana haki ya kupata elimu" na "Serikali ya Muungano itahakikisha kila mtoto anapata elimu."

Well, elimu ni reserved powers, sio suala la Muungano tena ("NECTA inawafelisha watoto wa Kizanzibar"), wala michezo ya watoto sio suala la Muungano. Sasa Jamhuri kwa nini iziingilie serikali shiriki kuhakikisha watoto wanasoma na wanacheza? Havieleweki. Kituko. Register that as kero mpya ya Muungano!
 
Nitangulize heshima, lakini mkuu hilo la kuweka maoni yote kwenye Rasimu huoni limepitiliza viwango vyote vya sanity? yaani una maana viwepo vipengele kwenye rasimu vinavyotimiza matakwa ya kila mtoa maoni ya katiba, Nina wasiwasi kama tutapata gari lenye ukubwa wa kutosha kubeba print document ya hiyo Rasimu:glasses-nerdy:

Hiyo si hoja na ndiyo maana wanatumia pesa za walipa Kodi!
Chukua mfano mdogo tu! Kwanini hawajapendekeza Serikali ya majimbo kama kweli walikuwa wanachukua maoni ya wananchi maana naamini washabiki na wanachama wengi wa Chadema wangependa kuona pendekezo hili.

Tambua Katiba ni Kanuni ya Maisha inayotakiwa kukubalika kwa wengi (Binadamu)ambapo wengi huiamini,kuisimamia na kuitekeleza bila shuruti katika maisha yao ya kila siku kijamii ,kisiasa na Kiuchumi, nje ya hapo hiyo ni Katiba ya genge la Watawala -take it or leave it!
 
Haya haya haya haya, mimi nilihudhuria mikutano mingi ya kutoa maoni ya kupata katiba, Watu waliotoa maoni ya kutaka Tanganyika irudi. Mimim kama mzaliwa wa Tanganyika natamani kuona Tanganyika inarudi katikas enzi yake. Haya maoni ya kumshambula Warioba kuwa kaja na hoja yake binafsi, huku sasa ni kufirisika.

Tume imezingatia maoni ya wananchi, suala Tanganyika najua kuna watu linawaumiza sana, kwa sababu wakula huku Tanganyika, wanacheulia Zenj, Kama ni suala la kuwa uwepo wa Tanganyika unaweza sababisha union ikafa, be it.
Tanganyika yetu irudi. Kama ni suala la serikali moja Tanganyika hakuna shida. Wazenj hawataki hilo. Acha Tanganyika irudi. Tutoe maoni kuhakikisha Tanganyika inarudi ulingoni kama zamani

Mkuu hoja hapa sikumshabulia J Warioba ila kuweka rekodi sawa.Jiulize wewe na nduguyo ni wangapi mnaungu hoja yakuiona Tanganyika ikimea tena? Hapo utagundua ninachozungumzia kwamba J.Warioba na Tume yake wameweka maoni yao kwenye maeneo mengi na hasa hili la Muungano.

Mfano mwingine huu hapa;Madudu kama haya kwa Dunia ya leo ni sawa na kuturudisha enzi za Chief Mangungo
na kuwapoka Wananchi Mamlaka ambayo wengi waliyatolea Damu enzi hizo za mkoloni

115. Kupitishwa kwa hoja za Serikali

(2) Serikali itawajibika kuyafanyia kazi mapendekezo ya Bunge kwa
kadri itakavyowezekana na kisha kuwasilisha tena Bungeni hoja husika
pamoja na maelezo ya utekelezaji wa maelekezo ya Bunge na endapo Bunge
litakataa kwa mara ya pili hoja kuhusu Bajeti ya Serikali, basi hoja hiyo
itahesabika kuwa imepitishwa na Bunge.

Kweli hapa kuna maoni ya wananchi au kimvuli cha wajumbe wa Tume ya Katiba?
Tuache kushabikia mambo J.Warioba na Tume yake bado naamini wananafasi ya kutupa Katiba nzuri na wataweza kufanya hivyo kama wataacha kusukumwa na hisia ,uccm na uhusika wao Serikalini ambao wengi wao wanategemea kuishi kwa Jasho la Wavuja Jasho la Watanganyika na Wazanzibar (Mafao)
 
Mkuu hoja hapa sikumshabulia J Warioba ila kuweka rekodi sawa.Jiulize wewe na nduguyo ni wangapi mnaungu hoja yakuiona Tanganyika ikimea tena? Hapo utagundua ninachozungumzia kwamba J.Warioba na Tume yake wameweka maoni yao kwenye maeneo mengi na hasa hili la Muungano.

Mfano mwingine huu hapa;Madudu kama haya kwa Dunia ya leo ni sawa na kuturudisha enzi za Chief Mangungo
na kuwapoka Wananchi Mamlaka ambayo wengi waliyatolea Damu enzi hizo za mkoloni



Kweli hapa kuna maoni ya wananchi au kimvuli cha wajumbe wa Tume ya Katiba?
Tuache kushabikia mambo J.Warioba na Tume yake bado naamini wananafasi ya kutupa Katiba nzuri na wataweza kufanya hivyo kama wataacha kusukumwa na hisia ,uccm na uhusika wao Serikalini ambao wengi wao wanategemea kuishi kwa Jasho la Wavuja Jasho la Watanganyika na Wazanzibar (Mafao)
Bado sija kifikia hicho kipengele, ulicho kielezea kama kiko hivyo kuna makosa ambayo tunayo fursa ya kurekebisha, lkn Tanganyika yetu irudi ili tuheshimiane, kuna watu wamezidi dharau, tunawasaidia halafu hawaridhiki kila siku kelele dawa yake ni kurudisha Tanganyika yetu. Hawiwezekani mtu anatumia raslimali za Tanganyika halafu anatuita sis Watanganyika eti ni wakoloni weusi > Tanganyika yetu acha irudi
 
Kwa vile amekuwa Mwenyekiti wa Tume hii ya kusikiliza maoni Warioba anataka watu waogope kupinga misimamo ya tume hiyo na mapendekezo yake ambayo mengine yanapakana na upuuzi. Sasa wananchi wanayo haki, uwezo na sababu wa kupinga ikibidi mapendekezo yote au mapendekezo yale ambayo yanaonekana kusukumwa na ajenda zilizoshindwa.

Wanaotaka serikali tatu wana haki sawa ya kutoa maoni kama vile wale wanaotaka serikali moja; na yeye kama Mwenyekiti wa Tume kusukumiza maoni yake kwa wananchi ni kutumia nafasi yake vibaya!

Na hii mbele ya safari itamletea shida.
Itakuwa jambo la busara na kutendea haki Nchi yao kama maoni ya pande zote yakawekwa kwenye rasimu na upigaji kura ya kupitisha Rasimu ndiyo uwemwamuzi wa mwisho wa maamuzi ya nini wa Tanzania wanakubaliana nacho kwa kila kipingele cha Rasimu na ushindi wa kila kipengele uwe zaidi ya 50% ya idadi ya watakaopiga kura.

Kama tutatumia utaratibu huu hapatakuwa na kuwekaweka viraka katiba ndani ya muda mfupi lakini kwa vile Watawala wanapenda kuweka mbele masilahi yao jambo kama hili ni vigumu kutokea mpaka masiha arudi.
 
Back
Top Bottom