Nyakijooga
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 506
- 806
Jaji Mstaafu Sinde Warioba amesema kwamba anamfahamu vyema aliyekuwa Makamu wa Rais, Balozi Emmanuel Nchimbi, akisema kuwa sio chawa.
Ameeleza kuwa Nchimbi amekuwa akimtembelea, ambapo hupata fursa ya kuzungumza masuala mbalimbali ya kisiasa, kichama pamoja na kiuchumi. Amesema kwamba moja ya jambo muhimu ambalo alimsisitiza Nchimbi alipomtembelea ni umuhimu wa kupata Katiba mpya na kushughulikia masuala ya rushwa .
View: https://www.youtube.com/live/ieUrniUezG0?si=UfWUqNulWAE6F8Ji
Amesema kwamba baada ya kuona taarifa alimpigia hakupokea, lakini anasema baada ya kusikia amevuliwa uanachama alimpigia lakini simu haikupokelewa wala ujumbe kujibiwa.
Hata hivyo amesema kuwa kuna taarifa kuwa amenyenganywa simu zake.
Aidha amedai kuwa kumekuwepo na madai kuwa kauli kuhusu katiba mpya ndizo zimechangaia kumtia matatani.
Warioba ameongeza kuwa kwa sasa kusema ukweli ni jambo ambalo linaleta changamoto na misukosuko.
Ameyasema hayo wakati akichangia mada kuhusu hali ya Demokrasia nchini katika jukwaa la Demokrasia ambalo limeandaliwa na wadau ikiwemo TLS, TWAWEZA , LHRC na UDASA
Sambamba na hayo Warioba amesema kwamba anasisitiza umuhimu wa katiba mpya kupatikana mapema kabla ya chaguzi zijazo ili kuepusha hali iliyojitokeza kwenye chaguzi zilizopita, amesema kama Katiba haitapatikana uenda hali itakuwa mbaya zaidi kwenye chaguzi zijazo.
Ameeleza kuwa Nchimbi amekuwa akimtembelea, ambapo hupata fursa ya kuzungumza masuala mbalimbali ya kisiasa, kichama pamoja na kiuchumi. Amesema kwamba moja ya jambo muhimu ambalo alimsisitiza Nchimbi alipomtembelea ni umuhimu wa kupata Katiba mpya na kushughulikia masuala ya rushwa .
View: https://www.youtube.com/live/ieUrniUezG0?si=UfWUqNulWAE6F8Ji
Amesema kwamba baada ya kuona taarifa alimpigia hakupokea, lakini anasema baada ya kusikia amevuliwa uanachama alimpigia lakini simu haikupokelewa wala ujumbe kujibiwa.
Hata hivyo amesema kuwa kuna taarifa kuwa amenyenganywa simu zake.
Aidha amedai kuwa kumekuwepo na madai kuwa kauli kuhusu katiba mpya ndizo zimechangaia kumtia matatani.
Warioba ameongeza kuwa kwa sasa kusema ukweli ni jambo ambalo linaleta changamoto na misukosuko.
Ameyasema hayo wakati akichangia mada kuhusu hali ya Demokrasia nchini katika jukwaa la Demokrasia ambalo limeandaliwa na wadau ikiwemo TLS, TWAWEZA , LHRC na UDASA
Sambamba na hayo Warioba amesema kwamba anasisitiza umuhimu wa katiba mpya kupatikana mapema kabla ya chaguzi zijazo ili kuepusha hali iliyojitokeza kwenye chaguzi zilizopita, amesema kama Katiba haitapatikana uenda hali itakuwa mbaya zaidi kwenye chaguzi zijazo.