Warioba: Mimi ni mwanaCCM kindakindaki

Warioba: Mimi ni mwanaCCM kindakindaki

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
26,025
Reaction score
25,432
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dr Judge Joseph Warioba amesema kwamba yeye ni mwanaCCM wa ukweli tofauti na wengine ambao wako CCM kuchumia tumbo. Alisema hayo akiwa wilayani Bunda akiongea kwenye kongamano lililoandaliwa na asasi ya Fikra Pevu. Dr Warioba alisema kwamba kuna baadhi ya wanaCCM ambao wakiona maslahi yao hayatimii hukimbilia vyama vingine na kisha kurejea tena ndani ya chama huku wakijifanya kuwa na mapenzi na chama wakati si kweli.

Chanzo: Uhuru

MAONI YANGU
Nakubaliana kabisa na maoni ya Dr Warioba. Kuna wanaCCM kama vile Wassira, Shibuda, Nsasugwanko, Bagenda, Ndobo na Makongoro Nyerere ambao waliikimbia CCM baada ya kuona maslahi yao hayatimii lakini baadaye waliamua kulamba matapishi yao na kurejea tena ndani ya CCM.

:yield:
 
....CCM chama cha maslahi bwana....hapo haunidanganyi hata chembe.
 
Hatuna mtu mwenye akili za kipuuzi ndani ya CCM kama alizonazo Warioba. Arejeshe tu kadi yetu kwa maana amekosa sifa za kuwa mwana CCM
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dr Judge Joseph Warioba amesema kwamba yeye ni mwanaCCM wa ukweli tofauti na wengine ambao wako CCM kuchumia tumbo. Alisema hayo akiwa wilayani Bunda akiongea kwenye kongamano lililoandaliwa na asasi ya Fikra Pevu. Dr Warioba alisema kwamba kuna baadhi ya wanaCCM ambao wakiona maslahi yao yapatimii hukimbilia vyama vingine na kisha kurejea tena ndani ya chama huku wakijifanya kuwa na mapenzi ya chama wakati si kweli.

Chanzo: Uhuru

MAONI YANGU
Nakubaliana kabisa na maoni ya Dr Warioba. Kuna wanaCCM kama vile Wassira, Shibuda, Nsasugwanko, Bagenda, Ndobo na Makongoro Nyerere ambao waliikimbia CCM baada ya kuona maslahi yao hayatimii lakini baadaye waliamua kulamba matapishi yao na kurejea tena ndani ya CCM.

:yield:
Ni kweli kabisa na siku hizi ndani ya CCM kusema ukweli ni kujenga uadui.
Tujitahidi kuujenga ukweli ili dhamira zetu ziwe huru.
Tukiweka matakwa yetu binafsi mbeke, hiyo ni recipe ya vurugu huko mbeleni.
 
Hizo ni gongo na SIGARA ndizo zilikuwa zinaongea siyo WARYOBA.
 
Ni kweli kabisa na siku hizi ndani ya CCM kusema ukweli ni kujenga uadui.
Tujitahidi kuujenga ukweli ili dhamira zetu ziwe huru.
Tukiweka matakwa yetu binafsi mbeke, hiyo ni recipe ya vurugu huko mbeleni.

kule CHADEMA, akina ZITTO, MKUMBO , MWIGAMBA, walisema uongo wakaitwa wasaliti? kweli nyani haoni ku.ndule
 
Hatuna mtu mwenye akili za kipuuzi ndani ya CCM kama alizonazo Warioba. Arejeshe tu kadi yetu kwa maana amekosa sifa za kuwa mwana CCM
Sifa kubwa ya kuwa mwana Ccm lazima uwe mwizi lakini Warioba aongozwi na tumbo Kama wana Ccm wengine .Warioba itendee mema nchi yako vizazi na vizazi vitakukumbuka na utakuwa umeweka historia ambayo aitafutika kamwe Big up
 
Hatuna mtu mwenye akili za kipuuzi ndani ya CCM kama alizonazo Warioba. Arejeshe tu kadi yetu kwa maana amekosa sifa za kuwa mwana CCM

Hapo kwenye bold umenifanya nifikirie ni sifa zipi alizokosa huyu mzee na nimezipata, kwa mara ya kwanza nakuunga mkono kwa kusema ukweli, Warioba sio MLA rushwa au MTOA rushwa, this is why hanafani na ccm, Thanks for the truth you have spoken today.
 
Hatuna mtu mwenye akili za kipuuzi ndani ya CCM kama alizonazo Warioba. Arejeshe tu kadi yetu kwa maana amekosa sifa za kuwa mwana CCM

Kwan mtu akiwa anatetea wananchi si ndo mpuuz!! Kumbe nyie ndo wa puuz kwa ufisad na kuiba rasilimal zote za watanzania, yaan umeiba kila kitu hd viwanda leo hii ajira hakuna, kama ni mwanamke lazima atoe hongo ya ngono ndo apate ajira, mama zk na dada zako wanajiuza kwasababu hakuna ajira, bado ww tu utajiuza sina uhakika kama unajiuza ila nawez sema umejiuza kwa kuuza utu wako.
 
Awache ukora.. kama yeye ccm damu damu mbona ameshindwa kuongoza tume na kuja na mapendekezo sawa na sera ya chama chake ya serikali mbili. Badala yake amekua boya tu na wajumbe wengine kuweza kuweka mapendekezo sawa na sera ya vyama vyao. Hawezi kusema hoja ya serkali mbili ni dhaifu. Huyu mzee amekua janga kwa ccm.
 
Hatuna mtu mwenye akili za kipuuzi ndani ya CCM kama alizonazo Warioba. Arejeshe tu kadi yetu kwa maana amekosa sifa za kuwa mwana CCM

Mkuu thibitisha waziwazi which offense au ni kitu gani ambacho mzee Warioba ame-commit kinachomwondolea sifa ya kuwa Kada na mwana-CCM,kama huwezi basi hizo zitakuwa ni porojo tu.
 
Back
Top Bottom