Warioba katika 'dakika 45' za ITV akihojiwa kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya...

Hongera mzee Sinde kwa kuendelea kusimamia na kupigania matakwa yawananchi kwa uzito ulele ulio kuwa unakutana nao wakati unakusanya maoni yetu.umeeleweka vizuri sana wabaya wako walio kutamkia maneno yasio kuwa na staha wanaumbuka mbele ya wapiga kura wao.
 
Halafu warioba alipaswa kujiweka pembeni na huo ushabiki coz kama hayo yalikua maoni ya wananchi anahangaika nini sasa? nani kamtuma awasemee? kazi yake ilikua kukusanya maoni na si kuwa mshabiki...
 
Huyu mzee anajua sana aiseee
ukweli ni kuwa warioba hakua convincing kabsa kama nilivyotarajia,ameshindwa hata kupangua hoja ya kuwa watu 17,000 waliotoa maoni ya serikali tatu wanakua vipi majority.

Anasema kero kubwa ya wanajeshi kuhusu serikali mbili ni kulazimika kufyatua mizinga kwa ma amiri jeshi wawili kama kwamba kuna uhaba wa mizinga.
Huku akisahau kuwa kwa serikali tatu wanaweza kufyatua mizinga mara tatu.
 
Kile kipande cha hotuba ya mwalimu itv kinachosema.TUNATAKA RAIS ANAYEWEZA KUISIMAMIA KATIBA NA KUILINDA ASIYEWEZA AKASIMAMIE SHAMBA LAKE KULE,mi naona kama anamsema ba riz.

Katiba ilishavunjwa tayari kwani Zanzibar sasa ni Nchi japo Mishahara,posho,Umeme Vinalipwa na Tanganyika,Wao sasa na Koloni la Tanganyika wanajilia vyao kiulaini.
 
Wana jamvi kama kweli vijana wa uvccm wana hoja na data za kupangua mawe aliyo toa jaji warioba leo itv tuna wataka watokee hadharani wamjibu mzalendo wetu jaji warioba kada wa ccm nguli na mweledi tangu enzi za mwl nyerere;waje jf watoe majibu msimamo wa serikali mbili wanaupata wapi?kwa data zipi walizo kusanya?
Kuwaita Uvmajanga waje wajibu hoja za Warioba ni sawa na kumuita mkutano wa hadhara Joseph Kone aje ajibu tuhuma zake.Hao ni wahuni ni kichaka na pango la wanyang`anyi hawana umoja wala makao rasmi unategemea watokee upande gani?
 
Halafu warioba alipaswa kujiweka pembeni na huo ushabiki coz kama hayo yalikua maoni ya wananchi anahangaika nini sasa? nani kamtuma awasemee? kazi yake ilikua kukusanya maoni na si kuwa mshabiki...


.....tulia!!!
 
Mzee anazidi kujichanganya sana sijui kama anajua anachofanya kwenye hii dunia.
 
Kasema nani?
Hayo ni mawazo yako binafsi
Sioni sababu ya kuyaheshimu kama mawazo ya wananchi.
sasa si umeweka thread tujadiri ama unataka nichangiaje?.

By the way mimi si mwananchi,mimi ni mlesotho.
 
maneno ya Jaji Warioba wamenikumbusha niaka ile ya themanini ambapo nilikuwa naishi kwa ndugu yangu kambi ya Mirambo Tabora, kila askari wa JWTZ alikuwa na shamba la kulima ili ajishughulishe baada ya kazi.
Hilo la kugawa vijiji, kata, wilaya hadi mikoa nakubaliana naye, haswa linasababishwa na uroho wa madraka pamoja na umimi, itafikia kipindi ichi itaganywa hadi mito na maziwa yawe ya watu flani.

Kupitia dk 45 ITV usiku huu, Jaji J. Warioba asema katiba mpya itaondoa kero ya nchi kuwa na maamiri jeshi wakuu 2 wanaopigiwa mizinga 21.
Asema wanaopinga serikali 3 ndiyo wasaliti wa Mwalimu Nyerere aliyeacha nchi hii ikiwa 1, Amiri Jeshi Mkuu 1, Bunge na Mahakama vyenye nguvu
Asema kauli za wabunge kuwa Jeshi litachukua nchi kama serikali 3 zitapita ni uchochezi unaolenga kuwafanya wananchi walichukie Jeshi lao.
Mods naomba sana uzi huu msiunganishe wa s2 waje wajibu haya aliyoyasema jaji warioba
 
hadi sasa nasoma utumbo wa makapi ya ccm sijaona jibu la Mkongwe Warioba zaidi ya mipasho ya akina T.OT.
 
Uvccm kuna mtu anaweza kujibu hoja za warioba jk mwenyewe ajajibu sehemu yenye watu aliowapa posho wampigie makofi hizo pumba zake anazoongea juzi kaita vitoto kamwaga pumba eti vinamshangalia sasa ataenda kwa wazeee wa dsmccm awape bahasha kama anapoint aje aoungee bila watu kumshangilia kwa viposho vyetu anavyogawa ndo mjue pumba zake
 
Hata siamini macho yangu ni wewe Ritz au naota? Hongera kwa kupona ugonjwa uitwao CCM
Mkuu hutakiwi kushangaa, ndivyo ilivyo, wanaCCM wenyewe wanataka serikali tatu, ndio maana viongozi wao wakaweka mbinu ya kupiga kura ya wazi ili kuwalazimisha wapigie serikali mbili,

Ikipigwa kura ya siri hata leo, serikali 3 zinapita kwa kishindo!!
 
Warioba anatetea maoni yake mzee karibu atapagawa eti kapika maoni mwenyewe halafu leo anayatetea sijui ataishia wapi.


Mkuu nimekaa nikijiuliza MTU aliyetumwa kukusanya maoni anapata wapi nguvu ya kutetea kile walichosema watoa maoni?

Kazi yake ilipaswa audhihirishie ulimwengu kuwa alichoweka kwenye rasimu ndicho kilisemwa na wananchi lakini kujigeuza mtetezi wa mapendekezo kinadhihirisha wazi alifanya kazi kishabiki

Kazi ya kukusanya maoni kamaliza sioni sababu na umuhimu kwake kuendekeza mabishano.
 
Back
Top Bottom