mkuu unatumia mtandao lkn hauwezi kukusaidia kupata taarifa zingine!? Ingia kwenye tovuti ya mwananchi lipo limewekwa tangu saa 1Wakuu, nimejitaidi kutafuta gazeti la MWANANCHI lakini sijalipata katika vijiwe kazaa huku Arusha.
Kwa atakae lipata tafadhali atujuze.
Ni akili za maiti tu ndio zinaweza kupinga kuwa kwa sasa viongozi wa Tanganyika wanawaogopa viongozi wa serikali ya Zanzibar kama jinsi swala anavyo muogopa Simba mwitu mwenye njaa! Waliovunja katiba ya Muungano wakanyamaziwa leo bado wanabebwa kwa mbereko za mlenda! Jk na uluteni wake aliapa kuilinda na kuitetea katiba ya JMT lakini mabadiliko ya 2010 yaliyoifanya ZnZ kuwa nchi kamili yalifanyika akiwa kajivalia zake kikoi huku kawekewa kashata za nazi na mkewe kipenzi akiwaza starehe anazopata akiwa mawingu kuelekea kwa Obama kumueleza namna Mbu wanavyo kuwa kikwazo cha maendeleo ya Wakwere.
Wewe lazima utakuwa ni mtoto wa warioba siyo bure pengine unahitaji kupepewa kabisa kwa haya mawazo yako ya hovyo.
Yeyote anayembeza nyerere atakuwa na mapungufu ya hali ya juuu sana mwalimu alijenga taifa lenye umoja kamili.
Mimi nitakuwa mtu wa mwisho kumwelewa huyu rais kwa sababu zifuatazo.
1.analalamikia idadi ya watu waliotoa maoni kuwa ni ndogo wakati tume aliunda yeye na muda na bajeti katoa yeye.
kwa hapa maswali ni haya.
.Kwa nini hakutoa mwaka mzima kama wa tume ya jaji kisanga?
.Kwa nini hakuongeza bajeti ili ikibido hata chopa zitumike?
.Yeye alichaguliwa na watanzania mil ngapi kati ya watu mil45?
2.Analalamikia mfumo wa serikali tatu na si mbili maswali hapa ni haya.
.Sio yeye alitoa hadidu za rejea?
.Kama ni yeye kwa nini yote aliyotunga juzi hakutunga wakati huo na kuyafanya hadidu za rejea?
.Kama serikali tatu ni mbaya kama alivyotuambia na kwa jinsi zanzibar ilivyovunja katiba ya jamhuri haoni ni wakati sasa wa kuwa na serikali moja?
.Je haoni kama aliyokuwa akitoa juzi ni maoni yake ambapo atakuwa amevunja sheria kwa kutoa maoni wakati kisheria muda ulishaisha?
3.Kwa mujibu wa sheria walizojiwekea jaji warioba alitakiwa kuwakilisha rasimu ya pili mbele ya bunge la katiba lakini kwa kupindisha sheria aliwakilisha rasimu mbele ya semina ya wajumbe ambao wangekuja kuwa wabunge wa bunge maalu la katiba,maswali hapa ni haya.
.Mh rais haoni kavunja sheria kwa kutoa maoni na msimamo badala ya kutimiza matakwa ya sheria yaliyomtaka kulizindua bunge>
.Rais haoni kuwa spika kakiuka sheria kwa warioba kuwakilisha rasimu kwa kitu ambacho shria yenyewe haikitambui?
.Nikienda mahakamani na kumshitaki kwa ukiukwaji mkubwa wa sheria uliofanywa na yeye atatumia hela za uma kulipa gharama za kesi au atatumia mshahara wake?
.Kwa nini hakuyatoa hayo maoni anayoona kwa busara zake ni mazuri katika tume ya warioba/au ni ushauri aliokuja kuupata mbele?
.Kwa ukiukwaji huu mkubwa wa shria uliofanya na rais ambaye tulitegemea kuwa ni mfano katika kusimamia sheria haoni ametufundisha sisi wa chini kuvunja sheria?
Mwisho namalizia kwa kumwambia atake serikali 1,2,3,4,5,6,7,8,9 ahakikishe TANG
kwa hiyo kwa akili yako ya kuazima kwa jirani unaona ni busara kwa rais kuleta mipasho wakati alikuwa na muda wa kutosha hata kupendekeza rasimu kurudiwa upya toka amekabidhiwa?Natumai una akili na wewe ni mtu mzima, ijapokuwa hata mtoto wa darasa la kwanza hawezi kuwa na hoja dhaifu kama za kwako;
Hapo kwenye Blue; Hakuna mahali Kikwete alilalamikia idadi ya watu waliotoa maoni kuwa ni ndogo, isipokuwa alihoji udogo wa namba ya watu waliozungumzia muundo wa muungano ikiwa kweli muundo uliopo unachukizwa/unanung'unikiwa na watu walio wengi kama ambavyo tume inataka kutuaminisha.
Hapo kwenye Red; Kitu kizima ni idadi ya watu waliotoa maoni na sio idadi ya watanzania wote kama ambavyo katika kura za urais kitu kizima kilikuwa ni idadi ya wapiga kura na sio idadi ya watanzania wote, kwa hiyo hoja yako haingii akilini kabisa.
Kwa hesabu za kitoto kabisa takwimu za tume hazionyeshi ukweli kuwa watanzania walio wengi wanataka muundo wa serikali 3, wanachofanya ni kugeuza uwingi kuwa uchache na uchache kuwa uwingi. Nashawishika kuwa maoni ya tume sio ya wanachi walio wengi, Rais ameliona hilo ndio maana kalisemea bila hiyana wala kificho, mkitaka kuamua vinginevyo amueni nyinyi ila yeye katimiza wajibu wake. Ni dhambi kubwa sana Tume kutumia mwamvuli wa maoni ya wananchi kupitisha maoni yao binafsi.
Wanaotetea serikali mbili haya hawayazungumzii, wamebuni slogan yao mpya ya "jeshi litachukua nchi"
kwa hiyo kwa akili yako ya kuazima kwa jirani unaona ni busara kwa rais kuleta mipasho wakati alikuwa na muda wa kutosha hata kupendekeza rasimu kurudiwa upya toka amekabidhiwa?
au na wewe ni mtu wa pwani wa kusubiri kusutana hadharani?