ndiuka
JF-Expert Member
- Dec 21, 2009
- 699
- 825
Leo asubuhi nikiwa stand ya mabasi nakata tiketi mdada mmoja wakati anapanda kwenye kagari kake akadondosha simu nikamuita ili nimweleze kilichotokea, akanisonya tena msonyo wa dharau.
Alipoondoa gari nikaiokota hiyo simu na kuondoka zangu; wala sikuizima.
Nafika town simu ile ikawa inaita nikapokea .... haya ndo yakawa maongezi yetu.
Mdada: Hallo habari yako?
Mimi : Nzuri, nani wewe?
Mdada : Mimi ndo mwenye hiyo simu
Mimi : Na mimi ndo nilokuita pale stand asubuhi leo ukanisonya
Mdada : Basi kaka nisamehe naomba unambie ulipo nije tuelewane
Mimi : Nitakwambia baadaye .. (nikakata simu)
Swali ni je nimwambie napatikana wapi au nimpotezee ili liwe fundisho kwake?
Alipoondoa gari nikaiokota hiyo simu na kuondoka zangu; wala sikuizima.
Nafika town simu ile ikawa inaita nikapokea .... haya ndo yakawa maongezi yetu.
Mdada: Hallo habari yako?
Mimi : Nzuri, nani wewe?
Mdada : Mimi ndo mwenye hiyo simu
Mimi : Na mimi ndo nilokuita pale stand asubuhi leo ukanisonya
Mdada : Basi kaka nisamehe naomba unambie ulipo nije tuelewane
Mimi : Nitakwambia baadaye .. (nikakata simu)
Swali ni je nimwambie napatikana wapi au nimpotezee ili liwe fundisho kwake?