thesym
JF-Expert Member
- Aug 15, 2012
- 3,791
- 4,679
Waraka mchafu wasambazwa
Katika hatua nyingine, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Said Issa Mohamed, amewataka Waislamu nchini kutopumbazwa na ujumbe wa simu unaosambazwa na watu ukilenga kuwachonganisha na chama hicho. Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Iringa, Issa Mohamed alisema kuna kundi la watu kwa sababu wanazozijua wenyewe wameamua kusambaza ujumbe wenye lengo la kuichafua CHADEMA, huku wakijua huo ni uchochezi wa kidini.
Ujumbe huo ambao Tanzania Daima imeuona umeandikwa; "Wapendwa katika bwana tumejipanga vyema kuchukua nchi 2015, Haleluyaa. Operesheni vua gamba vaa gwanda itasaidia kuwatia mkononi Waislam. Uingereza na Ujerumani zimeahidi kuwapa vijana wetu mafunzo ya uongozi na ya kivita, tusiache maandamano kwani yanajenga chama zaidi, mawakala wetu waliomo ndani ya CCM na CUF wanafanya kazi vyema tuliyowatuma, vyombo vya habari vimeahidi kutubeba hadi kieleweke, watangazie waumini wetu kuwa ule mpango wa KICHUNGAJI unaendelea vyema kafiri kakosea namba sambaza ujumbe huu kwa Waislamu tujipange."
Issa alisema kwa sababu ya tishio, Serikali ya CCM na wapambe wake wameogopeshwa na nguvu ya CHADEMA katika mikoa wanayopita, hivyo wameamua kubuni mbinu za kuwachonganisha na wananchi pasipo kujua hali hiyo inaliangamiza taifa.
Alivitaka vyombo vya usalama kuacha ushabiki wa kisiasa na badala yake vifuatilie hiyo meseji kwa kuwa ni sawa na uchochezi mwingine.
Kiongozi huyo aliwataka Waislamu kuzifanyia utafiti kila taarifa watazopewa ili wasije wakajuta baadae. Wakati huo huo, Mkuu wa Operesheni Sangara katika ziara ya CHADEMA maarufu kama M4C inayoendelea, Benson Kigaila amesema kitendo cha serikali kuwaomba wasimame kupisha zoezi la sensa kimekuwa na manufaa kwao kwa kuwa wameweza kufanya kazi kubwa ambayo wasingeweza kama wangeendelea na ratiba yao.
Alisema wamefika katika kata 46 za majimbo ya Iringa mjini, Mufindi Kusini na Kaskazini na kutembelea zaidi ya vijiji 200 kwa ajili ya mikutano ya ndani na kukutana na wanachama.
"Hawa polisi na CCM ni makatibu uenezi wetu wametusaidia sana katika kutuomba tusimame kazi tuliyofanya, hakika watajuta kwanini walibuni mchezo wao huo," alisema Kigaila.
Katika hatua nyingine, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Said Issa Mohamed, amewataka Waislamu nchini kutopumbazwa na ujumbe wa simu unaosambazwa na watu ukilenga kuwachonganisha na chama hicho. Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Iringa, Issa Mohamed alisema kuna kundi la watu kwa sababu wanazozijua wenyewe wameamua kusambaza ujumbe wenye lengo la kuichafua CHADEMA, huku wakijua huo ni uchochezi wa kidini.
Ujumbe huo ambao Tanzania Daima imeuona umeandikwa; "Wapendwa katika bwana tumejipanga vyema kuchukua nchi 2015, Haleluyaa. Operesheni vua gamba vaa gwanda itasaidia kuwatia mkononi Waislam. Uingereza na Ujerumani zimeahidi kuwapa vijana wetu mafunzo ya uongozi na ya kivita, tusiache maandamano kwani yanajenga chama zaidi, mawakala wetu waliomo ndani ya CCM na CUF wanafanya kazi vyema tuliyowatuma, vyombo vya habari vimeahidi kutubeba hadi kieleweke, watangazie waumini wetu kuwa ule mpango wa KICHUNGAJI unaendelea vyema kafiri kakosea namba sambaza ujumbe huu kwa Waislamu tujipange."
Issa alisema kwa sababu ya tishio, Serikali ya CCM na wapambe wake wameogopeshwa na nguvu ya CHADEMA katika mikoa wanayopita, hivyo wameamua kubuni mbinu za kuwachonganisha na wananchi pasipo kujua hali hiyo inaliangamiza taifa.
Alivitaka vyombo vya usalama kuacha ushabiki wa kisiasa na badala yake vifuatilie hiyo meseji kwa kuwa ni sawa na uchochezi mwingine.
Kiongozi huyo aliwataka Waislamu kuzifanyia utafiti kila taarifa watazopewa ili wasije wakajuta baadae. Wakati huo huo, Mkuu wa Operesheni Sangara katika ziara ya CHADEMA maarufu kama M4C inayoendelea, Benson Kigaila amesema kitendo cha serikali kuwaomba wasimame kupisha zoezi la sensa kimekuwa na manufaa kwao kwa kuwa wameweza kufanya kazi kubwa ambayo wasingeweza kama wangeendelea na ratiba yao.
Alisema wamefika katika kata 46 za majimbo ya Iringa mjini, Mufindi Kusini na Kaskazini na kutembelea zaidi ya vijiji 200 kwa ajili ya mikutano ya ndani na kukutana na wanachama.
"Hawa polisi na CCM ni makatibu uenezi wetu wametusaidia sana katika kutuomba tusimame kazi tuliyofanya, hakika watajuta kwanini walibuni mchezo wao huo," alisema Kigaila.