Waraka wasambazwa kuitafuna CCM 2010, kanisa Katoliki laukana

Wana deal na wrong audience! watanzania hawana shida na nyaraka fulana, kofia, khanga, pilau nk mambo poa
 

JK ni chaguo lako wewe na wenzio wenye mawazo yenye magengeza....na wewe unajiona ni mwenye nchi?pole sana
 
Kuibuka kwa mambo kama haya, yawe feki au siyo feki, ni ushahidi thabiti kuonyesha kuwa Kikwete hawezi kazi ya kuongoza Taifa hili.
 
Salva Rweyemamu kazi yake hiyo na huo waraka umeandaliwa na jamaa mmoja ktk ofisi ya akina salva na miongoni mwa aliyeupeleka same ni dogo mmoja hivi anaishi kigurunyembe moro.

Yawezekana nikakubaliana na namna hoja hii ilivyokaa. Lakini kama ni uongo nachelea kusema tutakuwa tumepoteza muda wetu na nguvu zetu kujadili hoja ambayo ama ilishapitwa sana na wakati au mtu tu kakurupuka nayo. Hata hivyo ninaona wazi kuwa hoja hii italeta kampasuko ambako ili kukaondoa la,zima ifanyike kazi ya wazi.

Napendekeza kanisa lijiondoe kwenye hii lawama kwa kutoa TAMKO rasmi nasi tuisute serikali ya CCM kwa kutengeneza cheap propaganda.
 
kanisa linatakiwa kuendelea kuelimisha wananchi jinsi gani wataondokana na umasikini kwa kupata watu wasio na choyo. Viongozi wa mifano na siyo Chadema au C.C.M. au udini. Nini ni haki ya Mtanzania?
 
Huo ni waraka wa CCM na si wa kanisa! CCM tu ndio wana muda wa kupandikiza chuki na majungu ili waendelee kuhodhi madaraka kifisadi na si kanisa kwani kanisa liko kuhubiri amani na umoja! JK atang'oka tu na hata akiiba kura tena mwisho wake utakuwa mbaya kama fisadi mwenzake mkapa. Hivi Mkapa anajisikiaje pale ambapo Mwinyi akipita mahali anashangiliwa na yeye akipita anazomewa!JK naye atazomewa sana kama tu bado akiwa madarakani ameanza kutupiwa mawe!
 

Kanisa Katoliki ni 'very organised institution'. Lina wasomi na wataalamu wa kila aina. Na hivyo, haliwezi kufanya kitu cha kipuuzi kama hicho. Ukiachilia mbali 'newsletters' ambazo zinaweza kuandikwa na kuchapishwa na parokia fulani kutokana na mahitaji yao au 'document' inayohusu taasisi mojawapo na maendeleo yake, nyaraka zote za Kanisa Katoliki zinaandikwa na (authorised by) maaskofu kwenda kwa Wakristo na mara zote huwa zina majina yao.

Hakuna waraka wowote wa Kanisa Katoliki ambao unasambazwa bila kuwa na majina ya waliouandika na kama waraka huu unasambazwa kwa maaskofu, mapadre na wachungaji nchi nzima, umeandikwa na nani? Note: Wachungaji si moja ya viongozi wa Kanisa Katoliki! Hapa inaonesha aliyeandika waraka huu hana uelewa wa safu ya viongozi wa Kanisa Katoliki.

Tetesi za waraka huu zilianza kusikika miezi kadhaa iliyopita na kama alivyosema mwenyekiti wa TEC, ni vyema vyombo vya dola viwakamate hao wanaousambaza ili waeleze wanautoa wapi na hapo ndipo ukweli utakapojulikana.

Sababu ni kwamba unaonekana kuwa waraka hatari na wenye lengo la kuwagawa Watanzania. Na pengine kwa vile umeonekana ukigawiwa msikitini, hao viongozi wa msikiti ndio wangeweza kusaidia vyombao vya dola kujua waliupata wapi. Binafsi, naona kuna watu wanacheza mchezo mchafu hapa ili kuleta mgawanyiko na migogoro ya kidini katika taifa letu.
 

Mbona Prof. kasema hajauona???
 
Acheni hizo fikra mgando Jee mmesahau katika uchaguzi uliyopita baadhi ya vikundi vya kiislamu vilipiga kampeni ya kutoichagua ccm na matokeo yake yalikuwaje? Mkumbuke kuna mamilioni ya watu ambao mnaweza kuwaita wajinga lakini pamoja na mimi bado tunaipenda ccm. Tatizo la nchi hii ni ubinafsi serikali haiajiri watu kutokana na muelekeo wa siasa hivyo kuna wengi ambao wapo kwenye ajira za umma ambao wanafanya mambo kifisadi hivi mnailaumu ccm???? Vinginevyo wawekwe makada katika sehemu hizo lazima mtalalamika. The only way forward ni kuwa na independent Ethic Code body yenye meno makali ili kuhakikisha kila kiongozi ambaye ana miliki mali iwe imepatikana kihalali vinginevyo kutaifisha
 
Lisemwalo lipo na kama halipo laja. Sasa CCM haifai, CUF haifai, Vp Chadema.

Inawezekana hata Chadema wana play hapo. Vipi waraka huo uonekane Mwanga wakati Dar sijasikia.

Lisemwalo Lipo. Chadema ....Vs......katoliki.
 
Wanataka kukimbia upuuzi wao, kanisa katoliki ndio limeandika huu waraka likazambaza kwa siri kuona joto linaendaje

Christian fundementalist at work! shame on them, wamezoea "Kupendelewa" hawataki justice lol

UKISIKIA KITU NA UKAKIKUBALI BILA KUFANYA UCHUNGUZI........ unaonyesha jinsi ambavyo unaendeshwa na hisia...... wenyewe wameukana halafu wewe unasema ni wa kwao.....MWAGA USHAHIDI.......

Waraka huu umeandikwa na wakatoliki kuendeleza mikakati yao kama kawaida,

MWAGA USHAHIDI........
 
Mbona Prof. kasema hajauona???
sishangai viongozi wetu kukana walichotamka a.k.a kumeza maneno yao....
1. ZENJI KUJIUNGA NA OIC WALIKANA BAADAYE WAKAKUBALI (wakalifungia gazeti la motomoto)
2. LORIONDO KUUZWA, WALIKANA BAADAYE WALIKUBALI (wakalifungia gazeti la motomoto)
3. KIKWETE MWENYEWE KAANZA KUKANA BAADHI YA MAMBO ALIYOYAAHIDI WAKATI WA KAMPENI
 

Wacha kutumwagia Pumba! Hivyo unataka tuamini kamba zako? Wapi !
Unafikiri CCM au Profesor mzima haelewi elimu duni ya uraia walio nayo wengi wa Watanzania? Wengi wa Watanzania ni wa kufuata upepo na ukija kwenye masuala ya dini ni kabisa. Kitu kikishaandikwa au kutangazwa kinakuwa ndio hicho kwa wengi wa Watanzania na hata ufanye vipi huwezi kukisawazisha. Sasa Waraka uwe kwa jina la dini ukizungumzia mafarakano ya kidini iwe CCM au Maghembe autumie? Wana uwezo gani wa kuwabadilisha Watanzania wahisi kuwa hayo yanayosemwa dhidi yao si kweli? Mbona hivi sasa wana kazi ya kujisafisha na ufisadi na wanashindwa halafu wakalianzishe hili?
Samahani ! mwenye akili yake akiacha unazi hawezi kukubali utumbo uliouandika. Bado atafutwe mchawi kwa hili na kwa mujibu wa matukio mbali mbali inawezekana ikawa huu waraka ulikuwa siri na ukavuja na si rahisi mtu kujibebesha nao sasa lakini waliozoeya kufanya hivi ndio wenye fursa nzuri ya kutowa nyaraka kama hizi.
 
Haya ndio mazingira halisi ya nchi yetu. Kwangu si jambo la kushangaza kuusikia waraka kama huo. Na nyingi nyingine zitakuja, kwani tatizo ni kutoka kwa ule waraka wa kwanza wa katoliki.

Kuwa Katoliki liliikumbatia na kutawala kupitia CCM siku za nyuma, ni maelezo yanayojieleza wazi hapa chini. Soma nukuu hii kwa makini.

"Kadhalika waraka huo unaenda mbali na kudai kuwa vyama vya CCM na CUF kwa sasa havifai kwa kanisa kwa kuwa vimekuwa mithili ya mbwa mwitu aliyejivika ngozi ya kondoo, huku ukitahadhariha kuwa Mahakama ya Kadhi na OIC ni hatari kwa Ukristo."


Kama hivi leo havifai, ni lini vilifaa na kwanini?
Hebu angalia mapendekezo ya chama mbadala katika nukuu hapa chini. (Kwa bahati mbaya sijasikia tamko lolote lile juu ya kauli hii toka kwa viongozi wa CHADEMA) lAKINI HASA NI NINI MAANA YAKE?

"Mwelekeo wa kanisa kwa sasa ni kuelekeza nguvu zetu kwa wakristo wote Tanzania kwa chama chetu cha CHADEMA katika uchaguzi ujao ili maslahi ya kanisa yarudi kama zamani,” unadai waraka huo."

Je wewe mwananchi unakubaliana na hilo. Kuwa CHADEMA inamvuto wa kikatoliki si siri.Na ushahidi kamili unajitokeza pale ambapo CHADEMA ina ushirikiano wa moja kwa moja na chama cha CHRISTIAN DEMOCRATIC PARTY (CDU) cha ujerumani. Si hivyo tu bali hata msaada mkubwa wapesa za kampeni huchangiwa toka katika shirikishi la kanisa katoliki la ujerumani na matajiri wa kijerumani wenye mgusu na msimamo mkali wa kikatoliki.

Ni kweli watanzania tunahitaji kukikabidhi madaraka chama chenye maadili ya aina hiyo. Yote tisa lakini ni muhimu tujifunze toka kwa jirani zetu Rwanda, Burundi na hata Kongo.

Mpaka hatujapata vyama mbadala kwa CCM, NI VYEMA KUBAKI NA ZIMWI LIKUJUALO.
 


Mawazo mfu
 

Sipendi mengi ya CCM lakini sipendi pia kuwa mnafiki. Siamini kuwa CCM wana haja ya kupandikiza jungu kama hili kwao wao itakuwa ni very cheap.

Tuwe wakweli na kuangalia tangu lini CCM wakakimbia kivuli chao badala ya kutetea matendo yao hata yawe mabaya? Tangu lini CCM wamewakataa wanaotajwa kwa ufisadi badala yake ndio wanawatetea.
Yanayoelezwa kwenye Waraka ni mambo ambayo CCM imekuwa ikishutumiwa nayo na wao wamekuwa mbele kuyatetea sasa wakurupuke na kujivika nayo kwa lengo gani?
Tunajidanganya tukifikiri kuwa CCM wanateteruka na vijineno vyetu humu JF, wao wanaamini kuwa wananchi wako nyuma yao. Naomba tujuulize hao tunaowaita wapiganaji wako wapi? Ni CCM na hao mafisadi wako wapi ? ni CCM kwa hivyo kwao wao ni moja baya au zuri linakaribishwa CCM.
Waraka huu bado una harufu ya Kanisa au kikundi fulani ndani ya Kanisa, suwala ni kuwa jee Kanisa kama Kanisa lina msimamo gani na waraka huo? Na iwapo linajivuwa na waraka huo basi tamko la kulaani yaliyoandikwa kwenye waraka huo ndio itakuwa kujinasua lakini kuanza kutafut mchawi bila ya kupinga lililotamkwa hakusaidii.
 


Unataka watamke na kuukataa mara ngapi ? Wao wamesema waraka wao wa mwanzo umesimama na ndiyo waraka pekee . Mbona hamuuleti hapa tuanmgalie kuanzia majina na sahihi ? Maana ukiwa hapa kila kitu kitaonekana waandishe waweke ngoma hapa badala ya kuandika habri tupu . Kanisa Katoliki hawawezi kukimbia maandiko yao hawana uoga huo. Kama huamini ngojea rungu la Pengo maana amekaa anautafuta ukweli then utamsikia
 
Lisemwalo lipo na kama halipo laja. Sasa CCM haifai, CUF haifai, Vp Chadema.

Inawezekana hata Chadema wana play hapo. Vipi waraka huo uonekane Mwanga wakati Dar sijasikia.

Lisemwalo Lipo. Chadema ....Vs......katoliki.

Kama hujasikia ni tatizo lako mwenyewe. Tetesi za waraka huu kuwepo zilianza kusikika mara tu baada ya kusambaa kwa Waraka wa Katoliki mwezi wa 7 au 8. Hata kiongozi fulani wa kisiasa aliwahi kusema anajua hata jina la msikiti unaousambaza na akasema akihitajika kuutaja atautaja.
 

Lugha ya huo waraka ina 'harufu' ya wafitini wa Kanisa Katoliki. Sijawahi kuona Kanisa Katoliki likiandika waraka unaosambazwa kwa maaksofu, mapadre na wachungaji na usio na jina la mwandishi wala publisher. Ni lini Kanisa Katoliki likawa na wachungaji? Ni akina nani hawa? Na mwandishi ni nani: maaskofu, mapadre au wachungaji?

Ila tukinusanusa tutakuja kugundua kwamba walioutunga ni wale wanaousambaza pia!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…