Civil Engineer tz
Senior Member
- Dec 17, 2017
- 103
- 82
WARAKA WA PASAKA KUTOKA KWA MHANDISI UJENZI MZALENDO
Nawasalimu wote,
Ndugu wa-Tanzania, kumekuwa na nyaraka mbalimbali zinazotolewa kwa serikali msimu huu wa Pasaka, nami nimeona vyema nitoe waraka huu kwa ajili ya kukumbushana.
Tupo duniani na hakuna atakayeweza kuturidhisha taifa lote katika uongozi wake. Sio Askofu au Mchungaji au Mufti au kiongozi yoyote wa dini au malaika au Yesu, wala sio wewe wala si mimi wala si shetani Hakuna yeyote ambaye akiwa Rais atapendwa na kila mtu au kila taifa jirani.
Hivyo nadhubutu kusema kuwa, kumsema vibaya kiongozi au kumtukana hakusaidii lolote bali kunaleta uvunjifu wa amani. Ni vyema kumwombea kwa Mungu azidi kumpa hekima na kuiombea nchi amani na kutoa ushauri unao-uonna upo sahihi akiutendea kazi sawa akiutupa sawa.
Mtu anayeefaa kuwa kiongozi ni nani?
Ni yule anayeona m/wenzake a/wanaenda kinyume nae, akachukua hatua ya kumshauri na kumwaombea mema bila ya kumtukana wala kumsema vibaya kwa watu, akiwa CCM au CHADEMA au POPOTE ni sawa.
Watu wanamna hiyo ni wachache sana hata katika bibilia, baadhi yao ni ;
01. Tunamsoma Ayubu. Huyu Mungu alimruhusu shetani kumtendea mabaya ila yeye hakumkufuru Mungu.
02. Tunamsoma Yesu. Huyu aliteswa na wanadamu ila aliwaombea mema wasipigwe na Mungu kwani hawajui walitendalo.
03. Tunamsoma Stefano. Huyu alipigwa mawe hadi kufa ila hakuwalaani waliompiga.
04. Na wengine uliowahi kuwasoma ambao walitendewa mabaya ila hawakulipa mabaya.
Nyakati hizi imekuwa rahisi kumwona mwanachama-MPINZANI anamwacha mumeo eti kisa mumewe kahamia ChamaTAWALA huku akitaka wa-Tanzania tumwone yeye ndio kiongozi mzuri.KUSEMA KWELI HUYO MWANAMAMA HATOFAA KUWA KIONGOZI BORA.
Nyakati hizi imekuwa rahisi kumwona mwanachama-MPINZANI anamsema vibaya au kumtusi mh Rais, huku akitaka kuonekana kuwa yeye atakuwa kiongozi bora akichaguliwa.KUSEMA KWELI HUYO HATOFAA KUWA KIONGOZI BORA
Nyakati hizi imekuwa rahisi kumwona mwanachama-TAWALA akiwatusi au kuwasema vibaya wapinzani, huku akitaka kuonekana yeye ni kiongozi bora akichaguliwa.KUSEMA KWELI HUYO HATOFAA KUWA KIONGOZI BORA.
Maoni yangu kwa wa-Tanzania wenzangu:
Kiongozi si UCHAMA, Kiongozi ni HEKIMA. Wa-Tanzania tushamchagua Mh Rais John Pombe Magufuli kuwa Kiongozi wa Wa-Tanzania.
Kilicho chema kwetu ni kumwombea kwa Mungu azidi kumpa hekima na kupendekeza/ kushauri yaliomema kwake. Kumsema vibaya na kumtusi hakusaidii lolote bali kunapelekea uvunjifu wa amani.
Kumbuka hata kama ni nani angekuwa kiongozi, sio watu wote wangeona mazuri yake, maana kuna watu wengine wanamchukia mtu tu- kwa ongea yake, wengine kwa sura yake, wengine kwa tembea yake. WANADAMU HATA MUNGU ALIYEWAUMBA WANAMPINGA SEMBUSE MTU MWENZAO.
RAIS JPM CHAPA KAZI USHAAMINIWA NA WENGI WEWE CHAPA KAZI, BINADAMU WENYE ROHO NJEMA HUWA WANAKUMBUKA MEMA YA MTU WAKATI AMEKUFA, NA WENYE ROHO MBAYA HUFURAHIA KIFO CHA MTU BALI WENYE HEKIMA WATAZIDI KUKUOMBEA KWA MUNGU AKUONGEZEE HEKIMA NA KUKUEPUSHA NA MABAYA YOTE.
Nawasalimu wote,
Ndugu wa-Tanzania, kumekuwa na nyaraka mbalimbali zinazotolewa kwa serikali msimu huu wa Pasaka, nami nimeona vyema nitoe waraka huu kwa ajili ya kukumbushana.
Tupo duniani na hakuna atakayeweza kuturidhisha taifa lote katika uongozi wake. Sio Askofu au Mchungaji au Mufti au kiongozi yoyote wa dini au malaika au Yesu, wala sio wewe wala si mimi wala si shetani Hakuna yeyote ambaye akiwa Rais atapendwa na kila mtu au kila taifa jirani.
Hivyo nadhubutu kusema kuwa, kumsema vibaya kiongozi au kumtukana hakusaidii lolote bali kunaleta uvunjifu wa amani. Ni vyema kumwombea kwa Mungu azidi kumpa hekima na kuiombea nchi amani na kutoa ushauri unao-uonna upo sahihi akiutendea kazi sawa akiutupa sawa.
Mtu anayeefaa kuwa kiongozi ni nani?
Ni yule anayeona m/wenzake a/wanaenda kinyume nae, akachukua hatua ya kumshauri na kumwaombea mema bila ya kumtukana wala kumsema vibaya kwa watu, akiwa CCM au CHADEMA au POPOTE ni sawa.
Watu wanamna hiyo ni wachache sana hata katika bibilia, baadhi yao ni ;
01. Tunamsoma Ayubu. Huyu Mungu alimruhusu shetani kumtendea mabaya ila yeye hakumkufuru Mungu.
02. Tunamsoma Yesu. Huyu aliteswa na wanadamu ila aliwaombea mema wasipigwe na Mungu kwani hawajui walitendalo.
03. Tunamsoma Stefano. Huyu alipigwa mawe hadi kufa ila hakuwalaani waliompiga.
04. Na wengine uliowahi kuwasoma ambao walitendewa mabaya ila hawakulipa mabaya.
Nyakati hizi imekuwa rahisi kumwona mwanachama-MPINZANI anamwacha mumeo eti kisa mumewe kahamia ChamaTAWALA huku akitaka wa-Tanzania tumwone yeye ndio kiongozi mzuri.KUSEMA KWELI HUYO MWANAMAMA HATOFAA KUWA KIONGOZI BORA.
Nyakati hizi imekuwa rahisi kumwona mwanachama-MPINZANI anamsema vibaya au kumtusi mh Rais, huku akitaka kuonekana kuwa yeye atakuwa kiongozi bora akichaguliwa.KUSEMA KWELI HUYO HATOFAA KUWA KIONGOZI BORA
Nyakati hizi imekuwa rahisi kumwona mwanachama-TAWALA akiwatusi au kuwasema vibaya wapinzani, huku akitaka kuonekana yeye ni kiongozi bora akichaguliwa.KUSEMA KWELI HUYO HATOFAA KUWA KIONGOZI BORA.
Maoni yangu kwa wa-Tanzania wenzangu:
Kiongozi si UCHAMA, Kiongozi ni HEKIMA. Wa-Tanzania tushamchagua Mh Rais John Pombe Magufuli kuwa Kiongozi wa Wa-Tanzania.
Kilicho chema kwetu ni kumwombea kwa Mungu azidi kumpa hekima na kupendekeza/ kushauri yaliomema kwake. Kumsema vibaya na kumtusi hakusaidii lolote bali kunapelekea uvunjifu wa amani.
Kumbuka hata kama ni nani angekuwa kiongozi, sio watu wote wangeona mazuri yake, maana kuna watu wengine wanamchukia mtu tu- kwa ongea yake, wengine kwa sura yake, wengine kwa tembea yake. WANADAMU HATA MUNGU ALIYEWAUMBA WANAMPINGA SEMBUSE MTU MWENZAO.
RAIS JPM CHAPA KAZI USHAAMINIWA NA WENGI WEWE CHAPA KAZI, BINADAMU WENYE ROHO NJEMA HUWA WANAKUMBUKA MEMA YA MTU WAKATI AMEKUFA, NA WENYE ROHO MBAYA HUFURAHIA KIFO CHA MTU BALI WENYE HEKIMA WATAZIDI KUKUOMBEA KWA MUNGU AKUONGEZEE HEKIMA NA KUKUEPUSHA NA MABAYA YOTE.