KingPower
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 1,099
- 1,747
Nimefurahishwa Sana na kusikia rais wetu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dr Samia Suluhu Hassan ni mtembeleaji mzuri wa jukwaa hili la JamiiForums na tunaamini atatusikia juu ya hiki kilio chetu.
Sisi Wahandisi tulioajiriwa kama walimu katika shule za ufundi Tanzania.
Bwiru Boys Secondary School
Mwadui Secondary School
Moshi Tech Secondary School
Mtwara Tech Secondary School
Tanga Tech Secondary School
Iyunga Tech Secondary School
Ifunda Tech Secondary School
Musoma Tech Secondary School
Chato Tech Secondary School
Tuliajiriwa December 2020, tunaenda Mwaka wa 3 huu kazini hatujathibitishwa, wala kupewa barua za ajira na hivyo kukosa baadhi ya stahiki za kiutumishi.
Swala letu tumelipeleka Kwa Wakurugenzi, Ma RAS mpaka katibu mkuu Tamisemi lakini hakuna majibu yeyote. Wakurugenzi na TSC wanasema hawawezi kututhibitisha kazini kwakuwa hatuna sifa za ualimu, hadi tukasomee post graduate diploma in education.
Kwenye shule za ufundi kuna watu mfano kama laboratory technician wameajiriwa na wapo chini ya Mkurugenzi, na wamethibishwa kazini na sio walimu inakuaje Kwa Wahandisi (Engineers) ambapo Tangazo la ajira la September 7 2020 kipengele cha IV, hakikusema kwamba tukiajiriwa twende tukasome?
Lakini huku kweny halmashauri wanatudai twende tukasome tena Kwa gharama zako. Huu ni utaratibu wa wapi? Tumejaribu kuandika barua Kwa katibu Mkuu Tamisemi tena sio moja lakini hakuna hata moja iliyojibiwa zaidi tu ya kusikia Kwa maafisa utumishi wakisema Tamisemi kuna utaratibu maalumu wanaouandaa, mwaka wa pili huu bila kuona chochote.
Huku wale walimu tulioajiriwa nao, wakithibitishwa kazini na kutuzidi Kwa maana ya seniority. Tumekuwa tukipitia vipindi vigumu vya manyanyaso, msongo wa mawazo na kukosa Hali au morali ya kazi. Tunafanya majukumu ya kiualimu kama kushika zamu, kuandaa lesson plan ect bila ya mkataba wa ajira unaokuonesha majukumu ya kazi yako, au kujua kazi yako ni temporary au permanent.
Ni heri ingewekwa wazi kama ajira zetu ni za mkataba Kwa maana ya temporary na wangespecify duration, ingetusaidia sana, Kwa maana Wakurugenzi wamekuwa hawapitishi barua za transfer ukipata sehemu nyingine wala hawapitishi barua za maombi ya kazi za utumishi ili twende kwenye Kada zetu tulizozisomea Kwa maana huku tulipo hawatutambui.
Ikikupendeza Mheshimiwa Rais tunakuomba Sana utusaidie kupata haki zetu Kwa maana ya kuthibitishwa kazini na kupatiwa barua ya ajira ili tuweze kufanya kazi Kwa Amani kwenye mioyo yeti na kuongeza weledi wa kazi.
Kwani ni haki ya mtumishi akimaliza probation period ya mwaka mmoja kuthibitishwa kazini na kupewa barua ya ajira.
Naomba
Kuwasilisha
Sisi Wahandisi tulioajiriwa kama walimu katika shule za ufundi Tanzania.
Bwiru Boys Secondary School
Mwadui Secondary School
Moshi Tech Secondary School
Mtwara Tech Secondary School
Tanga Tech Secondary School
Iyunga Tech Secondary School
Ifunda Tech Secondary School
Musoma Tech Secondary School
Chato Tech Secondary School
Tuliajiriwa December 2020, tunaenda Mwaka wa 3 huu kazini hatujathibitishwa, wala kupewa barua za ajira na hivyo kukosa baadhi ya stahiki za kiutumishi.
Swala letu tumelipeleka Kwa Wakurugenzi, Ma RAS mpaka katibu mkuu Tamisemi lakini hakuna majibu yeyote. Wakurugenzi na TSC wanasema hawawezi kututhibitisha kazini kwakuwa hatuna sifa za ualimu, hadi tukasomee post graduate diploma in education.
Kwenye shule za ufundi kuna watu mfano kama laboratory technician wameajiriwa na wapo chini ya Mkurugenzi, na wamethibishwa kazini na sio walimu inakuaje Kwa Wahandisi (Engineers) ambapo Tangazo la ajira la September 7 2020 kipengele cha IV, hakikusema kwamba tukiajiriwa twende tukasome?
Lakini huku kweny halmashauri wanatudai twende tukasome tena Kwa gharama zako. Huu ni utaratibu wa wapi? Tumejaribu kuandika barua Kwa katibu Mkuu Tamisemi tena sio moja lakini hakuna hata moja iliyojibiwa zaidi tu ya kusikia Kwa maafisa utumishi wakisema Tamisemi kuna utaratibu maalumu wanaouandaa, mwaka wa pili huu bila kuona chochote.
Huku wale walimu tulioajiriwa nao, wakithibitishwa kazini na kutuzidi Kwa maana ya seniority. Tumekuwa tukipitia vipindi vigumu vya manyanyaso, msongo wa mawazo na kukosa Hali au morali ya kazi. Tunafanya majukumu ya kiualimu kama kushika zamu, kuandaa lesson plan ect bila ya mkataba wa ajira unaokuonesha majukumu ya kazi yako, au kujua kazi yako ni temporary au permanent.
Ni heri ingewekwa wazi kama ajira zetu ni za mkataba Kwa maana ya temporary na wangespecify duration, ingetusaidia sana, Kwa maana Wakurugenzi wamekuwa hawapitishi barua za transfer ukipata sehemu nyingine wala hawapitishi barua za maombi ya kazi za utumishi ili twende kwenye Kada zetu tulizozisomea Kwa maana huku tulipo hawatutambui.
Ikikupendeza Mheshimiwa Rais tunakuomba Sana utusaidie kupata haki zetu Kwa maana ya kuthibitishwa kazini na kupatiwa barua ya ajira ili tuweze kufanya kazi Kwa Amani kwenye mioyo yeti na kuongeza weledi wa kazi.
Kwani ni haki ya mtumishi akimaliza probation period ya mwaka mmoja kuthibitishwa kazini na kupewa barua ya ajira.
Naomba
Kuwasilisha