Waraka kwa Rais Samia kuhusu vilio vyetu sisi Wahandisi tulioajiriwa kama Walimu

KingPower

JF-Expert Member
Jun 8, 2015
1,099
1,747
Nimefurahishwa Sana na kusikia rais wetu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dr Samia Suluhu Hassan ni mtembeleaji mzuri wa jukwaa hili la JamiiForums na tunaamini atatusikia juu ya hiki kilio chetu.

Sisi Wahandisi tulioajiriwa kama walimu katika shule za ufundi Tanzania.

Bwiru Boys Secondary School
Mwadui Secondary School
Moshi Tech Secondary School
Mtwara Tech Secondary School
Tanga Tech Secondary School
Iyunga Tech Secondary School
Ifunda Tech Secondary School
Musoma Tech Secondary School
Chato Tech Secondary School

Tuliajiriwa December 2020, tunaenda Mwaka wa 3 huu kazini hatujathibitishwa, wala kupewa barua za ajira na hivyo kukosa baadhi ya stahiki za kiutumishi.

Swala letu tumelipeleka Kwa Wakurugenzi, Ma RAS mpaka katibu mkuu Tamisemi lakini hakuna majibu yeyote. Wakurugenzi na TSC wanasema hawawezi kututhibitisha kazini kwakuwa hatuna sifa za ualimu, hadi tukasomee post graduate diploma in education.

Kwenye shule za ufundi kuna watu mfano kama laboratory technician wameajiriwa na wapo chini ya Mkurugenzi, na wamethibishwa kazini na sio walimu inakuaje Kwa Wahandisi (Engineers) ambapo Tangazo la ajira la September 7 2020 kipengele cha IV, hakikusema kwamba tukiajiriwa twende tukasome?

Lakini huku kweny halmashauri wanatudai twende tukasome tena Kwa gharama zako. Huu ni utaratibu wa wapi? Tumejaribu kuandika barua Kwa katibu Mkuu Tamisemi tena sio moja lakini hakuna hata moja iliyojibiwa zaidi tu ya kusikia Kwa maafisa utumishi wakisema Tamisemi kuna utaratibu maalumu wanaouandaa, mwaka wa pili huu bila kuona chochote.

Huku wale walimu tulioajiriwa nao, wakithibitishwa kazini na kutuzidi Kwa maana ya seniority. Tumekuwa tukipitia vipindi vigumu vya manyanyaso, msongo wa mawazo na kukosa Hali au morali ya kazi. Tunafanya majukumu ya kiualimu kama kushika zamu, kuandaa lesson plan ect bila ya mkataba wa ajira unaokuonesha majukumu ya kazi yako, au kujua kazi yako ni temporary au permanent.

Ni heri ingewekwa wazi kama ajira zetu ni za mkataba Kwa maana ya temporary na wangespecify duration, ingetusaidia sana, Kwa maana Wakurugenzi wamekuwa hawapitishi barua za transfer ukipata sehemu nyingine wala hawapitishi barua za maombi ya kazi za utumishi ili twende kwenye Kada zetu tulizozisomea Kwa maana huku tulipo hawatutambui.

Ikikupendeza Mheshimiwa Rais tunakuomba Sana utusaidie kupata haki zetu Kwa maana ya kuthibitishwa kazini na kupatiwa barua ya ajira ili tuweze kufanya kazi Kwa Amani kwenye mioyo yeti na kuongeza weledi wa kazi.

Kwani ni haki ya mtumishi akimaliza probation period ya mwaka mmoja kuthibitishwa kazini na kupewa barua ya ajira.

Naomba
Kuwasilisha
 
Sasa mwamba shida ipo wapi, finya postgraduate hata open universty then peleka vyeti ili uthibitishwe, mimi nilisoma law nikapiga postgraduate in education nachapa kipindi hapo shule, nikiendelea na michongo mingine, tatizo la ajira ni kubwa nchi hii shikilia hapo kwanza badae utajiongeza.
 
Mkuu asante Kwa ushauri wako

Embu fikiria baadhi ya watu wameajiriwa na Diploma za Engineering lakini analipwa mshara wa TGTS C3.

Ana deni la bodi ya mikopo Kwa maana wakati anaajiriwa alikua final year ya Bachelor Degree in Engineering

Amejaribu kupeleka cheti cha Bachelor Degree in Engineering, Maafisa utumishi wanasema system haikubali hadi apeleke cheti cha ualimu Kwa maana bachelor degree in education (yaani akasome tena 3 years Kwa gharama zake)

Ana familia, amepanga nje Kwa mshahara wa around 400K

Mkuu acha tu
sasa mwamba shida ipo wapi, finya postgraduate hata open universty then peleka vyeti ili uthibitishwe , mimi nilisoma law nikapiga postgraduate in education nachapa kipindi hapo shule, nikiendelea na michongo mingine , tatizo la ajira ni kubwa nchi hii shikilia hapo kwanza badae utajiongeza
 
Pole Sana aiseh ulivyofika vyuoni ungebadil muundo wa ajira yako kuwa mhandisi na siyo mwalimu🙅au ungeajiriwa Kama tutorial assistance ingekuwa yenyewe ila ualimu mweh ngumu kumeza
Mkuu asante Kwa ushauri wako

Embu fikiria baadhi ya watu wameajiriwa na Diploma za Engineering lakini analipwa mshara wa TGTS C3,

Ana deni la bodi ya mikopo Kwa maana wakati anaajiriwa alikua final year ya Bachelor Degree in Engineering

Amejaribu kupeleka cheti cha Bachelor Degree in Engineering, Maafisa utumishi wanasema system haikubali hadi apeleke cheti cha ualimu Kwa maana bachelor degree in education (yaani akasome tena 3 years Kwa gharama zake)

ana familia, amepanga nje Kwa mshahara wa around 400K

Mkuu acha tu,
 
sasa mwamba shida ipo wapi, finya postgraduate hata open universty then peleka vyeti ili uthibitishwe , mimi nilisoma law nikapiga postgraduate in education nachapa kipindi hapo shule, nikiendelea na michongo mingine , tatizo la ajira ni kubwa nchi hii shikilia hapo kwanza badae utajiongeza
Masuala ya Utumishi hayaendi kwa utashi wa mtu, kuwa na akili na kama hujui kitu tulia, tumia muda wako kusoma comments za wanaoelewa nawe ujifunze.
Mleta Post nakushauri masuala yafuatayo:

1. Angalia Cheo chako cha muundo ulichoajiriwa, kisha tafuta muundo wa Kada yako uone utaratibu uliowekwa wa kupanda madaraja kutoka ngazi moja na nyingine.

2. Kuthibitishwa kazini (kwa mujibu wa Sheria) ni kuanzia miezi 8 hadi mwaka baada ya kuajiriwa, na pale unapoona hujapewa barua baada ya muda huo kuisha Sheria inaelekeza kwamba wewe tayari unethibitishwa by pressumption.

3. Mwajiri wako alipaswa kukupa barua ya sababu ya kutokukuthibitisha kazini baada ya mwaka kuisha, kama hajafanya hivyo ni kwamba alishakuthibitisha isipokuwa hajakupa barua.

4. Kwenda kusoma postgraduate diploma ya ualimu maana yake unataka uhame kutoka kada ya uhandisi na kuingia kada ya ualimu, ukirejea uajiriwe na uanze upya (kataeni upuuzi huo) na anayewashauri hivi ni Afisa Utumishi asiye na akili au Afisa Elimu wa magumashi.

5. Kwakuwa mna miaka 3 kazini, bado mwaka mmoja tu msitahili kupanda daraja hivyo msipofuatilia haraka mnaweza kupoteza haki zenu kwani hamtakuwa kwenye eligible list kwa ajili ya promo kwenye mfumo wa HCMIS.

6. Mwenye Mamlaka ya Miundo ya Utumishi wa Umma Nchini ni Katibu Mkuu_ Utumishi na ndiye aliyetoa kibali muajiriwe kwa Kada hiyo na kupelekwa Shuleni, ni katika sura hiyo kuwa malalamiko yenu lazima yaelekezwe kwake yakiwa na barua zenu za ajira.

7. OR TAMISEMI ni wizara tumizi, inawatumia Watumishi huku wakiwa si wasimamizi wa Miundo na Mishahara, kwahyo malalamiko yenu mliwasilisha kwa watu wasiojua kitu mathalan ukute ziliangukia idara ya Elimu iliyojaa walimu wenzenu kama mlio nao huko.

8. Poleni, zingatieni taratibu hizo. Barua zote mlizowahi kuandika kwenye mamlaka mlizotaja mzitunze kwa matumizi ya baadaye maana kwenye Utumishi jambo likikaa vibaya kila mtu huruka, ni vyema zaidi kama zilipokelewa kwa Dispatch.

Ahsanteni na karibuni shambani tulime
Mizega.
 
Nimefurahishwa Sana na kusikia rais wetu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dr Samia Suluhu Hassan ni mtembeleaji mzuri wa jukwaa hili la Jamii forum na tunaamini atatusikia juu ya hiki kilio chetu

Sisi Wahandisi tulioajiriwa kama walimu katika shule za ufundi Tanzania ,

Bwiru boys secondary school
Mwadui secondary school
Moshi tech secondary school
Mtwara tech secondary school
Tanga tech secondary school
Iyunga tech secondary school
Ifunda tech secondary school
Musoma tech secondary school
Chato tech secondary school

Tuliajiriwa December 2020,
tunaenda Mwaka wa 3 huu kazini hatujathibitishwa, wala kupewa barua za ajira na hivyo kukosa baadhi ya stahiki za kiutumishi,

Swala letu tumelipeleka Kwa Wakurugenzi, Ma RAS mpaka katibu mkuu Tamisemi lakini hakuna majibu yeyote,

Wakurugenzi na TSC wanasema hawawezi kututhibitisha kazini kwakuwa hatuna sifa za ualimu, hadi tukasomee post graduate diploma in education.

Kwenye shule za ufundi kuna watu mfano kama laboratory technician wameajiriwa na wapo chini ya Mkurugenzi, na wamethibishwa kazini na sio walimu inakuaje Kwa Wahandisi (Engineers) ambapo Tangazo la ajira la September 7 2020 kipengele cha IV, hakikusema kwamba tukiajiriwa twende tukasome?

Lakini huku kweny halmashauri wanatudai twende tukasome tena Kwa gharama zako
Huu ni utaratibu wa wapi?

Tumejaribu kuandika barua Kwa katibu Mkuu Tamisemi tena sio moja lakini hakuna hata moja iliyojibiwa zaidi tu ya kusikia Kwa maafisa utumishi wakisema Tamisemi kuna utaratibu maalumu wanaouandaa, mwaka wa pili huu bila kuona chochote

Huku wale walimu tulioajiriwa nao, wakithibitishwa kazini na kutuzidi Kwa maana ya seniority

Tumekuwa tukipitia vipindi vigumu vya manyanyaso, msongo wa mawazo na kukosa Hali au morali ya kazi

Tunafanya majukumu ya kiualimu kama kushika zamu, kuandaa lesson plan ect bila ya mkataba wa ajira unaokuonesha majukumu ya kazi yako, au kujua kazi yako ni temporary au permanent


Ni heri ingewekwa wazi kama ajira zetu ni za mkataba Kwa maana ya temporary na wangespecify duration, ingetusaidia sana, Kwa maana Wakurugenzi wamekuwa hawapitishi barua za transfer ukipata sehemu nyingine wala hawapitishi barua za maombi ya kazi za utumishi ili twende kwenye Kada zetu tulizozisomea Kwa maana huku tulipo hawatutambui


ikikupendeza Mheshimiwa Rais tunakuomba Sana utusaidie kupata haki zetu Kwa maana ya kuthibitishwa kazini na kupatiwa barua ya ajira ili tuweze kufanya kazi Kwa Amani kwenye mioyo yeti na kuongeza weledi wa kazi

Kwani ni haki ya mtumishi akimaliza probation period ya mwaka mmoja kuthibitishwa kazini na kupewa barua ya ajira,

Naomba
Kuwasilisha
Muhimu kuzingatia hayo
 
Nimefurahishwa Sana na kusikia rais wetu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dr Samia Suluhu Hassan ni mtembeleaji mzuri wa jukwaa hili la Jamii forum na tunaamini atatusikia juu ya hiki kilio chetu

Sisi Wahandisi tulioajiriwa kama walimu katika shule za ufundi Tanzania ,

Bwiru boys secondary school
Mwadui secondary school
Moshi tech secondary school
Mtwara tech secondary school
Tanga tech secondary school
Iyunga tech secondary school
Ifunda tech secondary school
Musoma tech secondary school
Chato tech secondary school

Tuliajiriwa December 2020,
tunaenda Mwaka wa 3 huu kazini hatujathibitishwa, wala kupewa barua za ajira na hivyo kukosa baadhi ya stahiki za kiutumishi,

Swala letu tumelipeleka Kwa Wakurugenzi, Ma RAS mpaka katibu mkuu Tamisemi lakini hakuna majibu yeyote,

Wakurugenzi na TSC wanasema hawawezi kututhibitisha kazini kwakuwa hatuna sifa za ualimu, hadi tukasomee post graduate diploma in education.

Kwenye shule za ufundi kuna watu mfano kama laboratory technician wameajiriwa na wapo chini ya Mkurugenzi, na wamethibishwa kazini na sio walimu inakuaje Kwa Wahandisi (Engineers) ambapo Tangazo la ajira la September 7 2020 kipengele cha IV, hakikusema kwamba tukiajiriwa twende tukasome?

Lakini huku kweny halmashauri wanatudai twende tukasome tena Kwa gharama zako
Huu ni utaratibu wa wapi?

Tumejaribu kuandika barua Kwa katibu Mkuu Tamisemi tena sio moja lakini hakuna hata moja iliyojibiwa zaidi tu ya kusikia Kwa maafisa utumishi wakisema Tamisemi kuna utaratibu maalumu wanaouandaa, mwaka wa pili huu bila kuona chochote

Huku wale walimu tulioajiriwa nao, wakithibitishwa kazini na kutuzidi Kwa maana ya seniority

Tumekuwa tukipitia vipindi vigumu vya manyanyaso, msongo wa mawazo na kukosa Hali au morali ya kazi

Tunafanya majukumu ya kiualimu kama kushika zamu, kuandaa lesson plan ect bila ya mkataba wa ajira unaokuonesha majukumu ya kazi yako, au kujua kazi yako ni temporary au permanent


Ni heri ingewekwa wazi kama ajira zetu ni za mkataba Kwa maana ya temporary na wangespecify duration, ingetusaidia sana, Kwa maana Wakurugenzi wamekuwa hawapitishi barua za transfer ukipata sehemu nyingine wala hawapitishi barua za maombi ya kazi za utumishi ili twende kwenye Kada zetu tulizozisomea Kwa maana huku tulipo hawatutambui


ikikupendeza Mheshimiwa Rais tunakuomba Sana utusaidie kupata haki zetu Kwa maana ya kuthibitishwa kazini na kupatiwa barua ya ajira ili tuweze kufanya kazi Kwa Amani kwenye mioyo yeti na kuongeza weledi wa kazi

Kwani ni haki ya mtumishi akimaliza probation period ya mwaka mmoja kuthibitishwa kazini na kupewa barua ya ajira,

Naomba
Kuwasilisha
Swala la kwenda kusomea PGD lisiwe swala la ulazima liwe option maana katika walioajiriwa kuna wengine walisomea ELImu ya ufundi(vocational teachers)

Pia swala hili katibu mkuu analijua maana alishawahi fikishiwa na Abdul nondo na akasema atalifanyia kazi lkn kimya mpk leo hawa vijana hawajui hatma yao katika hio ajira wakurugenzi na maafisa utumishi wao wanawaambia wanasubiri maelekezo toka juu huu mwaka wa 3 sasa unaenda kuisha. Na Huku tume ya waalimu haiwatambui pia.
Ikiwa hawa wahandisi wazalendo wanajitoa katika kuelimisha wadogo zao

Kikubwa serikali iwathibitishe hao wahandisi kwa fani zao lakini viendelee kuwa hapo mashuleni hii itasaidia baadae mtu atapanda daraja na cheo kutokana na taaluma yake. Na hata akitaka kuhama hawezi anza upya katika idara atakayohamia na pia itawasaidia serikali pale watakapoitaji wataalam.

Pia serikali iajiri walimu wa ufundi maana kuna kozi imeanzishwa pale MUST na vijana wanamaliza mwaka huu.

Pia hawana 1)barua ya ajira 2) mkataba wa kazi 3) barua ya kituo cha kazi 4) barua ya uthibitisho kazini. Kitu ambacho kinapingana na standing orders ya utumishi wa umma.

Katibu mkuu tamisemi tatua hili tatizo watu wajue wanaitumikia vp nchi yao.
 
Back
Top Bottom