Wapi ninaweza kupata maboksi ya pizza?

Wapi ninaweza kupata maboksi ya pizza?

JZHOELO

Senior Member
Joined
Sep 20, 2011
Posts
196
Reaction score
360
Habari wanajamvi,

Hapa karibuni nimefungua pizza and burger shop ila nimejikuta nakwama katika suala zima la packaging, hususani kwenye upande wa pizza.

Maboksi niliyokuwa nayatumia awali niliagiza kutoka Arusha kuja Mwanza ila yalikuwa ni madogo na hayavutii. Na kwa hapa Mwanza kuna wahindi wanauza maboksi ila sio ya square ni ya round na bado hayavutii.

Nilikuwa naomba msaada kwa yeyote mwenye ufahamu na wapi ninaweza kupata maboksi ya pizza meupe au hata printed yawe ya square na kuanzia 14 square inches hadi 18 square inches. Sample ni kama hizi box hapa chini.

Packaging ni muhimu kuwa na mvuto maana ndicho mteja anachokiona kabla ya bidhaa na kisaikolijia mtu yeyote huwa anahamasishwa na muwasilisho wa bidhaa kabla hata ya bidhaa yenyewe.

Nashukuru kwa msaada wowote.

Take-1-YV121108368363-2_mod_web.jpg
56367337-pizza-box-cardboard-packaging-package-vector-set-isolated-on-white-background.jpg
56367337-pizza-box-cardboard-packaging-package-vector-set-isolated-on-white-background.jpg
67180053-brown-pizza-box-template-isolated-on-white-background.jpg
Open_Pizza_Box_PNG_Clip_Art-1272.png
Take-1-YV121108368363-2_mod_web.jpg
56367337-pizza-box-cardboard-packaging-package-vector-set-isolated-on-white-background.jpg
67180053-brown-pizza-box-template-isolated-on-white-background.jpg
Open_Pizza_Box_PNG_Clip_Art-1272.png
Take-1-YV121108368363-2_mod_web.jpg
 
waone hawa www.Merriam.co.za box zao ni kuanzia tsh 640 mpaka 1120 kwa fedha za kitanzania wapo pretoria ukihitaji naweza kununua na kutuma ntakapokua huko kwa sasa nipo Tanzania sio big deal zipo nyingi tuu kwa mwezi unahitaji kiasi gani au kama una mtu SA angalieni namba ya simu humo anakununulia anatuma tuu mabox hayo kodi yake ipo kidogo tuu ukishindwa nikiwa huko ntakusaidia kuzipata...tukumbushane tuu
 
Nenda kariakoo, Yale maduka yanayozunguka soko dogo shomoni uliza duka la kipara utayapata yenye quality nzuri Sana
 
Ni merrypak.co.za
shukran kwa msaada wako mkuu ila kwa sasa nilikuwa nahitaji soko la ndani maana niwe na urahisi wa upatikanaji.. nimekwisha fanya research hadi china wanauza box kwa sh 120 tzsh na ni la nch 19 printed, ila wao wanataka order za piece kuanzia 5000.. again thank you sana kwa majibu yako positive mkuu
 
Nenda kariakoo, Yale maduka yanayozunguka soko dogo shomoni uliza duka la kipara utayapata yenye quality nzuri Sana
sawasawa kaka.. ingawa kwa sasa nipo mwanza ila nina jamaa yangu yupo dar nitamjulisha akanitizamie mkuu, nadhani naanza kuuona mwanga kupitia wazo lako mkuu. nashukuru sana
 
Back
Top Bottom