Wapi naweza kupata folding table au meza ya kujikunja?

Wapi naweza kupata folding table au meza ya kujikunja?

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,633
Reaction score
6,563
Nina mahitaji ya haraka ya folding table au meza za kujikunja kama hii hapa kwenye picha. Zinapatikana wapi hapa Dar es Salaam?

Meza kama hii unaweza kunja miguu yake na hata zingine unaweza kuzikunja mara mbili. Tena hii unayoweza kuikunja mara mbili ndiyo hasa naitaka. Hii inasaidia katika ubebaji na usafirishaji wake.


20210101_224807.jpg
 
Alibaba na aliexpress online market ndiko zilipo ingia online kwa simu yako uagize
 
Hivi ni kwamba uzi wangu hamuuoni au mmeamua tu kuanza mwaka na kiburi na roho mbaya?
[emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji28] Dah.

Wanakuja mkuu kuwa na subira.
 
Ukimpa fundi anakutengenezea kiulaini tu tena mbao unayotaka
 
Ukimpa fundi anakutengenezea kiulaini tu tena mbao unayotaka
Mbao tena ndugu yangu? Mimi nataka iliyo rahisi kubeba na kuweka nyuma ya siti ya gari au kwenye buti. Nitakuwa natembea nayo sana kwa hiyo wepesi ni muhimu sana. Kwa hiyo ya plastiki ndiyo inafaa.

Kama ile ya kwenye picha au hiyo aliyopost mdau hapo juu ndiyo best.
 
Mbao tena ndugu yangu? Mimi nataka iliyo rahisi kubeba na kuweka nyuma ya siti ya gari au kwenye buti. Nitakuwa natembea nayo sana kwa hiyo wepesi ni muhimu sana. Kwa hiyo ya plastiki ndiyo inafaa.

Kama ile ya kwenye picha au hiyo aliyopost mdau hapo juu ndiyo best.
Kwahiyo ya mbao hutaki hata kama inajikunja?
 
Kwahiyo ya mbao hutaki hata kama inajikunja?
Labda sijui ni mbao gani mnazoongelea. Mkisema mbao nawaza vitanda na makabati yetu yalivyo mazito na makubwa. Mimi nataka kitu ambacho kwanza kinachukua sehemu ndogo baada ya kuikunja na pia isiwe na uzito. Na bei iwe ndani ya bei nayoweza kumudu.

Je mafundi wetu wanaweza kutimiza vigezo hivyo na wakati huo huo kutengeneza kitu chenye mvuto?

Nimewahi kujaribu kuwapa michongo mafundi wetu hawa kwa vitu kama hivi, nikaishia kuwa disappointed tu.
 
Back
Top Bottom