Wapi nakosea?

Wapi nakosea?

Slim5

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
28,374
Reaction score
38,248
SOMO – WAPI NAKOSEA?
Nikiwa mtoto niilifurahia maisha yangu ya utoto kama watoto wengine. Nilipokuja kupata akili za kipindi cha utoto, nilianza kupata maumivu kama mtoto kutokana na kutokuwepo kwa baba! Ile kutokumjua baba tu kwangu ilikuwa ni adhabu tena kubwa sana! Niliumia shuleni, niliumia nyumbani kila watoto wenzangu wanapotumia msamiati “baba”. Muda wote wa utoto na maisha ya elimu ya msingi nimekuwa nikiamini kuwa nina mzazi mmoja tu – MAMA! Huyu kwangu alikuwa both, a mother and a father at all time! Ni aina ya mama ambaye alijitambua, na alijua nini kinampasa kufanya katika mazingira ya kuachiwa watoto wawili wa kiume na mwanaume ambaye si tu aliingia mitini, hakugeuka nyuma, bali pia hakutaka kuskia wala kusimulia chochote kuhusu yeye kuwa na watoto wawili wa kiume somewhere in Tanzania!
Hapa namzungumzia “baba” ambaye aliyakimbia majukumu ya kifamilia si kwa vile hakuwa na kipato, laa hasha, alikuwa financially powerful, mtu na ajira yake, mtu na pesa zake! Alikuwa mmoja watu wenye nyadhifa ktk taasisi aliofanyia kazi! Aliishi maisha ya anasa na starehe, wanasema alikuwa mzuri katika anasa za dunia, wapenda anasa wanasema alikuwa mtu mwema sana! Haya yamesemwa na watu wake wa karibu, ndg na jamaa zake waliokuwa nae, akiwemo dadake! Mpaka naandika uzi huu, sijawai kujua nini kilimuachanisha na mamangu mpendwa (rip) na bahati nzuri pia sikuwai kuwa na haja ya kujua sababu!


Maisha ya wakati wa utoto yalikuwa magumu sana, mama hakuwa na uwezo wa kumudu gharama za maisha kwa familia yake kwa kiwango chote, alijitahidi kadri ya uwezo wake kuzimaliza changamoto zetu, na tulimshukuru mungu kwa kile kidogo alichotupatia (rip my hero mama). Pia tulimshukuru mungu kuwa na mama huyu! Bahati iliyopo ni kwamba tulikuwa na uwezo darasani, mimi na kakangu na bahati ikaja tukafaulu la 7 kwenda sekondari! Haya yanatokea baba hajulikani yu wapi! Hajui watoto tu wapi!


Mama aliugua, na 12[SUP]th[/SUP] April 1996 my mama gone to glory [rip mama]. From here, the situation became worse than before! things turned upside – down to my side!
Na mwishoni mwa mwaka huo ndio kwa mara ya kwanza nakutanishwa na baba, I was 18 yrs old! Naikumbuka ile conversation: Tukiwa mezani tunakula, shangazi anamuuliza baba, huyu kijana hapa unamjua? (mm na baba tukiwa tunatizamana mezani). Baba anamjibu hapana! [akilini baba alihisi dadake kapata new shamba boy] then anaambiwa huyu ni ********! Baba anashtuka! Taharuki! Ananiuliza: “ninyi mpo wawili, wewe ndio mkubwa ama mdogo?” [wanaume wenzangu hata kama hawa kinamama wana matatizo yao, tusifikie hatua hii] Halafu akaniuliza kuhusu mama, nikamjibu tumemzika mwaka huu! Taharuki! Shangazi anadakia mazungumzo yetu, anamuelezea kwa niaba yangu kuhusu msiba huo, nilishaanza kulia! Shangazi alibahatika kuhudhuria mazishi ya mama.

Nayakumbuka sana maisha yangu ya sekondari, maisha ya mtaa yalinifundisha kitu more or less similar to what I learnt in school system. Nilipokuwa kidato cha pili tayari nilishajua namna ya kufanya biashara za kimachinga tena za aina mbali mbali ktk jiji la DSM (nikienda DSM wakati wa likizo) nyakati ambazo wenzangu wanahaha kubadili tuition 1 baada ya nyingine kutafuta walimu wazuri!


Mpaka nafika Form 4 nilishajua kuuza misokoto, nilishamjua pusha, nilishajua nini maana ya booster! Nilishakuwa na uhusiano wa karibu na mateja! Najua bidhaa yao inapatikanaje pale mkoani kwetu! Nilishajua namna gani DSM mzigo unaingia! Kwa nini nisijue wakati walionifadhili maisha yangu ya mtaani na shuleni, hizo zilikuwa shughuli zao za kila siku! Katika njia hii nilimpoteza my only lovely brother (rip brother). Pengine kukosa muongozo kulichangia, na pia labda iliandikwa iwe – ikawa! Thanks lord I had never used such a stuff! Wana-JF mnajua madhara ya mtoto wa rika la sekondari kukosa muongozo wa maisha, kukosa mtu wa kumsimamia kwa karibu! Kumuacha mtoto wa umri huu afanye anachoweza! Hayo maisha niliyapitia!


To cut the story short! Nilifanikiwa kumaliza A – level, nikafanya undergraduate, then nikafanya postgraduate udsm. Nina ajira yangu ya serikali! A good loving wife ambae nilikutana nae kipindi cha dhiki iliopitiliza (kama unasoma huu uzi, jua nakupenda sana, una maana kubwa sana kwangu). Tumebahatika kupata 2 baby girls! Mkubwa anasoma shule nzuri, mdogo is only 1.5 yrs old.


Turudi kwa “baba”. Yupo ktk maisha yake ya uzee. Vijana wanasema amefulia! Amebaki kuwa ni mkulima wa hapa na pale. Sasa hv anapigania afya yake hospitalini, anaumwa huko aliko. Namhudumia na kumpa msaada [tigopesa, mpesa zinahusika hapa] kadri ninavoona naweza. Watu wake wa karibu (wengi wao nawaskia kwa majina tu mf. Baba mdg, baba mkbw n.k) wananilaumu kuwa sijajitolea kiwango cha kutosha! Sijajitolea kama mtoto anavojitolea kwa mzazi wake! Wanasema sina mapenzi na baba. Mimi najua mapenzi ni natural, an inborn attitude, huwezi ambiwa PENDA na wewe UKAPENDA! Kweli sina mapenzi nae, lakini nambieni naanzia wapi kumpenda “baba”? Naendelea kupokea lawama! Unaesoma uzi huu, naomba nasaha zako, hapa mimi nakosea wapi? Pia zingatia kuwa mimi ni mwanadamu, kama ambavyo yeye pia! Siwezi kuvaa viatu vya kulipiza, ila haya ni maisha yangu na yeye ana maisha yake!
 
Pole kwa yote mazito uliyopitia

Najua hali kama hiyo kisaikolojia inakunyima raha sana, ila wewe usisikilize sana maneno ya watu, jitahidi pale utakapoweza kwa uwezo wako, watakaosema waachje waseme

Huwezi mridhisha kila mmoja hapa ulimwenguni
 
pole sana mkuu kwa uliyopitia hongera za dhat zimfikie pia huyo malaika malikia wako.
Back to the topic.wewe huna kosa lakin huna budi kujiongezea baraka na neema kwa kumhudumia baba yako,ni ngumu lakin inawezkana!
 
^^
Unapokosea ni pale unapofikiri utaweza kupendeza kila jicho la mwanadamu.
Unapokosea ni pale unapojilaumu na kujihukumu moyoni kwa makosa ambayo si yako.
Mkono hujikuna unapoweza. Fanya unayoweza na hakika utafanikiwa. Kuna wakati tunatakiwa tusiumie sana pale watu wapatapo thawabu zao wangali duniani.
^^
 
So sad jamani, pole sana.

Ukiwa kama binaadam wengine huwezi kuwa na mapenzi na baba yako, thats normal hata hao wanaokusema wanajua kabisa ndani ya mioyo yao. Wanasema mzazi ni Mungu wa duniani, so nakushauri tu timiza wajibu wako kadiri ya uwezo wako kwa huyo mzazi wako. Jitahidi sana kutomuonesha kinyongo JUST FOR GOD!Namaanisha mfanyie wema kwa sababu Mungu anataka tuwafanyie wema hata wale waliotutendea mabaya, and trust me, God will pay you back!!

Hao ndugu wanaokusema achana nao, wala wasikupe shida. Tafuta muda ukamtembelee mzee na umpatie mahitaji yake ya muhimu, na ikibidi fanya zaidi ili baba yako AONE AIBU MWENYEWE!

Pole sana
 
Hujakosea mkuu! Kwanza ubarikiwe kwa kie kitendo tu cha kumsaidia baba yako!

Hao wapambe nuksi hata humu JF wamo, so wewe endelea kumuogopa Mungu na kufanya yako.
 
hadithi nyingi za maisha ya kitanzania zinaendaga hivi hivi.. pole sana kijana kwa yaliyokusibu..

lakini kwanini baba ajiuguze huko? kwanini usimlete angalau kweny ehospitali njema huku mjini ili apone mapema?
 
Pole sana, msaidie kadri utakavyoweza kwani atabaki kuwa mzazi wako japo aliyakwepa majukumu yake, Ndugu wasikuumize kwa maneno yao,hata ukitenda wema kiasi gani bado watasema tu.
 
Una moyo sana kaka. Mimi sidhani kama ningeweza hata kumtumia vocha ya mia tano
 
  • Thanks
Reactions: Luv
So sad jamani, pole sana.

Ukiwa kama binaadam wengine huwezi kuwa na mapenzi na baba yako, thats normal hata hao wanaokusema wanajua kabisa ndani ya mioyo yao. Wanasema mzazi ni Mungu wa duniani, so nakushauri tu timiza wajibu wako kadiri ya uwezo wako kwa huyo mzazi wako. Jitahidi sana kutomuonesha kinyongo JUST FOR GOD!Namaanisha mfanyie wema kwa sababu Mungu anataka tuwafanyie wema hata wale waliotutendea mabaya, and trust me, God will pay you back!!

Hao ndugu wanaokusema achana nao, wala wasikupe shida. Tafuta muda ukamtembelee mzee na umpatie mahitaji yake ya muhimu, na ikibidi fanya zaidi ili baba yako AONE AIBU MWENYEWE!

Pole sana

WALIMWEUSI nashukuru kwa ushauri wako, ni kweli sijaenda kumuona, nimekuwa nikiongea nae tu kwa simu, najipanga hapa ofisini soon ntaenda kumuona!
 
Pole ndugu yangu, kwa akili ya kibinadamu huwezi trust me, mimi kuna vitu nilipitia kuhusu ndugu ambavyo mpaka leo bado vinaniumiza nimejaribu sana kusahau na ku move on lakini wapi nimebaki kumuomba Mungu anipe uwezo wa kusahau na kuwapenda tena, kwani naamini kwa uwezo wake tu ndo ntaweza hivi hivi sitaweza, basi na wewe nakushauri kumbuka kwamba tunatakiwa kuweka hazina mbinguni na si duniani, hivyo basi tunapasawa kuwapenda zaidi wale wanaotuumiza kwani kuwapenda wale watupendao hakuna ziada yoyote kwa Mungu. Muangalie baba yako kwa macho ya rohoni na si kwa macho ya nyama ili uweze kutenda yakupasayo. Mungu akutie Nguvu kaka
 
Una moyo sana kaka. Mimi sidhani kama ningeweza hata kumtumia vocha ya mia tano

Najaribu kushindana na hisia na moyo dadangu kat.ph, nashukuru sana!
 
Pole ndugu yangu, kwa akili ya kibinadamu huwezi trust me, mimi kuna vitu nilipitia kuhusu ndugu ambavyo mpaka leo bado vinaniumiza nimejaribu sana kusahau na ku move on lakini wapi nimebaki kumuomba Mungu anipe uwezo wa kusahau na kuwapenda tena, kwani naamini kwa uwezo wake tu ndo ntaweza hivi hivi sitaweza, basi na wewe nakushauri kumbuka kwamba tunatakiwa kuweka hazina mbinguni na si duniani, hivyo basi tunapasawa kuwapenda zaidi wale wanaotuumiza kwani kuwapenda wale watupendao hakuna ziada yoyote kwa Mungu. Muangalie baba yako kwa macho ya rohoni na si kwa macho ya nyama ili uweze kutenda yakupasayo. Mungu akutie Nguvu kaka

Nashukuru Mrsleo! Nitajitahidi wng
 
Najaribu kushindana na hisia na moyo dadangu kat.ph, nashukuru sana!

Nina rafiki zangu kama wanne hivi...na wao wameyapitia hayo. Wameshindwa kabisa kuwasamehe... wewe una moyo wa ajabu sana. Keep it up.
Mie siwezi
 
Hujakosea mkuu! Kwanza ubarikiwe kwa kie kitendo tu cha kumsaidia baba yako!

Hao wapambe nuksi hata humu JF wamo, so wewe endelea kumuogopa Mungu na kufanya yako.

Nashukuru sana, nafanya mchakato wa ruhusa ofisini ya wiki 1 niende nikamuone!
 
kaka..mimi sikupi pole nakupa bigUP...hayo ndio maisha uliyoandikiwa uyapitie..kama kweli umemshika Mungu na maandiko yake matakatifu nakushauri nenda kamuone mzee wako ujue anaendeleaje...fahamu kila jambo lina kusudi maalum..

usimhukumu baba yako,haya maisha wamepitia wengi sana...nenda tafadhali!!
 
hadithi nyingi za maisha ya kitanzania zinaendaga hivi hivi.. pole sana kijana kwa yaliyokusibu..

lakini kwanini baba ajiuguze huko? kwanini usimlete angalau kweny ehospitali njema huku mjini ili apone mapema?

kule aliko anaishi na mke wake, na wana watoto wawili! watoto hao walionyesha nia yakumpeleka DSM akatibiwe, "mama" akakataa kwa maelezo atamuuguza mwenyewe!
 
kaka..mimi sikupi pole nakupa bigUP...hayo ndio maisha uliyoandikiwa uyapitie..kama kweli umemshika Mungu na maandiko yake matakatifu nakushauri nenda kamuone mzee wako ujue anaendeleaje...fahamu kila jambo lina kusudi maalum..

usimhukumu baba yako,haya maisha wamepitia wengi sana...nenda tafadhali!!

Kweli tupu mkuu, nashukuru kwa ushauri mkuu!
 
Una moyo sana kaka. Mimi sidhani kama ningeweza hata kumtumia vocha ya mia tano

Wee kama mimi.....!
maana kabla sijamaliza kusoma kichwa kilishaanza kuuma!
R.I.P mama! na hongera kwa kupata replacement ya mama (mkeo)
 
Nashukuru sana, nafanya mchakato wa ruhusa ofisini ya wiki 1 niende nikamuone!

yeah, you do that.

He is your father my friend, even though he wasn't much of a Dad.

But one thing is for sure, you are gonna miss him when he is gone so do what you can now.
 
Back
Top Bottom