Ugari una mboga zake, siyo ugari nyama au maharage, ugari mboga zake kama samaki wa kukaanga, nyama choma, mlenda sijui bamia ya kuchanganyikiwa na biringanya nyanya changu daaah, au ugari makange ya kuku au ya mbuzi
Huo Kigoma wanaula na dagaa wa mawese, lakini kwetu Pemba twala mhogo na papa, kisha twapumzika, kwa shibe, kiza kikiingia twaenda pwani maana hakuna vyoo.
Mimi ninapenda sana kula ugali, ninaweza kula chakula hiki siku saba za juma mradi tu nibadilishe kitoweo. Kuna wanaume nikiwaeleza mapenzi yangu kwa ugali wananiona mlugaluga.
Imebidi nipunguze ulaji wa ugali kutokana na issue za uzito wa mwili. Siku hizi ninakula ugali Jumamosi tu. Kuna wanawake wanaopenda kula ugali kama mimi?
Ha ha haaaa, nilishukiaga pale Bweli stand, Musoma town nikamkuta dada wa kikurya anakamua ugali wa mtama na kichuri ndo nikajua "Sasa umeingia kanda ya wababe "
unaishi tanzania apa apa au upo nchi za ugenini mana nikifuatiliaga post zako unaonekana kama upo nchi za ighaibuni sasa uko ugaibuni ugali unapataje...???