Yofav
JF-Expert Member
- Mar 12, 2021
- 4,331
- 7,955
Habari yenu wakuu,
Huu uzi kama unavyojieleza hapo ni kwaajili ya wapambanaji wenzangu katika maisha, hivi katika hali ya kawaida upo kwenye 20-30yrs and still maisha hujayapatia kivile kwa kuwa una uwezo wa kujilisha wewe pekee yako hivyo basi hauna mke wala mtoto kwa wakati huo, Ila unakuta una wazazi ambao uliwaacha mji mwingine na wewe upo mji mwingine unatafuta.
aba aliachana na Mama hivyo pia hawaishi pamoja ila wewe kama mtoto still unawasiliana na wote normal pia kuna wakati kila mmoja anakulilia shida yake na unajaribu kutatua bila shida ila sasa inafika sehemu unatafakari maisha yako kiujumla kila ukicheki kesho yako unaona ina kipengele (Kama vile haina uhakika sana) Na ni heri basi ungekuta una elimu unayoitegemea kwa kiasi fulani lakini pia hauna elimu yoyote unaishi tu kiujanjaujanja na Msaada wa Mungu tu.
Ni heri ungekuwa una-focus kujiwazia kesho yako pekee lakini sivyo kwani unawaza Kesho yako pamoja na ya wazazi wako pia kwani umri unakwenda na huko mbele wao watahitaji msaada wako zaidi ya sasa. Mbaya zaidi wazazi washajenga ile mentality kwamba unapaswa uwasaidie shida zao kuanzia muda huu, Mama ni 38yrs na Baba 48yrs.
Ebu tushauriane hapa wakuu nawezaje ku-handle hii hali na niwe na future poa huko mbele maana sina mke wala mtoto ila pia mbele napaswa kuwa nao, Na pia mbele hukohuko napaswa pia kuwasaidia wazazi kwani wanaonesha kabisa huko mbele nina kazi kubwa sana kuliko hata sasa japo hata sasa nishaanza kulemewa, Kuna wakati nakula nikiwa na mawazo kwamba pengine nakula lakini wazazi wangu hawali huko walipo, Nashindwa kuwa huru kufurahia maisha kwa kuwa naona pengine nafurahi na wazazi wangu hawafurahi
Note: Sinywi pombe, Sio mtu wa mbususu (Single✅), Hunikuti viwanja na yote hiyo ni kwa kuwa sina hela ya kukidhi vyote hivyo, Ao starehe yangu kubwa naweza kusema ni kula.
Kama upo kwenye situation hii niambie unawezaje kui-handle na hata kama una ushauri nini nifanye ili niende sawa na niweze kuifurahia kesho yangu.
Karibu sana kwa maoni na ushauri wako.
Huu uzi kama unavyojieleza hapo ni kwaajili ya wapambanaji wenzangu katika maisha, hivi katika hali ya kawaida upo kwenye 20-30yrs and still maisha hujayapatia kivile kwa kuwa una uwezo wa kujilisha wewe pekee yako hivyo basi hauna mke wala mtoto kwa wakati huo, Ila unakuta una wazazi ambao uliwaacha mji mwingine na wewe upo mji mwingine unatafuta.
aba aliachana na Mama hivyo pia hawaishi pamoja ila wewe kama mtoto still unawasiliana na wote normal pia kuna wakati kila mmoja anakulilia shida yake na unajaribu kutatua bila shida ila sasa inafika sehemu unatafakari maisha yako kiujumla kila ukicheki kesho yako unaona ina kipengele (Kama vile haina uhakika sana) Na ni heri basi ungekuta una elimu unayoitegemea kwa kiasi fulani lakini pia hauna elimu yoyote unaishi tu kiujanjaujanja na Msaada wa Mungu tu.
Ni heri ungekuwa una-focus kujiwazia kesho yako pekee lakini sivyo kwani unawaza Kesho yako pamoja na ya wazazi wako pia kwani umri unakwenda na huko mbele wao watahitaji msaada wako zaidi ya sasa. Mbaya zaidi wazazi washajenga ile mentality kwamba unapaswa uwasaidie shida zao kuanzia muda huu, Mama ni 38yrs na Baba 48yrs.
Ebu tushauriane hapa wakuu nawezaje ku-handle hii hali na niwe na future poa huko mbele maana sina mke wala mtoto ila pia mbele napaswa kuwa nao, Na pia mbele hukohuko napaswa pia kuwasaidia wazazi kwani wanaonesha kabisa huko mbele nina kazi kubwa sana kuliko hata sasa japo hata sasa nishaanza kulemewa, Kuna wakati nakula nikiwa na mawazo kwamba pengine nakula lakini wazazi wangu hawali huko walipo, Nashindwa kuwa huru kufurahia maisha kwa kuwa naona pengine nafurahi na wazazi wangu hawafurahi
Note: Sinywi pombe, Sio mtu wa mbususu (Single✅), Hunikuti viwanja na yote hiyo ni kwa kuwa sina hela ya kukidhi vyote hivyo, Ao starehe yangu kubwa naweza kusema ni kula.
Kama upo kwenye situation hii niambie unawezaje kui-handle na hata kama una ushauri nini nifanye ili niende sawa na niweze kuifurahia kesho yangu.
Karibu sana kwa maoni na ushauri wako.