PostGE2025 Waombelezaji wanatishwa, hakuna kuongelea misiba iliyotokea wakati wa maandamano, wanamaliza misiba bila miili!

PostGE2025 Waombelezaji wanatishwa, hakuna kuongelea misiba iliyotokea wakati wa maandamano, wanamaliza misiba bila miili!

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Black Opal

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2023
Posts
304
Reaction score
543
Wakuu,

Hiki ndio kinachoendelea mtaani kipindi hiki! Wakati wa maandamano wananchi walishuhudia wapendwa wao wakipigwa risasi na polisi na kuona miili ikizagaa mtaani wengine mpaka siku tatu.

Walipojaribu kuchukua miili hii kwa taratibu nyingine za kupumzisha wapendwa wao, polisi waliwakataza, na kuwaambia miili itapelekwa katika hospitali husika (kutegemea na eneo) na wataweza kuichukua huku, lakini sicho kilichotokea.

Wakienda hospitali na kuomba miili ya wapendwa wao wanaambiwa haipo, hata kama mtu alifia hospitalini hapo!

Sasa huku mtaani shida zinaendelea! Misiba inafanywa na kumalizwa bila ya kuwa na miili. Na waandishi wakijaribu kupata taarifa hawapati ushirikiano toka kwa wananchi kutokana na hofu walizonazo. Ni kama polisi wamepita mitaani na kutisha wananchi kuongea na vyombo vya habari, jambo linalokuwa changamoto kupata taarifa kipindi hiki.

Yaani serikali inafanya kila jambo kuhakikisha wanazuia taarifa, lakini wanazuia vipi na mambo yapo akilini mwa kila mtu na vithibitisho kadha wa kadha kwenye simu zetu?

Yaani mmekosa kabisa njia bora ya kuwajibika na hili na kuponya mioyo ya Watanzania inayovuja damu? Hizi hasira zinazoongezeka zitakuja kuleta crisis kubwa zaidi ya hii iliyotokea, na kwa mara nyingine tumewaonya muda mrefu lakini mmeshupaza shingo.
 
Kuna kanisa nilipita juzi nikaona kuna msiba, nikauliza nikaambiwa kijana alipigwa shaba kwenye maandamano ila nadhani mwili wake uliletwa. Nikakaa pale kusoma watu wanaoingia na kutoka na waliozagaa maeneo yale, nikagundua watu wasiojulikana walikuwa ni wengi. Nikaangaliaaa baadae nikaondoka zangu.
 
Back
Top Bottom