Waomba siku nzima, kufufua maiti

Kazi kweli kweli, wanakondoo bwana

The problem is the bible itself (source)
 
Waumini hao wa kanisa hilo lilillopo nchini Kenya, walilazimika kuyaamini maneno hayo baada ya kuamua kufanya kazi ya kuwafufua wachungani wawili wa kanisa hilo waliofariki kwa ajali ya gari

Kwa mujibu wa habari kutoka Nakuru, Kenya ambako ndiko liliko kanisa hilo, Jumamosi iliyopita waumini hao walijikusanya mbele ya majeneza mawili ya wachungaji wao huku wakiongozwa na mtume John William Kimani kuomba siku nzima wakiaamini kuwa wachungaji hao wangefufuka na kutoka ndani ya majeneza.

Kabla ya kuanza kwa ibada hiyo ya kuwafufua marehemu hao, waumini waliyafunua majeneza na kupokea maelezo ya kufumba macho na kuendelea na maombi wakitarajia miujiza kwamba marehemu hao watainuka na kukaa kitako wakiwa hai kwenye majeneza waliyokuwamo.

Waumini hao walikuwa wakijaribu kuwafufua kwa miujiza wachungaji wao, Patrick Wanjohi aliyekuwa msaidizi wa kanisa hilo na Fransis Kamau Ndekei aliyekuwa mchungaji wa eneo la Nyahururu, wote walifariki Jumatatu ya wiki iliyopita.

Habari zilisema wachungaji hao walikufa katika ajali ya gari iliyotokea kwenye Barabara ya Nakukuru-Nairobi, ambapo mchungaji Ndekei alifariki dunia mara baada ya kumfikisha hospitali na mchungaji Wanjohi alifariki dunia kwenye eneo la ajali.

Kwa mujibu wa taarifa, waumini hao walikataa kuwazika kwa maelezo kuwa watafanya maombi ya kuwafufua kwasababu kazi waliyotumwa kuifanya duniani bado haijakamilika.

Habari zilisema viongozi na waumini wa kanisa hilo waliamua kufunga kwa siku tatu kuanzia Alhamisi ya wiki iliyopita, kabla ya kufanya maombi maalum ya kuwafufua.

Mtume Kimani alisema hawawezi kuwazika, kwakuwa bado wanawahitaji kwa ajili ya kuliimarisha kanisa.

Eneo la kanisa hilo lilifurika watu na wengine kulazimika kukwea juu ya miti kushuhudia ‘kituko’ hicho cha kuwafufua wachungaji wa kanisa hilo. Kamanda wa polisi wa Nakuru, Johnstone Ipara, alisema wamewaomba waumini hao kuacha kuwafanyia mizaha marehemu hao, na wamewataka wawatendee haki kwa kuwazika.

Mtume Kimai kwa upande wake alisema wamesalimu amri na kwamba wapo kwenye taratibu za mazishi ambayo yanatarajiwa kufanyika kesho.
 
Haijawahi kutokea watu wakaombea mahiti kisha zikafufuka, hii kali...!

Wapewe tu miaka miwili wakae na maiti wakiomba wasiruhusiwe kumuweka kwenye frezeer..wataondoka wenyewe kwa harufu mbaya na hafufuki mtu..maarifa hakuna ndio tatizo la wanakondoo..
 
False Prophets! What is religion coming to? People are so destitute they will look for miracles every where. It's very sad, that this particular congregation does not realize the grand scheme of the CREATOR, JEHOVAH.
When JUDGEMENT day comes they will rise up, but not now. The sooner that these congregants know that the better.
May God rest their souls in Eternal Peace as they await to resurrect on the day of the trumpet.
 
Tatizo ni uelewa mdogo na fanatic profiles za extremists wengi... extremists wa kikristu ni wengi sana siku hizi

Acha warudishwe duniani kwa mifano halisi
 
hizi ni dalili za siku za mwisho.... kutatokea manabii wa uwongo, magonjwa yasiyotibika, kutoelewana kwa mataifa, makanisa ya ajabu ajabu kama haya yakitumia biblia kuhadaa watu nk

this is ridiculous - hapa ni kumjaribu bwana mungu wao - unaombea maiti ifufuke?- hawa jamaa ni kama wale waliowahi kwenda DSM airport bila document yoyote eti wanataka kuzunguka dunia nzima kuhubiri dini wakati hata ticket ya ndege hawana. - eti wanatumia kifungu - enendeni mkawafanye mataifa kulijua neno langu na mkiwabatiza kwa jina la baba na la mwana na roho mtakatifu. Jamaa wakatimuliwa na mapolice - so its same senario with this.

sawa waulize maiti zao zilifufuka?

be careful with this Churches..cha msingi ni shika ulicho nacho....shetani asije akakulaghai ndugu yangu
 
Duh jana niliokuwa natazama TBC1 taarifa ya habari sikuamini nilichokuwa nakitazama kuna baadhi ya wahubiri wanawapotosha waumini wao kiasi kwamba wanakuwa wanawaabudu wao badala ya mwenyezi mungu.

Watumishi wa mungu kama Askofu Kakobe wanaingia moja kwa moja katika hili kundi la kuabudiwa wao badala ya Mungu.Fikiria waumini wanashinda siku nzima kanisa kulinda TANESCO wasipitishe waya kwenye kanisa lao,sijui wanatafuta riziki zao saa ngapi ?.Twende mbali kidogo hivi Askofu Kakobe akitangulia mbele ya haki waumini wake wataacha kufanya vituko kama hao jamaa wa huko Kenya ?.Niliwahi kusema haya makanisa ya aina Mzee wa upako,Askofu Kakobe,Mtume na Nabii Jodev na nk yafaa yatazamwe kwa makini sana kwasababu mara nyingi badala ya kumhubiri Kristo mfufuka yamejikita zaidi kuwatukuza viongozi wao.

Neno la Mungu linasema........... katika siku za mwisho watatokea manabii wa uongo, nao watawadanganya yumkini hata wateule....................katika siku ile watasema, Bwana, si tulifanya miujiza kwa jina lako, tuliponya kwa jina lako........Naye atawajibu ONDOKENI KWANGU ninyi mliolaaniwa.

Kwa hiyo ndugu zangu hizi ni siku za mwisho, yote yaliyotabiriwa katika Mathayo 24 yanatimia, lililopo ni kila mtu kuachana na dhambi.
 
E mwenyezi mungu utuhurumie na kutukumbuka wanao tunaopotoshwa na mbwa mwitu waliovaa mavazi ya kondoo!
 
Tatizo la waumini wengi wa madhehebu mengi ya dini hasa ya kilokole na kipentekositi wanawaamini na kuwaabudu viongozi wao badala ya kumwabudu mungu. Waumini watafanya lolote kiongozi analotaka lifanyike. Neno la MUNGU lipo wazi kwamb "KILA NAFSI ITAYAONJA MAUTI"..
 
Kufufuka inawezekana kabisa. Yesu ndiye ufufuo na uzima.

Wakati anajiandaa kumfufua Lazaro, Mariam na Martha walifikiri anazungumzia ufufuo siku ya kiama.

Kilichoshindikana kwa hawa jamaa ni mambo yafuatayo:

1. Yesu hakumuweka Lazaro kwenye jeneza, wala si yeye aliyemzika, sasa hawa jamaa miili wameiweka wenyewe kwenye jeneza tayari kuzikwa halafu wanaomba ufufuo, hapo hakuna Imani.

2. Yesu alikuwa anakesha milimani akiomba, mpaka kesho yake anapoingia hekaluni uweza wa Mungu unakuwepo kuponya, leo hii wachungaji wanakesha wakisengenyana, wamegeuza makanisa miradi, hapo hakuna uweza wa Mungu bali uweza wa mwekundu wa msimbazi ambao hauwezi kufufua.

3. Yesu alifufua kwa utukufu wa Mungu, hao jamaa wanataka mtu afufuke kwa uchungu binafsi walio nao, na wengine ili wajaze makanisa mapato yaongezeke, hapo Mungu hashawishiki kufufua.

4. Makanisa ya sasa yamemfukuza Roho mtakatifu na kumkaribisha roho ya fedha itawale, sasa bila Roho mtakatifu ufufuo utatokea wapi? Leo hii ukiingia makanisa yao unaendesha Hummer unapewa uzee wa Kanisa siku hiyo hiyo. Kuna ufufuo hapo?

5. Wakristo wa leo wanaogopa uchawi, shetani na kifo kuliko Mungu. Mungu anasema akiogopacho muovu ndicho kimpatacho. Leo hii ukitaka watu waache kusikiliza neno la Mungu na wakusikilize wewe masaa yote wewe danganya kuwa ulikuwa mchawi na sasa umeokoka. Wataacha mambo yote ya maana kanisani ili wasikilize ulivyokuwa mchawi mahiri Afrika nzima ukichezea mapadre, wachungaji na mashehe.

Naomba niishie hapo. Ufufuo unawezekana kabisa isipokuwa mwana wa adamu atakaporudi JE ATAIKUTA IMANI DUNIANI?

Arguments zako ziko kisomi kiasi kwa maana ya kwamba unaamini yote yanawezekana kwa Mungu, lakini ni kwa utashi na mpango wa Mungu mwenyewe, na kamwe si kwa mpango wa mwanadamu. Hapo tuko pamoja.

Nisichoamini hata kidogo hapo ni kuwa ati kuna uwezekano wa kumshawishi Mungu afanye alichokuwa hajakipanga kiwe hivyo. Kama kweli Mungu ni mjuzi na mweza wa vyote, ninaamini kuwa Mungu alijua kabla hata hao wachungaji hawajazaliwa kuwa itafika tarehe hiyo iliyofika ya wao kupata ajali ya gari na kufariki dunia, na kuwa hao wafuasi wao wangeomba sana awafufue na pia Mungu anajua kuwa ombi hilo angelitimiza au la. Na tena basi hata ile hali ya utofauti kuwa kuna watakaoamini hayo na wengine hawataamini, bado ni Mungu pia ndiye aliyeumba tofauti hiyo (tukiamini hakuna muumbaji mwingine, na pia haiwezekani jambo lolote kutokea kama Mungu hataki ama hajaridhia jambo hilo kutokea). Kumbe basi wanaomba nini?

Hivi ukimwomba sana Mungu jambo fulani na likatokea hivyo kweli, ni matunda ya sala zako au ni mpango wa Mungu tangu awali kuwa ilikuwa iwe hivyo ilivyotokea? Na iwapo umemwomba Mungu jambo fulani na hukulipata, ni kwamba Mungu kakukatalia maombi yako au ni uleule mpango wake uliokuwako kabla hata hujazaliwa?

Kuna binadamu mwenye uwezo wa kumshawishi Mungu akubali kubadili mpango wa Mungu? Contradictions! Na wajinga wanaendelea kugugunwa tu! Pole yao.
 
Hata kama Nabii Yesu (as) alifufua mtu, basi ndio kwa nderemo na vifijo namna hiyo?

Na hawa wakiristu wamekuwa kama waganga wa kienyeji... Watakuja na sababu rukuki kwa nini ilishindikana wachungaji wao kufufuka!
 
Arguments zako ziko kisomi kiasi kwa maana ya kwamba unaamini yote yanawezekana kwa Mungu, lakini ni kwa utashi na mpango wa Mungu mwenyewe, na kamwe si kwa mpango wa mwanadamu. Hapo tuko pamoja.

Nisichoamini hata kidogo hapo ni kuwa ati kuna uwezekano wa kumshawishi Mungu afanye alichokuwa hajakipanga kiwe hivyo. Kama kweli Mungu ni mjuzi na mweza wa vyote, ninaamini kuwa Mungu alijua kabla hata hao wachungaji hawajazaliwa kuwa itafika tarehe hiyo iliyofika ya wao kupata ajali ya gari na kufariki dunia, na kuwa hao wafuasi wao wangeomba sana awafufue na pia Mungu anajua kuwa ombi hilo angelitimiza au la. Na tena basi hata ile hali ya utofauti kuwa kuna watakaoamini hayo na wengine hawataamini, bado ni Mungu pia ndiye aliyeumba tofauti hiyo (tukiamini hakuna muumbaji mwingine, na pia haiwezekani jambo lolote kutokea kama Mungu hataki ama hajaridhia jambo hilo kutokea). Kumbe basi wanaomba nini?

Hivi ukimwomba sana Mungu jambo fulani na likatokea hivyo kweli, ni matunda ya sala zako au ni mpango wa Mungu tangu awali kuwa ilikuwa iwe hivyo ilivyotokea? Na iwapo umemwomba Mungu jambo fulani na hukulipata, ni kwamba Mungu kakukatalia maombi yako au ni uleule mpango wake uliokuwako kabla hata hujazaliwa?

Kuna binadamu mwenye uwezo wa kumshawishi Mungu akubali kubadili mpango wa Mungu? Contradictions! Na wajinga wanaendelea kugugunwa tu! Pole yao.

Nilitaka nikupotezee lakini si vizuri ukashindwa kujua sababu ya kukupotezea.

Upeo wako kwenye masuala ya Mungu ninayemzungumzia mimi ni mdogo saaaaana. Naomba tukubaliane kuwa Mungu ninayemzungumzia mimi na unayemzungumzia wewe ni tofauti. Na pia inaonekana tangu uzaliwe huajawahi kusoma Biblia.

Inaonyesha ni mjadala kati ya Christian na Scintologist.

Unachoamini wewe ni kuwa hakuna haja ya kuomba likizo kwa mwajiri wako kwa kuwa anajua una siku kadhaa za likizo.

Unachosema wewe ni kwamba kumwomba Mungu hakuna maana kwa sababu Mungu anajua tayari kila kitu, Kwa hiyo Waumini wa dini zote wanaomuomba Mwenyezi Mungu wanagugunwa kama ulivyo dai?

How old are you? Keep living my child, utakujanikumbuka tu.
 
Kufufuka inawezekana kabisa. Yesu ndiye ufufuo na uzima.

Wakati anajiandaa kumfufua Lazaro, Mariam na Martha walifikiri anazungumzia ufufuo siku ya kiama.

Kilichoshindikana kwa hawa jamaa ni mambo yafuatayo:

1. Yesu hakumuweka Lazaro kwenye jeneza, wala si yeye aliyemzika, sasa hawa jamaa miili wameiweka wenyewe kwenye jeneza tayari kuzikwa halafu wanaomba ufufuo, hapo hakuna Imani.

2. Yesu alikuwa anakesha milimani akiomba, mpaka kesho yake anapoingia hekaluni uweza wa Mungu unakuwepo kuponya, leo hii wachungaji wanakesha wakisengenyana, wamegeuza makanisa miradi, hapo hakuna uweza wa Mungu bali uweza wa mwekundu wa msimbazi ambao hauwezi kufufua.

3. Yesu alifufua kwa utukufu wa Mungu, hao jamaa wanataka mtu afufuke kwa uchungu binafsi walio nao, na wengine ili wajaze makanisa mapato yaongezeke, hapo Mungu hashawishiki kufufua.

4. Makanisa ya sasa yamemfukuza Roho mtakatifu na kumkaribisha roho ya fedha itawale, sasa bila Roho mtakatifu ufufuo utatokea wapi? Leo hii ukiingia makanisa yao unaendesha Hummer unapewa uzee wa Kanisa siku hiyo hiyo. Kuna ufufuo hapo?

5. Wakristo wa leo wanaogopa uchawi, shetani na kifo kuliko Mungu. Mungu anasema akiogopacho muovu ndicho kimpatacho. Leo hii ukitaka watu waache kusikiliza neno la Mungu na wakusikilize wewe masaa yote wewe danganya kuwa ulikuwa mchawi na sasa umeokoka. Wataacha mambo yote ya maana kanisani ili wasikilize ulivyokuwa mchawi mahiri Afrika nzima ukichezea mapadre, wachungaji na mashehe.

Naomba niishie hapo. Ufufuo unawezekana kabisa isipokuwa mwana wa adamu atakaporudi JE ATAIKUTA IMANI DUNIANI?

You are right; the main issue here is Holy Spirit was not there! there was no consent of Holy Spirit in this issues. Their emotions ruled them.

Niliifikiria tena na hiyo point yako ya Imani, you are correct, imani ni hakika, kama mnaomba bado mmeweka mwili kwenye Jeneza mnaomba nini?
 
The only mistake they did is to put them in the caskets, the homes of dead person!...How possible could they come out from those closed "doors"???. Real joking with GOD this guys.....

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=CuqXwOgiOY4"]YouTube- The 'Dead Will Wake Up' Mission[/ame]
 
Speaking as a christian, what they are doing is absurd. Of-course in Jesus name dead can be raised, but with a purpose and a special reasons, and all miraclea are meant to show people who dont believe!

I dont see any spiritual katika hili, ilikuwa ni uchungu na mshtuko walioupata

Poleni kanisa, kila kitu kina sababu

Yeh! give us facts who has been raised apart from Jesus himself. Naona walokole wanavuka mipaka na kutia doa dini yetu.
 
Walokole wengi wana matatizo ya akili na kwa imani yao wanaona kila asiyeokoka hatauona ufalme wa mungu. Na viongozi wao kama bwana kakobe kawafanya waumini wake ndondocha kukaa juani muda wote kuzuia Tanesco wasipitishe nguzo mbele ya kanisa.Hawa jamaa wanafanya kazi ya kuwaingizia kipato saa ngapi?
 
Back
Top Bottom