Wanyamwezi wa Urambo!

Wanyamwezi wa Urambo!

urambo enzi hizo (1951)!

View attachment 40603iyo staili ya nywele ya uyo jamaa wa kushoto ilikuwa inaitwa "way" yaani nywele ziachane kama za mzungu vile!

View attachment 40604hata enzi hizo miembe ilikuwa mingi. Waafrica wanachimbua tairi wakati wazungu wameshika mikono. Kama inavyokuwa sasa (historia inajirudia)!

hao jamaa hapo kwenye picha walikuwa ni manamba au???/
 
nyumba-gladwell.jpg Hiyo nyumba ya mkoloni ilikuwepo kwenye mtaa wa Gladwell huko Urambo. Ingawa paa lilikuwa la nyasi lakini bado inaonekana nzuri na hata umeme ulikuwapo.

siku-ya-kuzaliwa-malkia.jpg Mkoloni akikagua gwaride siku ya sherehe za kuzaliwa Malkia. Urambo 1951. Miaka kumi na moja kabla ya uhuru wa Tanganyika!
 
Nimeipenda hiyo land rover, nafikiri matatizo ya kuibiana power windows na side mirrors hayakuwako enzi hizo!
 
Ndugu yangu hii picha ya stesheni karibu initoe machozi. Hakuna kilichobadilika hata rangi ya jengo ni ile ile aliyoiacha mkoloni. Ile barabara ya kuelekea sokoni nayo ni hivyo hivyo. Nasikia uchungu sana kuona kwetu hakukui hakubadiliki. Kuna mwana jamii mmoja baada ya uchaguzi wa Igunga aliandika anaona aibu kuzaliwa mnyamwezi, mimi najihisi vibaya sana kuona Urambo yetu iko vile miaka yote, watu wanaondoka hawarudi , tena wanaume wa urambo ndio kabisaa tukiondoka huko hata kurudi kuoa wa kwetu hatutaki, tunazidi kupotea
 
Tena huko Urambo hata ndege zilikua zinatua miaka hiyo ingawa kiwanja kilikuwa ndio kama hicho ukionacho (Krismasi 1951)

uwanja-wa-ndege.jpg
 
asante sana Askari Kanzu kwa kutukumbusha asili zetu,tudumisheni tamaduni zetu,mdharau kwao mtumwa.Nalog off
 
Ndugu yangu hii picha ya stesheni karibu initoe machozi. Hakuna kilichobadilika hata rangi ya jengo ni ile ile aliyoiacha mkoloni. Ile barabara ya kuelekea sokoni nayo ni hivyo hivyo. Nasikia uchungu sana kuona kwetu hakukui hakubadiliki. Kuna mwana jamii mmoja baada ya uchaguzi wa Igunga aliandika anaona aibu kuzaliwa mnyamwezi, mimi najihisi vibaya sana kuona Urambo yetu iko vile miaka yote, watu wanaondoka hawarudi , tena wanaume wa urambo ndio kabisaa tukiondoka huko hata kurudi kuoa wa kwetu hatutaki, tunazidi kupotea
Hakika wa Tz wengi ndivyo tulivyo.
 
Ndugu yangu hii picha ya stesheni karibu initoe machozi. Hakuna kilichobadilika hata rangi ya jengo ni ile ile aliyoiacha mkoloni. Ile barabara ya kuelekea sokoni nayo ni hivyo hivyo. Nasikia uchungu sana kuona kwetu hakukui hakubadiliki. Kuna mwana jamii mmoja baada ya uchaguzi wa Igunga aliandika anaona aibu kuzaliwa mnyamwezi, mimi najihisi vibaya sana kuona Urambo yetu iko vile miaka yote, watu wanaondoka hawarudi , tena wanaume wa urambo ndio kabisaa tukiondoka huko hata kurudi kuoa wa kwetu hatutaki, tunazidi kupotea

Mabadiliko yaanze na wewe. Maana kila mtu anamshangaa mwenzake.
 
Hizi picha waliopiga wametutangulia ila watoto wao ambao ni wazee sana sasa ndio wameziweka kwenye Flickr gallery
Ila kuna kasichana ka kizungu walikuwa wanataka kukajua sijui kama walipata jina lake
Ilikuwa 1952
Da umenikumbusha mbali sana
Kwenye mashamba ya karanga
Hiyo Station bado iko vile vile mjerumani balaa
 
Hapo utagundua kuna maeneo Tanzania haipigia hatua. Mwaka jana nilipita hapo stesheni yaani panafanana hivihivi. Hakuna mabadiliko yeyote.

Hata ndani bado mambo yaleyale ya zamani hata compyuta hamna

Unasema computer
Station master anatumia simu janja kuwasiliana na masters wengine zile simu za mezani zilikufa miaka mingi iliyopita , watu walipita na waya zote

Yaani utaona saa ya ukutani iliyoachwa na mkoloni bado ipo hapo
Yaani hakuna mabadiliko kabisa kwa sababu ya udhalili wao wenyewe

Unapewa nyumba unashindwa hata kuipaka rangi
 
Back
Top Bottom