Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Wataalamu wa saikolojia wanalielezea tatizo hili kama tatizo la kiakili. Mtu mwenye tatizo au ugonjwa huu huwa anashindwa kujizuia au kuzuia kishawishi kitokacho ndani mwake cha kuiba, tatizo hili hufahamika kitaalamu kama Kleptomania. Lakini jambo la ajabu ni kwamba kitu hicho ambacho kinaleta ushawishi kuibwa ni kitu ambacho hakina thamani kifedha wala hakina matumizi yoyote kwa mwibaji.
Hapa ni vizuri jambo hili nikaliweka wazi, kwamba, ninachozungumzia siyo tabia ya kuchomolea watu mifukoni au kuwapora mikononi. Hapa ninachozungumzia ni kuiba bila mwibaji kupanga kwamba leo au sasa hivi nijiandae kuiba hiki au kile. Baadhi ya wataalamu wa matatizo ya kiakili wanaamini kwamba, kishawishi cha kuiba kinapomjia mgonjwa huwa kinakuwa kama kitu kipya akilini mwake, yaani kinakua kitu ambacho hakitaki lakini hawezi kukiondoa au kukisimamisha.
Ndipo pale unakuta mtu anafika nyumbani kwako na anajitahidi sana hadi anaiba hata kijiko kidogo cha chai, huku akiwa ni mtu mwenye uwezo wa kutosha. Ndipo pale ambapo unakuta mtu anafika mghahawani na baada kula huiba uma, wakati mtu huyo ana uwezo mkubwa kifedha. Huenda hata wewe umeshawahi kusikia au kumuona mtu mwenye tabia kama hii, ambapo mara nyingi huwa tunamwita mwizi. Kuna wakati unaweza kusikia, "Mwanamke yule ni mwizi kweli, tena anaiba hata vitu visivyo na maana na siyo kwamba ana shida, ila basi tu." Huenda mwanamke huyu anayeongelewa anakabiliwa na tatizo hili la Kleptomania, yaani ugonjwa wa wizi au udokozi.
Kwa kawaida wanaokabiliwa na maradhi haya kama ambavyo nimebainisha, ni wanawake na hasa kuanzia umri wa miaka 36, na maradhi haya hudumu kwa wastani wa miaka 16. Hata hivyo kuna taarifa za kuwepo kwa wagonjwa kama hawa ambao walianzwa na tatizo hilo wakiwa na umri wa miaka mitano. Hakuna hasa ushahidi tatizo hili husababishwa na nini, lakini wataalamu wengi wanaamini kwamba linatokana na kuwepo kwa hitilafu kwenye kemikali ya ubongo iitwayo serotonin. Hii ni kwa sababu vidonge ambavyo huwa vinatumika katika kuondoa sononi vinavyofahamika kwa jina la Prozac, ambavyo huwa vinaongeza kiwango cha kemikali hii ya serotonin, vilitumika kwa wanawake wenye tatizo hili. Wanawake hao walipata nafuu kubwa.
Wanawake wenye tatizo hili ni vigumu sana kwao kujenga uhusiano au ndoa imara kwa sababu wanaume wengi huwakwepa kwa kuogopa fedheha watakayoipata katika jamii. Mara nyingi huishia kuzalishwa na kutelekezwa. Ni pale tu watakapokuwa wamepona tatizo hilo ndipo watakaponusurika na adha ya kukimbiwa na wanaume.
Hapa ni vizuri jambo hili nikaliweka wazi, kwamba, ninachozungumzia siyo tabia ya kuchomolea watu mifukoni au kuwapora mikononi. Hapa ninachozungumzia ni kuiba bila mwibaji kupanga kwamba leo au sasa hivi nijiandae kuiba hiki au kile. Baadhi ya wataalamu wa matatizo ya kiakili wanaamini kwamba, kishawishi cha kuiba kinapomjia mgonjwa huwa kinakuwa kama kitu kipya akilini mwake, yaani kinakua kitu ambacho hakitaki lakini hawezi kukiondoa au kukisimamisha.
Ndipo pale unakuta mtu anafika nyumbani kwako na anajitahidi sana hadi anaiba hata kijiko kidogo cha chai, huku akiwa ni mtu mwenye uwezo wa kutosha. Ndipo pale ambapo unakuta mtu anafika mghahawani na baada kula huiba uma, wakati mtu huyo ana uwezo mkubwa kifedha. Huenda hata wewe umeshawahi kusikia au kumuona mtu mwenye tabia kama hii, ambapo mara nyingi huwa tunamwita mwizi. Kuna wakati unaweza kusikia, "Mwanamke yule ni mwizi kweli, tena anaiba hata vitu visivyo na maana na siyo kwamba ana shida, ila basi tu." Huenda mwanamke huyu anayeongelewa anakabiliwa na tatizo hili la Kleptomania, yaani ugonjwa wa wizi au udokozi.
Kwa kawaida wanaokabiliwa na maradhi haya kama ambavyo nimebainisha, ni wanawake na hasa kuanzia umri wa miaka 36, na maradhi haya hudumu kwa wastani wa miaka 16. Hata hivyo kuna taarifa za kuwepo kwa wagonjwa kama hawa ambao walianzwa na tatizo hilo wakiwa na umri wa miaka mitano. Hakuna hasa ushahidi tatizo hili husababishwa na nini, lakini wataalamu wengi wanaamini kwamba linatokana na kuwepo kwa hitilafu kwenye kemikali ya ubongo iitwayo serotonin. Hii ni kwa sababu vidonge ambavyo huwa vinatumika katika kuondoa sononi vinavyofahamika kwa jina la Prozac, ambavyo huwa vinaongeza kiwango cha kemikali hii ya serotonin, vilitumika kwa wanawake wenye tatizo hili. Wanawake hao walipata nafuu kubwa.
Wanawake wenye tatizo hili ni vigumu sana kwao kujenga uhusiano au ndoa imara kwa sababu wanaume wengi huwakwepa kwa kuogopa fedheha watakayoipata katika jamii. Mara nyingi huishia kuzalishwa na kutelekezwa. Ni pale tu watakapokuwa wamepona tatizo hilo ndipo watakaponusurika na adha ya kukimbiwa na wanaume.