Wanawake wanataka nini/What do women want?

Wanawake wanataka nini/What do women want?

amini msemo huu
"mwalimu wa wanawake ni kipofu"
Sikubaliani na wewe kwa asilimia nyingi kaka. Suala hapa ni kupenda, penzi linamea popote bila kujali uwezo. Sura, urefu n.k. Vinginevyo wakina Remmy wasingeoa wazungu tena wenye pesa. Wanasema money can't buy everything.
 
Hapa nakupa mia kwa mia siri anayo mwenyewe huwaa hawasemi yaan mtu anamuacha mtu wake meneja anaenda kwa choka mbaya mtaan watu bana
anachotaka mwanamke kwa mwanaume ni siri yake moyoni mwake.ndo mana havifanani!ila Mara nyingi wanawake tunapenda tupate wanaume wenye sifa zinazofanana na baba zetu iwapo baba ni mume mwema kwa mama yako.na ikitokea baba yako si baba mwema au alimtelekeza mama yako basi utapenda uwe na mume mwenye sifa tofauti na baba yako.
 
Ngoja wanawake waje waeleze hili
Cc: Kongosho, Fixed Point, lara1

Naandika hii hoja nikitafuta majibu yakinifu na ya msingi kutoka kwa wanawake pia wanaume wenye majibu sahihi uzi wangu nimeuliza wanawake wanataka nini?

Maana nimeangalia katika hili nimeshindwa kupata majibu.

Case study yetu ya swali hili itamlenga mke wa pili wa rais wa zamani wa Gabon Judith Lucien Bongo mwanamke huyu alikuwa mtoto wa Rais wa Congo Brazaville Rais Denis Sassou Nguesso akiwa msomi kabobea kwenye taaluma ya udaktari na pia ni mwanamke mzuri kwelikweli aliamua kuolewa na mwanaume anayemzidi takribani miaka 30

Pamoja na kuwa ni mtoto wa Rais Denis Sessou Nguesso kakulia kwenya mali na madaraka pia ana taaluma na ni mzuri anaweza olewa kwa kugombaniwa ukizingatia ni mtoto wa president ambaye hakuwa na ukomo wa kutawala lakini bado aliamua kuolewa na Rais wa nchi jirani ya Gabon akiwa mke wa pili na aliyemuoa akiwa na miaka 8 zaidi ya umri wa baba yake na akimzidi Judith miaka 29 na si kwamba ni handsome bali wa kawaida mwenye kimo cha futi 4 11" hata futi tano hafiki

Kwanini afanye vile? Angekuwa mtoto wa masikini tungeelewa, angekuwa hana taaluma tungeelewa,

angekuwa fukara tungeelewa, baba yake asingekuwa rais tungeelewa yaani kwanini aamue kuolewa na mzee vile kwa sababu tu mmewe ni Rais wakati na baba yake ni rais pia na kakulia ikulu?

Jamani naomba majibu yasiyo na mzaha nijue psychology ya hili swala ni nini haswa jibuni kwa kadri mjuavyo. Ahsanteni
 
Last edited by a moderator:
Ngoja wanawake waje waeleze hili
Cc: Kongosho, Fixed Point, lara1
swali lake kalikosea.....
badala ya kutuweka wooooteee kwenye chungu kimoja angeuliza kila mtu anataka nini.....
hata matakwa ya mtu huyo huyo mmoja yanatofautiana kulingana na muda, sehemu, na hali. takwa langu la sasa siyo la kesho wala la mwakani.
 
Nilipitiwa ilisharekebishwa nimeandika usiku natoka mechi ya Brazil vs Mexico nilikuwa na haraka ya kuandika bahati mbaya ukikosea title kuedit shughuli

Mkuu nimekusoma, hii inawezekana imesababishwa na golikipa wa Mexio.

BTT, ni vigumu kujenerolaiz na kukonkludi kiujumla kuwa mwanamke anataka nini. Wakati wewe unamshangaa huyo kuna wengi pia wanapigwa na butwaa kuwaona watoto wa kike wa matajiri wakiwa hoi na hawana la kusema kwa vijana wa kimaskini.... haya yanatokea sana. Hii inaweza kunikubalisha na mawazo ya wengi kuwa ukiondoa tamaa ya utajiri na usanii, mapenzi ya kweli hayana formula.

Hilo toto la rais inawezekana likawa limependa kweli kwakuwa mapenzi hayaangalii umri, lakini pia inawezekana lilishapata kila kitu ila kupewa attention na ulinzi, kusindikizwa na ving'ora na hadhi ya umama wa kwanza ni ndoto ambayo asingekuja kuipata kama asingekubali kuolewa na huyo kikongwe....
 
Jamani mbona Riz1 ana kifaa kikali alafu kirefu kuliko yeye.
By the way,its love maana hata wasira ana dem mdogo kuliko huyo waif wako.
 
Wanawake ni viumbe ambao hata Mungu amewazungumzia kwa kina sana, yaani kiukweli ni viumbe wa aina yake na ukitaka kuishi kwa amani achana na hiyo falsafa ya kutaka kujua wanawake wanahitaji nini, maana naamini hata wao wenyewe hawajui wanahitaji nini, leo anaweza kuhitaji kitu kimoja na kesho kingine na keshokutwa tofauti kabisa, kwa ujumla anachohitaji mwanamke ni fumbo la Muumba na mwanamke mwenyewe anayehitaji.
 
Mkuu nimekusoma, hii inawezekana imesababishwa na golikipa wa Mexio.

BTT, ni vigumu kujenerolaiz na kukonkludi kiujumla kuwa mwanamke anataka nini. Wakati wewe unamshangaa huyo kuna wengi pia wanapigwa na butwaa kuwaona watoto wa kike wa matajiri wakiwa hoi na hawana la kusema kwa vijana wa kimaskini.... haya yanatokea sana. Hii inaweza kunikubalisha na mawazo ya wengi kuwa ukiondoa tamaa ya utajiri na usanii, mapenzi ya kweli hayana formula.

Hilo toto la rais inawezekana likawa limependa kweli kwakuwa mapenzi hayaangalii umri, lakini pia inawezekana lilishapata kila kitu ila kupewa attention na ulinzi, kusindikizwa na ving'ora na hadhi ya umama wa kwanza ni ndoto ambayo asingekuja kuipata kama asingekubali kuolewa na huyo kikongwe....

Toka nimuone Peter Schmichel wa Manchester United akifuta magori ya wazi sijawahi ona kipa mwingine akifuta magori bali ni huyu wa Mexico ile mechi ilistahili kuwa sare na naamini ndio mechi bora kabisa mpaka sasa katika kombe hili la dunia
 
Back
Top Bottom