Wanawake waliomuacha huwa hawaolewi

Wanawake waliomuacha huwa hawaolewi

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,951
Nawasalimia wana JF

Niko na rafiki yangu wa karibu sana amenisimulia historia yake ya uhusiano na wanawake (sasa hivi ameoa na anawatoto wawili mapacha).

Alinieleza wanawake wote walio muacha kwa vituko wote hawajaolewa. Kanitajia kweli wote wapo wapo tu na umri wao sasa unaenda, na ukiwatazama wanahitaji sana japo wapate wenzi wao.

Sikuelewa sababu gani au imetokea tu. Jamaa kusema kweli huwa anajari, lakini katika maisha yake wanawake zaidi ya watatu walimwacha kwa visingizio eti kwamba hana mkwanja wakutosha.

Japo kuwa rafiki yangu wakati ule alikuwa na kazi ndogo iliyokuwa inamwingizia kipato.

Nimejaribu kuongea naye kuwa hiyo huenda ni jambo la kiroho zaidi, inabidi aende akaongee nao na awasamehe na kuwaachilia.

Yeye kasema alishawasamehe. Lakini nikamsisitiza awatafute aongee nao ili waeze kufunguliwa. Maana kinachoonekana kile walichokuwa wanakihitaji mpaka leo hii hawajakipata. Na wanahaha sasa na sura zao zinaanza kupoteza mvuto.

Mwana JF hebu toa nawewe ushauri hivi hii ni kweli inaweza kutokea?

Nawasilisha hoja.



 
Naona mnaangalia upande wa jamaa peke yake hebu chunguzeni na upande wa pili wa shilingi inawezekana wao pia hawajajisamehe na wanatafuta au wanafikiria ipo siku jamaa atarudi ndio maana wakitokewa na vi dume vingine utendaji wa kazi unakuwa zero au ni kweli kabisa wako zero kwenye utendaji ndio maana wanaonjwa na kuachwa ......
 
hamna kitu kibaya kama kumuacha mtu bila sababu(awe mme/mke)ni vyema kabla hujaanza relation na ufikirie na si uache kabisa pindi ukishaanza,uzoefu uliopo unaonesha wenzi wengi waliacha wenzi wao bila sababub za msingi au waliishi bila kuolewa,waliolewa wamechelewa sana,au waliolewa na ndoa zao hazikudumu,kamwe si busara kumwacha mtu without reasons habari ya uhusiano ni serious this should get into our brains!
 
mhhh majanga atakuwa mchawiii sio siri wanawake wawewanauliza kuingia ingia nako balaaa
 
Annael Tusikimbilie kwenye uchawi, inawezekana hao wanawake wake waliomuacha wana tabia za kuacha wanaume mara wanapogundua hana kipato au kipato kimeshuka na mwisho wa siku staili yao imewachelewesha kuolewa na mtaani wameonekana hawajatulia!
 
.....jibu lipo hapohapo, hawajapata wanaume wenye 'uwezo' waliojiwekea wao...

Watasubiri sana!
 
Labda ungesema hawajaolewa sio hawaolewi maana pengine mda waliopangiwa kuolewa haujafika

Kwani hao wanawake ni wangapi na ni mda gani umepita tangu aachane nao kumfanya aconclude kua hawaolewi?
 
Labda ungesema hawajaolewa sio hawaolewi maana pengine mda waliopangiwa kuolewa haujafika

Kwani hao wanawake ni wangapi na ni mda gani umepita tangu aachane nao kumfanya aconclude kua hawaolewi?
Ni wanawake kama watano hivi ni miaka tofauti tofauti. si chini ya miaka saba
 
Ni wanawake kama watano hivi ni miaka tofauti tofauti. si chini ya miaka saba

Basi ajue tu kwa karne hii a good man is hard to find.....na sio kila mwanamke yupo tayari kusettle for less than what she desire

Kuna tofauti kubwa kati ya delay na failure
 
mimi walioniacha wanataabika umasikin umewapiga adi wakataka kurudi tena nikakataa.

na sijawablock fb kila siku naweka picha nikila bata.
nchi mbalimbali za mbali. ili nizidi waumiza.

na wamekosa watu wa maana wanaishia kupata wa vijiwen siku 2 wanaachana.
 
Hakuna mapepo wala nini

Nachoweza changia tu hapa ni kuwa, mtu anaweza date mwanamme mwenye vigezo fulani, cut off grade ikawa ya juu
wakiachana anashindwa ku-cope na wengine anakuwa anawaona chai chai tu
Anakuja kumbuka kuwa, pamoja na yule wa awali hakuwa na pesa ila labda alikuwa na vigezo vingine vya juu zaidi

Kuna watu wana mipesa ila vichwa vya kuku, pesa peke yake haitoshi kumwingiza mtu ndoani.
 
How old are you?

mimi walioniacha wanataabika umasikin umewapiga adi wakataka kurudi tena nikakataa.

na sijawablock fb kila siku naweka picha nikila bata.
nchi mbalimbali za mbali. ili nizidi waumiza.

na wamekosa watu wa maana wanaishia kupata wa vijiwen siku 2 wanaachana.
 
^^
Awe wazi,,kuna nadhiri anawawekea ambazo wanaondoka pasina kuziondoa pamoja.
^^
 
Nawasalimia wana JF

Niko na rafiki yangu wa karibu sana amenisimulia historia yake ya uhusiano na wanawake (sasa hivi ameoa na anawatoto wawili mapacha).


Alinieleza wanawake wote walio muacha kwa vituko wote hawajaolewa. Kanitajia kweli wote wapo wapo tu na umri wao sasa unaenda, na ukiwatazama wanahitaji sana japo wapate wenzi wao.

Sikuelewa sababu gani au imetokea tu. Jamaa kusema kweli huwa anajari, lakini katika maisha yake wanawake zaidi ya watatu walimwacha kwa visingizio eti kwamba hana mkwanja wakutosha.

Japo kuwa rafiki yangu wakati ule alikuwa na kazi ndogo iliyokuwa inamwingizia kipato.

Nimejaribu kuongea naye kuwa hiyo huenda ni jambo la kiroho zaidi, inabidi aende akaongee nao na awasamehe na kuwaachilia.

Yeye kasema alishawasamehe. Lakini nikamsisitiza awatafute aongee nao ili waeze kufunguliwa. Maana kinachoonekana kile walichokuwa wanakihitaji mpaka leo hii hawajakipata. Na wanahaha sasa na sura zao zinaanza kupoteza mvuto.

Mwana JF hebu toa nawewe ushauri hivi hii ni kweli inaweza kutokea?

Nawasilisha hoja.



Umejuaje kama wanahitaji kuolewa, je kama walishaamua kuishi single? au labda bado wapo wapo hawajaamua kuolewa?
 
Back
Top Bottom