Kiongozi naomba ufafanue hapo bold kama hutojali..!
Mahusiano ya mtandaoni ni changamoto sana...ngoja wadau waje watiririke.....
hao wa huku mitandaoni si ndio hao hao wa mtaani
Mtizamo/maoni yako nimeyaelewa na pia hiyo mifano uliyotoa.''Online dating ni playground ya wasiojua kuwinda...''
Matamshi hayo ni kwa mujibu wa mtizamo wangu katika suala zima la sanaa ya utongozaji...
Wanadamu pamoja na utashi tulionao bado haituondolei sifa ya unyama kama walivyo wananyama wengine wawindao...
Utongozaji kwa mwanaume na mwanamke ni kama uwindaji ufanyikavyo yaani kuna 'prey' na 'predator'...
Mathalani simba hawezi kuwinda mnyama ambaye hajamtia machoni na kumfanyia tathmini kwa kumuona kwanza na hadi anapoamua kufukuza ujue ana uhakika wa kumkamata...
Fisi hafanyi hivyo na ndio maana huishia kula mizoga ambayo imesuswa na waliokwisha kushiba mawindo yao...
Ukiacha hilo pia utongozaji huambatana na lugha ya ulainishaji ambayo huwa na nguvu zaidi pale watendaji wa tendo hili wanapokua ana kwa ana...
Kuna lugha ambayo viungo vyetu huwa vinazungumza na lugha hii huwa ni muhimu sana kwenye kufanikisha azma ya utongozaji...
Hizi mbwembwe za kuwasiliana online, huja tu kama hatua zinazofuata kuimarisha au kujenga mahusiano zaidi na kutimiza azma kuu...
Mnanishangaza sana, kwani nikitongoza wa mtandaoni namuoa siku hiyo hiyo? Huwa nyie mnaotongoza wa kanisani mnafuata principle gani kuwaoa hao mnaowatongoza? Mnatongoza leo na kuoa kesho au mnatongoza na kufuata njia sahihi za urafiki, uchumba hadi kufikia ndoa? Don't be shortsighted watu wa mmu. Nimedate online na nimetafuta wa kanisani, niliachana na hao wa kanisani longiiii, nothing interesting from them, nimemuona mtu from jan-Dec sina ashki nae, nimtongoze wa nini? I fancy embarking on relationships online, na mahusiano nilioanzia online yamekuwa matamu kuliko hayo ya kukutana church, kwenye daladala na mtaani.
this handwriting??? i gues i know yuo G....