Wanawake: Ukimpenda mwanaume mtongoze

Hayo pia yapo kwa wanawake. Wengine wanakubali kumbe unafiki. Nenda saloon utajua kwamba haya unayosema nanyi mnayo..kwani tukiwatogoza huwa hamsemi?
 
Duh! Ila kweli wanaume tunatofautiana tabia na mtazamo lakini kwa sisi tulio starabika naona kawaida tu Kwa kuwa hata ww ni binadamu unapenda.
Au unatumia style ya kumtega hadi ajiongeze mwenyewe.
Teh kumtega tena ndo shida
 
Hayo pia yapo kwa wanawake. Wengine wanakubali kumbe unafiki. Nenda saloon utajua kwamba haya unayosema nanyi mnayo..kwani tukiwatogoza huwa hamsemi?
Hahaa lakini wewe kidume hata ukikubaliwa leo kinafiki na Ashura kesho ukaachwa ukaenda kwa Neema then Amina baadae Sarah haikuondolei sifa ya kuwa mwanaume sasa mimi mwanamke nikizurura hivyo tayari nimeshapachikwa jina la Malaya. Kuhusu kusema ni sawa ila mapokezi ya habari mwanamke kutongozwa haiwezi kuwa sawa na pale mtu anaposikia eti Khantwe katongoza kulingana na jamii yetu ilivyozoea
 
Tumekuwa conditioned na society tunazoishi. Kwasababu mnadai haki za wanawake na hilo liwekeni kwenye agenda maana linawanyima haki zenu za msingi. Sasa mpaka mtu utongozwe na unayempenda asipokuja. Halafu utamsikia binti eti sijapata chaguo langu. Anakuwaje chaguo kama hujalitatafuta? Kwahiyo wenye chaguo japo ni me na wala si ke.
 
Navumilia mkuu najitahidi kupambana na hali yangu baadae nazoea naanza kumuona kawaida ila sio rahisi
Aiseee! Vipi kama yy atajuaje Kwa muda ule kama usha mtamani ili aanze kuchangamkia fursa.
 
Mie mke wangu alikuwa na haibu sana kwangu....yaani ni mwanamke mzuri na alikuwa mcheshi sana kwa wengine ila kila aliponiona sehemu ghafla alikuwa anaishiwa nguvu na kubaki kunitizama tu hata kunisalimu alikuwa anashindwa. Siku ya siku tukakutana hana kwa hana, nikamshika mkono na kumsalimu akabaki anatetemeka na kuangalia chini. Nikamwambia najuwa unanipenda nami nakupenda, ghafla akageuka na kunikumbatia. Toka siku ile mpaka leo ni miaka 13, tuko na watoto 3 na tabasamu alituishi kila tukikumbuka.
 
Kabisa mkuu jamii tunayoishi ndo imetujenga hivyo. Ndio maana wanasema asilimia kubwa ya wanawake wanaolewa na mwanaume wasiowapenda
 
Waooh... How sweet
 
Safi sana hii
 
Waooh... How sweet


It is sweet, ila kwa kweli wanawake inawawia vigumu sana kutongoza. Let me tell you one thing ambacho nimegundua from experience ya mke wangu na mimi mwenyewe.....ukihisi una mfeel jamaa basi juwa kuna kitu (nguvu) kinawavutia mkutane, kama mwanamke unampenda mwanamme usihofu kukataliwa kwani ni moja ya maisha pia, wewe jitose tu na umweleze ukweli huyo mwanamme, kwa mwanamme LAZIMA atakuelewa tu na sie tuko wepesi sana kumuelewa mwanamke shinda nyie mnavyotudhania.
 
Ilikuwa bahati yake nae mkeo bwana lol I doesn't work with everyone aisee siwezi kabisa wacha nibaki na maumivu yangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…